Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Mataifa ya Ghuba yasema yako tayari kuzungumza na Qatar

MTEULE THE BEST

Bahrain AuƟenminister von VAE, Saudi Arabien und Ƅgypten (picture-alliance/abaca/Stringer)

Mataifa manne ya Kiarabu yaliovunja uhusiano na Qatar yamesema yako tayari kwa mazungumzo ya kutatua mzozo huo ikiwa Doha itaonyesha nia ya kushughulikia madai yao. Qatar imesema huo ni upotoshaji wa jamii ya kimataifa.
Kundi la mataifa hayo linaloongozwa na Saudi Arabia lilikata mahusiano na Qatar Juni 5, wakiituhumu kwa kuyaunga mkono makundi ya wanamgambo na kushirikiana na hasimu wao mkuu wa kikanda  Iran, madai ambayo serikali mjini Doha inayakanusha vikali.
Juhudi za kidiplomasia za Kuwait na zinazoungwa mkono na mataifa ya magharibi zimeshindwa mpaka sasa kukomesha mzozo huo, ambao unahusisha kuwekewa vikwazo vya usafiri na mawasiliano Qatar  na mataifa hayo manne.
Wasema Qatar haina ni ya kusuluhisha
Saudi Arabi na washirika wake awali walitoa orodha ya  madai 13 kwa Qatar, ambayo yanahusisha kuitaka nchi hiyo kukomesha uungaji wake mkono kwa kundi la Udugu wa Kiislamu, kufunga kituo cha Televishen cha Al Jazeera chenye makao yake mjini Doha, kufunga kambi ya kijeshi ya Uturuki, na kushusha kiwango cha uhusiano na adui wa mataifa ya Ghuba Iran.
Katar AuƟenminister von Saudi Arabien Adel bin Ahmed Al-Jubeir in Manama (Reuters/H. I. Mohammed)
Waziri wa mambo ya nje wa Saudi Arabia Adel bin Ahmed Al-Jubeir akizungumza na waandishi habari mjini Manama Jumapili, 30.07.2017.
Waziri wa mambo ya nje wa Saudi Arabia Adel Al-Jubeir alisema Qatar haikuwa na nia ya kutekeleza matakwa hayo. "Tuko tayari kuzungumza na Qatar kuhusu utekelezaji wa matakwa, kuhusu utekelezaji wa kanuni, ikiwa Qatar ina nia, lakini imekuwa dhahiri kwamba haiko tayari," alisema waziri huyo katika mkutano na waandishi wa habari.
Mataifa hayo manne pia yameorodhesha kanuni sita wanzotaka Qatar itekeleze. Waziri wa mambo ya nje wa Qatar Sheikh Mohammed bin Abdurlrahman Al-Thani alipinga tamko la Jumapili kutoka kwa mataifa hayo na kusema vikwazo walivyoikwekea nchi yake vinakwenda kinyume na sheria za kimataifa.
Al-Thani alisema katika mahojiano na kituo cha Al Jazeera kwamba hakukuwa na dira ya wazi kutoka mkutano wa Manama, na kwamba kilichopo ni sera korofi kutoka mataifa yanayoizingira nchi yake na kukataa kwao kukiri kuwa hatua hizo ni haramu. Mapema Jumapili, gazeti la la al-Hayat lilisema likizinukuu duru zisizotajwa kutoka Ghuba, kwamba mataifa hayo manne yalitarajiwa kuweka vikwazo ambavyo taratibu vitaathiri uchumi wa Qatar.
Malumbano kuhusu Mahujjaji wa Qatar
Saudi Arabia imefunga mpaka wake wa nchi kavu na Qatar, huku mataifa yote manne yakikata mawasiliano ya angani na baharini na Doha, wakiitaka nchi hiyo inayosafirisha nishati ya gesi kwa wingi kuchukuwa hatua kadhaa kuonyesha inabadilisha sera zake.
Katar - Scheich Tamim bin Hamad Al Thani (Reuters/Qatar News Agency)
Mfalme wa Qatar, Sheikh Tamim bin Hamad al-Thani wakati akitoa hotuba kwa njia ya Televisheni mjini Doha, Qatar, Julai 21,2017.
Qatar imeituhumu Saudi Arabia kwa kuhatarisha safari ya hijja kwa raia wake kwa kukataa kuwahakikisha usalama wao. Julai 20 Saudi Arabia ilisema Waqatari wanaotaka kufanya hijja mwaka huu wataruhusiwa kuingia nchini humo, lakini ikaweka masharti fulani. Wizara ya Hajji ya Saudia ilisema Mahujjaji wa Qatar wanaowasili kwa ndege laazima watumie zinazokubaliana na Riyadh.
Pia watapaswa kuomba viza waakti wa kuwasili Jedda au Madina, ambavyo ndiyo vituo pekee kwao kuingilia katika taifa hilo la Kifalme. Kwa mujibu wa taarifa ya wizara ya masuala ya Kiislamu ya Qatar, raia 20,000 wa nchi hiyo wamejiandikisha kushiriki katika ibada ya hijja mwaka huu

