Ruka hadi kwenye maudhui makuu

TRUMP AVUNZA MKATABA KUMKERA BARACK OBAMA SIRI HADHARANI



Barua mpya iliyovuja yadai Trump amevunja mkataba wa nyukilia 'ili kumkera Obama'



Rais Donald Trump ameachana na mkataba wa nyukilia wa Iran ili kumkera Barack Obama, hiyo ni kwa mujibu wa barua ya siri iliyovuja kutoka kwa aliyekuwa balozi wa Uingereza nchini Marekani.

Sir Kim Darroch alielezea hatua ya Trump kuvunja mkataba huo kama "ubadhirifu wa kidiplomasia" kwa mujibu wa gazeti la Mail on Sunday.

Gazeti hilo linadai kuwa barua hiyo iliandikwa baada ya aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Nje wa Uingereza Borris Johnson kuirai Marekani mwaka 2018 kusalia ndani ya makubaliano hayo.


Barua hii mpya inavuja katikakipindi ambacho polisis nchini Uingereza wameonya juu ya uchapishwaji wa barua hizo.

Barua ya kwanza kutoka kwa balozi huyo ambayo ilikuwa inakosoa utawala wa Trump ilivuja wiki moja iliyopita na kusababisha majibizano ya hasira baina ya Uingereza na Marekani.

Majibizano hayo yamesababisha Sir Kim kujiengua kwenye wadhifa wake licha ya serikali ya Uingereza kupitia Waziri Mkuu Theresa May kueleza kuwa inamuunga mkono.

Barua mpya iliyovuja inasema nini?

Gazeti la Mail on Sunday linaripoti kuwa Sir Kim alimwandikia Bw Johnson akimuelezea kuwa rais Trump kutoka chama cha Republican anavunja mkataba huo kwa sababu za "utashi binafsi" - kwa sababu makubaliano hayo yalifikiwa na mtangulizi wake kutoka chama cha Democrat, Barack Obama.

Kupitia mkataba huo, Iran ilikubali kuacha kurutubisha madini ya urani katika viwango vya kutilia mashaka na nchi za magharibi zikiongozwa na Marekani zikakubali kuiondolea nchi hiyo vikwazo vikali vya kiuchumi.


Trump alitangaza kuwa asingeshirikiana tena na Sir Kim Darroch (kulia) kabla ya balozi huyo kutangaza kujiuzulu Jumatano.

Hata hivyo, Trump alidai kuwa haamini kama makubaliano hayo yalisaidia kwa kina kuizuia Iran katika ndoto zake za kutengeneza silaha za nyuklia.Akaenda mbali zaidi kwa kurejesha vikwazo vya Marekani dhidi ya taifa hilo na kujitoa kwenye mkataba huo mwezi Mei 2018.

Balozi huyo wa Uingereza katika barua yake kwenda London inasemekana alieleza kuwa kulitokea mgawanyiko mkubwa miongoni mwa washauri wa rais Trump, na kuwa Ikulu ya White Haouse haikuwa na mpango thabiti wa kuliendea jambo hilo baada ya kujitoa kwenye makubaliano.



Katika barua hiyo, Sir Kim anadaiwa kuandika kuwa: "Matokeo yake ni kuwa kitendawili cha Ikulu ya White House kimeonekana: unaweza kumuona kila mtu kasoro rais mwenyewe: lakini katika uhalisia, utawala huu upo katika hali ya ubadhirifu wa kidiplomasia, kwa sababu za kiitikadi na utashi binafsi - maana yalikuwa ni makubaliano ya Obama.

"Na zaidi ni kuwa, hwana mpango thabiti wa baada ya kujitoa kwenye makubaliano; na vyanzo vyetu kutoka wizara ya mambo ya nje (ya Marekani) asubuhi hii vinaeleza kuwa hakuna mpango wowote wa kuwasiliana na washirika, iwe katika ukanda huu (Amerika) ama Ulaya."

Mzozo wa barua hizo umeendaje?


Sir Kim alijiuzulu ubalozi Jumatano akisema imekuwa ni vigumu kwake kuendelea na nafasi hiyo.

Barua ya kwanza kabisa iliyovuja ya Sir Kim, ilionesha kuwa balozi huyo akimuelezea Trump kama hakuwa mtu mwerevu na stadi.

Trump akajibu mapigo kwa kumita Sir Kim kuwa ni "mtu mpumbavu sana", na kuongeza kuwa asingeshirikiana naye tena.

Sir Kim alijivua wadhifa wake Jumatano akisema imekuwa ni vigumu kwake kuendelea na nafasi hiyo.

Johnson ambaye ndiye alikuwa akiandikiwa barua hizo kwa sasa ni mgombea wa nafasi ya Uwaziri Mkuu kupitia chama cha Conservative na ameshutumiwa vikali kwa kutoonesha kumuunga mkono hadharani Sir Kim kwenye mjadala wa runingawiki iliyopita.

Serikali ya Uingereza pia imeanzisha uchunguzi kujua imekuwaje barua hizo za siri zimevuja.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

MAPENZI: Kuna faida na ni muhimu Mpenzi wako kuwa rafiki yako pia

Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi.  Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria.  Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao.  Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...

Urusi: Vikwazo dhidi ya Korea Kaskazini havitafua dafu

MTEULE THE BEST Image caption Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Sergei Lavrov na mwenzeka wa Marekani Rex Tillerson Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Segei Lavrov amemwambia waziri wa ulinzi nchini Marekani Rex Tillerson kwamba kuiwekea vikwazo zaidi Korea Kaskazini hakutafua dafu. Taarifa iliochapishwa na wizara ya kigeni nchini Urusi inasema kuwa wawili hao walizungumza kwa njia ya simu na kushutumu majaribio ya makombora ya hivi karibuni yaliotekelezwa na Pyongyang . Lakini inasema kuwa bwana Lavrov alisisitiza kwamba diplomasia ndio njia ya pekee ya kumaliza wasiwasi katika rasi ya Korea, na kutaka hatua zozote dhidi ya taifa hilo kusitishwa akionya huenda zikasababisha madhara yasiojulikana. Waziri wa ulinzi nchini Marekani amesisitiza kuwa bado kuna fursa ya kidiplomasia katika kukabiliana na Korea Kaskazini. Mapema rais Trump alichapisha ujumbe katika akaunti yake ya Twitter akisema mazungumzo sio suluhisho.

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania Miaka 60 siku kama ya leo ugunduzi mkubwa ulifanyika katika eneo la Olduvai Gorge, kwenye kreta ya Ngorongoro. Wanaakiolojia Louis na Mary Leakey waligundua fuvu la mtu anayeaminika kuwa ni wa kale zaidi waliyompa jina la Zinjanthropus. Ugunduzi huo uliofanyika saa nne asubuhi Julai 22, 1959 kipindi hicho kwenye eneo la Tanganyika ulikuwa wa vipande zaidi ya 100 ukasaidia katika kutambua asili ya watu wa awali duniani. Kabla ya ugunduzi huo, wanasayansi na wanahistoria walikuwa wakiamini kuwa binadamu wa kale walitokea Uchina baada ya ugunduzi wa mafuvu ya kale baina ya 1923 na 1927 nchini humo ya Homo eractus, ama maarufu kama Peking Man. Mafuvu hayo ya Uchina yalikuwa na umri wa takribani miaka 750,000. Mafuvu ya Olduvai eneo ambalo kwa sasa lipo Tanzania wakati wa ugunduzi wake lilikuwa na umri wa takribani miaka milioni 1.75, na hakuna mabaki ya mtu wa kale zaidi ambayo mpaka sasa yamegundul...