Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Tetesi za Soka Ulaya Jumapili

Tetesi za Soka Ulaya Jumapili 14.07.2019: Nyemar, Odoi, Pogba, Coutinho, Maguire, Mane




Neymar alijiunga na PSG kutoka Barcelona kwa dau lililovunja rekodi la pauni milioni 200 mwaka 2017

Mchezaji ghali zaidi duniani wa Paris St-Germain, Neymar, amekoleza uvumi kuwa anarudi Barcelona baada ya kuachia video anayoonekana amevaa jezi ya Barca, pamoja na mistari ya biblia yenye mafumbo. (Goal.com)


Bayern Munich hawatakata tamaa ya kumsajili mshambuliaji kinda wa Chelsea Callum Hudson-Odoi, 18, huku wakitarajiwa kutangaza dau la pauni milioni 45 wiki hii. (Mail)

Liverpool pia wamejiunga kwenye mbio za kinyang'anyiro cha kutaka kumsajili mshambuliaji wa CSKA Moscow Fedor Chalov mwenye thamani ya pauni milioni 20. Arsenal, Manchester City, Tottenham, Chelsea na Manchester United pia wanamnyemelea mchezaji huyo mwenye miaka 21. (Mirror)


Barcelona ilimsajili Coutinho kutoka Liverpool kwa pauni milioni 142 Januari 2018

Kiungo wa Barcelona Philippe Coutinho, 27, atakataa ofa ya kujiunga na Manchester United, akiwa na malengo ya kuelekea klabu Paris St-Germain, japo anaweza pia kukubali kurejea Liverpool.(Express)

Barcelona wamemuhakikishia wakala wa Coutinho kuwa hawana mpango wa kumuuza mchezaji huyo, japo anadai kuwa mteja wake anawekwa sokoni na wawakilishi walio karibu kabisa na klabu hiyo. (Sky Sports)

Manchester United hawatamuuza kiungo Mfaransa Paul Pogba kwenda Real Madrid iwapo miamba hiyo ya Uhispania watawasilisha ofa yao baada ya dirisha la usajili kufungwa kwa upande wa England, Agosti 8. (Mirror)

Beki wa Leicester na England Harry Maguire, 26 - ambaye anahusishwa na uhamisho kwenda Man United kwa dau la Ā£75m - ameambia klabu yake kuwa anataka kuondoka. (Mail)


Maguire ametia nia ya kuihama Leicester kwenye dirisha hili la usajili

Maguire ameishutumu Leicester kwa kumkadiria kwa dau ghali ili asinunulike. Tayari klabu hiyo imeshazikataa ofa za pauni milioni 70 kutoka kwa United na City. (Sun)

Kiungo mchezeshaji wa Tottenham na timu ya taifa ya Denmark Christian Eriksen, 27, yawezekana akaendelea kusalia kwenye klabu hiyo ya jijini London baada ya kuwa na uhaba wa klabu ambazo zimeonesha nia ya kumsajili. (Guardian)


Sadio Mane kung'oka Liverpool?

Liverpool hawajafanya mazungumzo yoyote na Real Madrid juu ya mshambuliaji raia wa Senegal Sadio Mane, 27, licha ya mkuu wa chama cha soka cha Senegal Saer Seck kudai kuwa Madrid wamepeleka ofa ya usajili. (Liverpool Echo)

Kiungo wa Everton na Senegal Idrissa Gueye, 29, amesema anafahamu juu ya tetesi zinazomhusisha na uhamisho kwenda PSG lakini kwa sasa amedai malengo yake yapo AFCON. (Sport Witness)

Arsenal wapo Tayari kuminyana na Tottenham na Juventus katika mbi za kumsajili kiungo waklabu ya Roma ya Italia Nicolo Zaniolo, 20. (Calciomercato)

Liverpool pia wamejiunga kwenye mbio za kinyang'anyiro cha kutaka kumsajili mshambuliaji wa CSKA Moscow Fedor Chalov mwenye thamani ya pauni milioni 20. Arsenal, Manchester City, Tottenham, Chelsea na Manchester United pia wanamnyemelea mchezaji huyo mwenye miaka 21. (Mirror)

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

MAPENZI: Kuna faida na ni muhimu Mpenzi wako kuwa rafiki yako pia

Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi.  Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria.  Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao.  Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...

Urusi: Vikwazo dhidi ya Korea Kaskazini havitafua dafu

MTEULE THE BEST Image caption Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Sergei Lavrov na mwenzeka wa Marekani Rex Tillerson Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Segei Lavrov amemwambia waziri wa ulinzi nchini Marekani Rex Tillerson kwamba kuiwekea vikwazo zaidi Korea Kaskazini hakutafua dafu. Taarifa iliochapishwa na wizara ya kigeni nchini Urusi inasema kuwa wawili hao walizungumza kwa njia ya simu na kushutumu majaribio ya makombora ya hivi karibuni yaliotekelezwa na Pyongyang . Lakini inasema kuwa bwana Lavrov alisisitiza kwamba diplomasia ndio njia ya pekee ya kumaliza wasiwasi katika rasi ya Korea, na kutaka hatua zozote dhidi ya taifa hilo kusitishwa akionya huenda zikasababisha madhara yasiojulikana. Waziri wa ulinzi nchini Marekani amesisitiza kuwa bado kuna fursa ya kidiplomasia katika kukabiliana na Korea Kaskazini. Mapema rais Trump alichapisha ujumbe katika akaunti yake ya Twitter akisema mazungumzo sio suluhisho.

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania Miaka 60 siku kama ya leo ugunduzi mkubwa ulifanyika katika eneo la Olduvai Gorge, kwenye kreta ya Ngorongoro. Wanaakiolojia Louis na Mary Leakey waligundua fuvu la mtu anayeaminika kuwa ni wa kale zaidi waliyompa jina la Zinjanthropus. Ugunduzi huo uliofanyika saa nne asubuhi Julai 22, 1959 kipindi hicho kwenye eneo la Tanganyika ulikuwa wa vipande zaidi ya 100 ukasaidia katika kutambua asili ya watu wa awali duniani. Kabla ya ugunduzi huo, wanasayansi na wanahistoria walikuwa wakiamini kuwa binadamu wa kale walitokea Uchina baada ya ugunduzi wa mafuvu ya kale baina ya 1923 na 1927 nchini humo ya Homo eractus, ama maarufu kama Peking Man. Mafuvu hayo ya Uchina yalikuwa na umri wa takribani miaka 750,000. Mafuvu ya Olduvai eneo ambalo kwa sasa lipo Tanzania wakati wa ugunduzi wake lilikuwa na umri wa takribani miaka milioni 1.75, na hakuna mabaki ya mtu wa kale zaidi ambayo mpaka sasa yamegundul...