Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Kampuni iliomsadia Trump, ''yamfanyia kazi'' rais Kenyatta

MTEULE THE BEST

Rais Uhuru Kenyatta wa Kenya
Rais Uhuru Kenyatta wa Kenya
Kampuni moja ya data ya mitandaoni iliomfanyia kazi Donald Trump na ambayo ilitumika katika kampeni za Brexit sasa imeripotiwa kumfanyia kazi rais wa Kenya Uhuru Kenyatta.
Lengo la Cambridge Analytica ni wazi. Katika Mtandao wake kampuni hiyo inasema inatumia data kubadili tabia ya wateja wake.
Kampuni hiyo iliokodishwa na kundi la kampeni za rais Trump imepongezwa kwa ushindi wa rais huyo.
Kampuni hiyo inanunua na kukusanya data kuhusu wapiga kura ikiwemo historia ya utumizi wao wa mtandao, mahali walipo pamoja na 'Likes' zao {wanachopenda} katika mtandao wa facebook.
    Katika mtandao wake, Cambridge Analytica inadai kukusanya maeneo 5,000 ya data miongoni mwa wapiga kura milioni 320 wa Marekani.
    Zinapochanganywa pamoja na utafiti unaofanywa , Cambridge Analytica inaweza kutumia data hiyo kutoa ujumbe muhimu kwa wapiga kura.
    Kwa sasa Cambridge Analytica inafanya kazi Kenya , ikisaidia juhudi za kuchaguliwa tena kwa rais Uhuru kenyatta.
    Rais Uhuru Kenyatta kushoto na Donald Trump katikati
    Rais Uhuru Kenyatta kushoto na Donald Trump katikati
    Mnamo mwezi Mei , gazeti la The Star nchini Kenya liliripoti kwamba Chama cha rais Kenyatta, Jubilee kimekodisha kampuni hiyo , na mwezi mmoja baadaye ,gazeti hilo hilo liliripoti kwamba Cambridge Analytica ilikuwa ikifanya kazi katika ghorofa ya 7 ya jumba la makao makuu ya chama hicho jijini Nairobi.
    Cambridge Analytica ilikataa kutoa tamko lolote kuhusu ripoti hizo kwa kitengo cha habari cha BBC Trending, lakini shirika la Privacy International lilithibitisha kwamba liliona habari kama hizo katika gazeti la The Star kufuatia duru kadhaa, na kusema kuwa Cambridge Analytica inalipwa dola milioni sita kwa kazi yake nchini humo.
    Cambridge Analytica ilishirikishwa katika siasa za Kenya 2013 wakati kampuni hiyo ilipomsaidia Kenyatta na chama cha National Alliance ambacho kilibadilika na kuwa Jubilee
    Wakati wa kampeni za mwaka huo kampuni hiyo ilichanganya data ya mitandaoni na tafiti 47,000.
    Kulingana na mtandao wa Analytica hatua hiyo iliisaidia kampuni hiyo kutengeza maelezo mafupi ya mpiga kura wa Kenya na kutafuta mikakati ya kampeni inayolingana na mahitaji ya mpiga kura mbali na hofu ya kuzuka kwa ghasia za kikabila.
    Kenyatta alishinda uchaguzi huo wa 2013.
    Wakenya ni miongoni mwa watu wanaotumia sana mtandao barani Afrika.
    Idadi ya watu wanaotumia simu za rununu nchini humo iliongezeka kutoka watu milioni nane 2007 hadi milioni 30, 2013 na asilimia 88 ya idadi ya watu sasa wanaweza kutumia mtandao kupitia simu zao.
    Baada ya kuhudumu kama waziri wa habari na mawasiliano kutoka 2005 hadio 2013 , Bitange Ndemo alikuwa mmoja wa viongozi waliosadia kupanua sekta ya teknolojia.
    Aliambia BBC Trending kwamba mitandao ya kijamii ina jukumu kubwa katika kampeni za uchaguzi nchini humo.
    ''Inatoa njia ya haraka ya kujibu propaganda za mpinzani wako'' , alisema, mbali na kuwa mfumo wa mawasiliano unaoweza kuwafikia vijana wengi.

    Maoni

    Machapisho maarufu kutoka blogu hii

    MAPENZI: Kuna faida na ni muhimu Mpenzi wako kuwa rafiki yako pia

    Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi.  Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria.  Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao.  Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...

    Urusi: Vikwazo dhidi ya Korea Kaskazini havitafua dafu

    MTEULE THE BEST Image caption Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Sergei Lavrov na mwenzeka wa Marekani Rex Tillerson Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Segei Lavrov amemwambia waziri wa ulinzi nchini Marekani Rex Tillerson kwamba kuiwekea vikwazo zaidi Korea Kaskazini hakutafua dafu. Taarifa iliochapishwa na wizara ya kigeni nchini Urusi inasema kuwa wawili hao walizungumza kwa njia ya simu na kushutumu majaribio ya makombora ya hivi karibuni yaliotekelezwa na Pyongyang . Lakini inasema kuwa bwana Lavrov alisisitiza kwamba diplomasia ndio njia ya pekee ya kumaliza wasiwasi katika rasi ya Korea, na kutaka hatua zozote dhidi ya taifa hilo kusitishwa akionya huenda zikasababisha madhara yasiojulikana. Waziri wa ulinzi nchini Marekani amesisitiza kuwa bado kuna fursa ya kidiplomasia katika kukabiliana na Korea Kaskazini. Mapema rais Trump alichapisha ujumbe katika akaunti yake ya Twitter akisema mazungumzo sio suluhisho.

    Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania

    Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania Miaka 60 siku kama ya leo ugunduzi mkubwa ulifanyika katika eneo la Olduvai Gorge, kwenye kreta ya Ngorongoro. Wanaakiolojia Louis na Mary Leakey waligundua fuvu la mtu anayeaminika kuwa ni wa kale zaidi waliyompa jina la Zinjanthropus. Ugunduzi huo uliofanyika saa nne asubuhi Julai 22, 1959 kipindi hicho kwenye eneo la Tanganyika ulikuwa wa vipande zaidi ya 100 ukasaidia katika kutambua asili ya watu wa awali duniani. Kabla ya ugunduzi huo, wanasayansi na wanahistoria walikuwa wakiamini kuwa binadamu wa kale walitokea Uchina baada ya ugunduzi wa mafuvu ya kale baina ya 1923 na 1927 nchini humo ya Homo eractus, ama maarufu kama Peking Man. Mafuvu hayo ya Uchina yalikuwa na umri wa takribani miaka 750,000. Mafuvu ya Olduvai eneo ambalo kwa sasa lipo Tanzania wakati wa ugunduzi wake lilikuwa na umri wa takribani miaka milioni 1.75, na hakuna mabaki ya mtu wa kale zaidi ambayo mpaka sasa yamegundul...