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

MAPENZI: Kuna faida na ni muhimu Mpenzi wako kuwa rafiki yako pia

Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi.  Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria.  Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao.  Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...

Urusi: Vikwazo dhidi ya Korea Kaskazini havitafua dafu

MTEULE THE BEST Image caption Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Sergei Lavrov na mwenzeka wa Marekani Rex Tillerson Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Segei Lavrov amemwambia waziri wa ulinzi nchini Marekani Rex Tillerson kwamba kuiwekea vikwazo zaidi Korea Kaskazini hakutafua dafu. Taarifa iliochapishwa na wizara ya kigeni nchini Urusi inasema kuwa wawili hao walizungumza kwa njia ya simu na kushutumu majaribio ya makombora ya hivi karibuni yaliotekelezwa na Pyongyang . Lakini inasema kuwa bwana Lavrov alisisitiza kwamba diplomasia ndio njia ya pekee ya kumaliza wasiwasi katika rasi ya Korea, na kutaka hatua zozote dhidi ya taifa hilo kusitishwa akionya huenda zikasababisha madhara yasiojulikana. Waziri wa ulinzi nchini Marekani amesisitiza kuwa bado kuna fursa ya kidiplomasia katika kukabiliana na Korea Kaskazini. Mapema rais Trump alichapisha ujumbe katika akaunti yake ya Twitter akisema mazungumzo sio suluhisho.

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania Miaka 60 siku kama ya leo ugunduzi mkubwa ulifanyika katika eneo la Olduvai Gorge, kwenye kreta ya Ngorongoro. Wanaakiolojia Louis na Mary Leakey waligundua fuvu la mtu anayeaminika kuwa ni wa kale zaidi waliyompa jina la Zinjanthropus. Ugunduzi huo uliofanyika saa nne asubuhi Julai 22, 1959 kipindi hicho kwenye eneo la Tanganyika ulikuwa wa vipande zaidi ya 100 ukasaidia katika kutambua asili ya watu wa awali duniani. Kabla ya ugunduzi huo, wanasayansi na wanahistoria walikuwa wakiamini kuwa binadamu wa kale walitokea Uchina baada ya ugunduzi wa mafuvu ya kale baina ya 1923 na 1927 nchini humo ya Homo eractus, ama maarufu kama Peking Man. Mafuvu hayo ya Uchina yalikuwa na umri wa takribani miaka 750,000. Mafuvu ya Olduvai eneo ambalo kwa sasa lipo Tanzania wakati wa ugunduzi wake lilikuwa na umri wa takribani miaka milioni 1.75, na hakuna mabaki ya mtu wa kale zaidi ambayo mpaka sasa yamegundul...