Ruka hadi kwenye maudhui makuu

TETESI ZA SOKA ULAYA JUMAMOSI 05.08.2017

MTEULE THE BEST

Chelsea wameripotiwa kuwasiliana na Paris Saint-Germain kutaka kumsajili beki Serge Aurier, 24, huku kukiwa na taarifa kuwa mchezaji huyo wa kimataifa wa Ivory Coast anakaribia kujiunga na Manchester United. (Manchester Evening News)

Inter Milan wanataka kuwapiku Manchester United na Chelsea katika kumsajili beki Serge Aurier wa PSG. (Calciomercato)

Meneja wa Monaco Leonardo Jardim amedokeza kuwa Kylian Mbappe, 18, anayenyatiwa na Real Madrid, Manchester City, Barcelona na Arsenal, huenda akaondoka kabla ya dirisha la usajili kufungwa. (Independent)

Philippe Coutinho, 25, ameachwa katika kikosi cha Liverpool kitakachocheza na Athletic Bilbao siku ya Jumamosi kwa sababu ya jeraha la mgongo. Mchezaji huyo ananyatiwa na Barcelona ili kuziba nafasi ya Neymar. (Mirror)

Barcelona wamewasiliana na Borussia Dortmund kuhusu mchezaji wa kimataifa wa Ufaransa Ousmane Dembele, 20, ili kuchukua nafasi ya Neymar. (Daily Mail)

Ousmane Dembele amesema anakaribisha taarifa za yeye kuhusishwa na kuhamia Barcelona. (Metro)

Barcelona nao wamejiunga katika mbio za kutaka kumsajili winga wa Monaco Thomas Lemar anayenyatiwa na Arsenal. (Lā€™Equipe)

Mshambuliaji wa Real Madrid Cristiano Ronaldo, 32, amekiri kuwa angependa kurejea England, wakati akizungumza mahakamani kwenye kesi yake ya tuhuma za kukwepa kodi nchini Uhispania. (Cadena SER)

Real Madrid watafikiria kumuuza winga Gareth Bale, 28, kwenda Manchester United, lakini ikiwa tu kipa David De Gea atahusishwa katika mkataba huo. (Don Balon)

Gareth Bale amemuambia mchezaji mwenzake Luka Modric kuwa anataka kurejea England na kujiunga na Manchester United. (Don Balon)

Paris Saint-Germain baada ya kumsajili Neymar, sasa wanataka kupambana na Arsenal katika kumsajili kiungo wa Nice Jean Michael Seri, 26. (Metro)

Monaco wapo tayari kupanda dau la pauni milioni 45 kumtaka mshambuliaji wa Arsenal Alexis Sanchez, 28. (Sun)

Meneja wa Chelsea Antonio Conte imeripotiwa yuko tayari kumruhusu beki Andreas Christensen, 21, kwenda Inter Milan ili kubadilishana na winga Antonio Candreva, 30. (Tuttosport)
Kiungo wa Leicester City Danny Drinkwater yuko tayari kuiambia klabu yake kuwa anataka kuondoka na kujiunga na Chelsea. (Mirror)

Chelsea wamekanusha habari kuwa Antonio Conte anamtoa kwa nguvu Diego Costa, 28, Stamford Bridge. (Independent)

AC Milan wanafikiria kumchukua mshambuliaji wa zamani wa Manchester United na Chelsea Radamel Falcao, 31. (Sky Sport Italia)

Kiungo wa Inter Milan Geoffrey Kongodbia, 26, anayesakwa na Liverpool na Tottenham, ameomba kuondoka katika klabu yake. (Gazzetta dello Sport)

Everton huenda wakalipa pauni milioni 50 ambayo itavunja rekodi ya klabu ili kumsajili kiungo wa Swansea Gylfi Sigurdsson, 27. (The Times)

Watford wanamtaka beki wa Liverpool Alberto Moreno, 25, baada ya Liverpool kukataa dau la pauni milioni 11 kutoka Napoli. (Liverpool Echo)..

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

MAPENZI: Kuna faida na ni muhimu Mpenzi wako kuwa rafiki yako pia

Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi.  Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria.  Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao.  Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...

Urusi: Vikwazo dhidi ya Korea Kaskazini havitafua dafu

MTEULE THE BEST Image caption Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Sergei Lavrov na mwenzeka wa Marekani Rex Tillerson Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Segei Lavrov amemwambia waziri wa ulinzi nchini Marekani Rex Tillerson kwamba kuiwekea vikwazo zaidi Korea Kaskazini hakutafua dafu. Taarifa iliochapishwa na wizara ya kigeni nchini Urusi inasema kuwa wawili hao walizungumza kwa njia ya simu na kushutumu majaribio ya makombora ya hivi karibuni yaliotekelezwa na Pyongyang . Lakini inasema kuwa bwana Lavrov alisisitiza kwamba diplomasia ndio njia ya pekee ya kumaliza wasiwasi katika rasi ya Korea, na kutaka hatua zozote dhidi ya taifa hilo kusitishwa akionya huenda zikasababisha madhara yasiojulikana. Waziri wa ulinzi nchini Marekani amesisitiza kuwa bado kuna fursa ya kidiplomasia katika kukabiliana na Korea Kaskazini. Mapema rais Trump alichapisha ujumbe katika akaunti yake ya Twitter akisema mazungumzo sio suluhisho.

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania Miaka 60 siku kama ya leo ugunduzi mkubwa ulifanyika katika eneo la Olduvai Gorge, kwenye kreta ya Ngorongoro. Wanaakiolojia Louis na Mary Leakey waligundua fuvu la mtu anayeaminika kuwa ni wa kale zaidi waliyompa jina la Zinjanthropus. Ugunduzi huo uliofanyika saa nne asubuhi Julai 22, 1959 kipindi hicho kwenye eneo la Tanganyika ulikuwa wa vipande zaidi ya 100 ukasaidia katika kutambua asili ya watu wa awali duniani. Kabla ya ugunduzi huo, wanasayansi na wanahistoria walikuwa wakiamini kuwa binadamu wa kale walitokea Uchina baada ya ugunduzi wa mafuvu ya kale baina ya 1923 na 1927 nchini humo ya Homo eractus, ama maarufu kama Peking Man. Mafuvu hayo ya Uchina yalikuwa na umri wa takribani miaka 750,000. Mafuvu ya Olduvai eneo ambalo kwa sasa lipo Tanzania wakati wa ugunduzi wake lilikuwa na umri wa takribani miaka milioni 1.75, na hakuna mabaki ya mtu wa kale zaidi ambayo mpaka sasa yamegundul...