Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Tetesi za Soka Ulaya Jumanne 16.07.2019

Tetesi za Soka Ulaya Jumanne 16.07.2019:Maguire, Neymar, Bruce, Fernandes, Alderweireld, Coutinho



Leicester imemwambia mlinzi wake wa kati Harry Maguire, 26, kuwa anaweza kuondoka (Telegraph)

Mshambuliaji wa Paris St-Germain Neymar, 27, amerejelea kauli yake uhusu nia yake ya kuondoka kwenye klabu hiyo kwenye mkutano wake na mkurugenzi wa ufundi Leonardo . (ESPN)

Newcastle watalipa pauni milioni 4 kama fidia kwa timu ya Sheffield Wednesday kwa ajili ya kocha wao wa zamani Steve Bruce.(Sun)

Wasaidizi wa Bruce Steve Agnew na Stephen Clemence pia wameondoka Sheffield Wednesday na watajiunga naye St James'Park .(Newcastle Chronicle)

Manchester United watapeleka rasmi ofa ya kumnasa kiungo wa kati wa Sporting Lisbon Bruno Fernandes, 24, katika kipindi cha majuma matatu yajayo.

Mkurugenzi wa Roma Gianluca Petrachi amethibitisha kuwa klabu yake ina mpango wa kumsajili mchezaji wa nafasi ya ulinzi wa Tottenham Toby Alderweireld, 30. (Football Italia)

Alderweireld na mchezaji mwenzake Christian Eriksen, 27, wanajiandaa kusafiri kwenda Singapore na klabu siku ya Jumatano, ingawa kumekuwa na maswali kuhusu mustakabali wao.(London Evening Standard)

Kiungo wa Barcelona Philippe Coutinho, 27, huenda akarejea Liverpool kwa mkataba wa miaka miwili kwa mkopo, huku timu hiyo yenyewe ikiwa na mipango ya kumnunua kwa pauni milioni 88.(Calciomercato, via Sport Bible)

Bayern Munich imekata matumaini ya kumalizia dili la pauni milioni mmoja kumnasa winga wa Manchhester City Leroy Sane, 23.(Sky Germany, via Mail)

Arsenal imeendelea kuwa na mazungumzo na Celtic kuhusu dili la kumpata beki wa kushoto Kieran Tierney .(London Evening Standard)

Inter Milan wana shaka kuhusu kitita cha pauni milioni 75 Manchester United inakihitaji kwa ajili ya mshambuliaji wa Ubelgiji Romelu Lukaku.Inter imetoa ombo la mkopo wa miaka miwili, ambapo wataweza kulipa kwa awamu za Pauni milioni 9, pauni milioni 27 na pauni milioni 27, lakini United wanataka fedha zote kwa mkupuo. (Star)

West Ham wako kwenye mazungumzo wakitaka saini ya mshambuliaji Sebastien Haller, 25. (London Evening Standard)

Wolves wako na mipango ya kumsajili Wallace, 24,mlinzi wa Lazio (Birmingham Mail)

Gatasaray wanakabiliwa na ushindani kutoka kwa magwiji wa ligi ya Serie A, AC Milan ili kumpata kiungo wa Fulham Jean Mchael Seri, 27 . (Fanatik, via Sport Witness)

Kocha wa zamani wa Manchester United Jose Mourinho anatazama uwezekano wa kuhamia Bundesliga. (Independent)

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

MAPENZI: Kuna faida na ni muhimu Mpenzi wako kuwa rafiki yako pia

Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi.  Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria.  Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao.  Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...

Urusi: Vikwazo dhidi ya Korea Kaskazini havitafua dafu

MTEULE THE BEST Image caption Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Sergei Lavrov na mwenzeka wa Marekani Rex Tillerson Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Segei Lavrov amemwambia waziri wa ulinzi nchini Marekani Rex Tillerson kwamba kuiwekea vikwazo zaidi Korea Kaskazini hakutafua dafu. Taarifa iliochapishwa na wizara ya kigeni nchini Urusi inasema kuwa wawili hao walizungumza kwa njia ya simu na kushutumu majaribio ya makombora ya hivi karibuni yaliotekelezwa na Pyongyang . Lakini inasema kuwa bwana Lavrov alisisitiza kwamba diplomasia ndio njia ya pekee ya kumaliza wasiwasi katika rasi ya Korea, na kutaka hatua zozote dhidi ya taifa hilo kusitishwa akionya huenda zikasababisha madhara yasiojulikana. Waziri wa ulinzi nchini Marekani amesisitiza kuwa bado kuna fursa ya kidiplomasia katika kukabiliana na Korea Kaskazini. Mapema rais Trump alichapisha ujumbe katika akaunti yake ya Twitter akisema mazungumzo sio suluhisho.

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania Miaka 60 siku kama ya leo ugunduzi mkubwa ulifanyika katika eneo la Olduvai Gorge, kwenye kreta ya Ngorongoro. Wanaakiolojia Louis na Mary Leakey waligundua fuvu la mtu anayeaminika kuwa ni wa kale zaidi waliyompa jina la Zinjanthropus. Ugunduzi huo uliofanyika saa nne asubuhi Julai 22, 1959 kipindi hicho kwenye eneo la Tanganyika ulikuwa wa vipande zaidi ya 100 ukasaidia katika kutambua asili ya watu wa awali duniani. Kabla ya ugunduzi huo, wanasayansi na wanahistoria walikuwa wakiamini kuwa binadamu wa kale walitokea Uchina baada ya ugunduzi wa mafuvu ya kale baina ya 1923 na 1927 nchini humo ya Homo eractus, ama maarufu kama Peking Man. Mafuvu hayo ya Uchina yalikuwa na umri wa takribani miaka 750,000. Mafuvu ya Olduvai eneo ambalo kwa sasa lipo Tanzania wakati wa ugunduzi wake lilikuwa na umri wa takribani miaka milioni 1.75, na hakuna mabaki ya mtu wa kale zaidi ambayo mpaka sasa yamegundul...