Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Guterres: Uhamiaji umekuwepo Duniani tangu jadi

MTEULE THE BEST

Tarehe 18, Desemba ni Siku ya Uhamiaji Duniani. Katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amesema suala la uhamiaji limekuwepo tangu jadi na utaendelea kuwepo siku zote.


Libyen FlĆ¼chtlinge Schlauchboot (picture alliance/dpa/Str)
Katibu huyo wa Umoja wa Mataifa amesema jibu katika kushughulikia suala la uhamiaji ni ushirikiano mzuri wa kimataifa katika kuangazia sababu zinazochangia ongezeko la wahamiaji ili kuhakikisha manufaa yake yanasambazwa kwa usawa na haki za binadamu zinalindwa ipasavyo.
Umoja wa Mataifa umesema katika historia ya mwanadamu, uhamiaji umekuwa kielelezo cha kuonyesha ujasiri na ari ya watu binafsi kukabiliana na changamoto mbele yake ili kutimiza ndoto ya kuwa na maisha bora.
Katika ulimwengu wa sasa wa utandawazi pamoja na kuimarika katika teknolojia za mawasiliano na usafiri, kumechangia pakubwa katika kurahisisha kuhama kutoka sehemu moja hadi nyingine kwa watu na kuongeza idadi ya watu ambao wana dhamira na uwezo wa kuhamia kwingine duniani.
Nyakati hizi za sasa zimetoa fursa na changamoto kwa jamii kote duniani na pia inatoa nafasi ya kuhusisha uhamiaji na maendeleo kwa jumuiya ya kimataifa kutizama kwa undani suala la je uhamiaji unaweza kuchangia vipi katika kuimarisha sekta ya kiuchumi na kijamii kwa wanakotokea wahamiaji na wafikapo.
UN: Uhamiaji pia una manufaa
Uhamiaji umefungamanishwa na manufaa katika siasa za kikanda, biashara, na utamaduni lakini licha ya hayo, uhasama dhidi ya wahamiaji unazidi kuongezeka duniani.
USA Haitianer auf dem Weg zur kanadischen Grenze (Getty Images/AFP/G. Robind)
Wahamiaji kutoka Haiti wakijitayarisha kuingia mpaka wa Canada
Katika kuadhimisha siku hii ya uhamiaji, ulimwengu umetakiwa kushughulikia kwa uwazi changamoto, ugumu, matukio ya dharura na yasiyotarajiwa yanayoibuka kutokana na uhamiaji kwa kushirikiana zaidi kati ya nchi na kanda hadi kanda.
Umoja wa Mataifa unachangia pakubwa katika wajibu huu ikiwa na lengo la kuanzisha mijadala zaidi na ushirikiano zaidi miongoni mwa mataifa na kanda mbali mbali duniani ili uhamiaji liwe ni suala la kuchipuka kwa fursa na kukuza utangamano zaidi badala ya kuwa suala linalotizamwa kama mzigo na kitisho.
Mnamo tarehe 19 mwezi Septemba mwaka jana, Baraza kuu la Umoja wa Mataifa lilipitisha azimio la pamoja la nchi wanachama kujitolea kuwalinda wahamiaji na wakimbizi na kuimarisha maisha yao.
Makubaliano hayo yajulikanayo azimio la New York kuhusu wakimbizi na wahamiaji, linatilia msisitizo umuhumi wa nchi kuhakikisha haki za wakimbizi zinalindwa na wanapewa mazingira salama na maisha yao kuboreshwa kupitia hifadhi, elimu na huduma za afya.
Kauli mbiu ya mwaka huu ya maadhimisho ya siku ya uhamiaji duniani ni uhamiaji salama kwa ulimwengu unaosonga mbele. Katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amesema katika kuadhimisha siku hii wanatambua na kusherehekea  mchango wa wahamiaji takriban milioni 258 duniani

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

MAPENZI: Kuna faida na ni muhimu Mpenzi wako kuwa rafiki yako pia

Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi.  Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria.  Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao.  Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...

Urusi: Vikwazo dhidi ya Korea Kaskazini havitafua dafu

MTEULE THE BEST Image caption Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Sergei Lavrov na mwenzeka wa Marekani Rex Tillerson Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Segei Lavrov amemwambia waziri wa ulinzi nchini Marekani Rex Tillerson kwamba kuiwekea vikwazo zaidi Korea Kaskazini hakutafua dafu. Taarifa iliochapishwa na wizara ya kigeni nchini Urusi inasema kuwa wawili hao walizungumza kwa njia ya simu na kushutumu majaribio ya makombora ya hivi karibuni yaliotekelezwa na Pyongyang . Lakini inasema kuwa bwana Lavrov alisisitiza kwamba diplomasia ndio njia ya pekee ya kumaliza wasiwasi katika rasi ya Korea, na kutaka hatua zozote dhidi ya taifa hilo kusitishwa akionya huenda zikasababisha madhara yasiojulikana. Waziri wa ulinzi nchini Marekani amesisitiza kuwa bado kuna fursa ya kidiplomasia katika kukabiliana na Korea Kaskazini. Mapema rais Trump alichapisha ujumbe katika akaunti yake ya Twitter akisema mazungumzo sio suluhisho.

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania Miaka 60 siku kama ya leo ugunduzi mkubwa ulifanyika katika eneo la Olduvai Gorge, kwenye kreta ya Ngorongoro. Wanaakiolojia Louis na Mary Leakey waligundua fuvu la mtu anayeaminika kuwa ni wa kale zaidi waliyompa jina la Zinjanthropus. Ugunduzi huo uliofanyika saa nne asubuhi Julai 22, 1959 kipindi hicho kwenye eneo la Tanganyika ulikuwa wa vipande zaidi ya 100 ukasaidia katika kutambua asili ya watu wa awali duniani. Kabla ya ugunduzi huo, wanasayansi na wanahistoria walikuwa wakiamini kuwa binadamu wa kale walitokea Uchina baada ya ugunduzi wa mafuvu ya kale baina ya 1923 na 1927 nchini humo ya Homo eractus, ama maarufu kama Peking Man. Mafuvu hayo ya Uchina yalikuwa na umri wa takribani miaka 750,000. Mafuvu ya Olduvai eneo ambalo kwa sasa lipo Tanzania wakati wa ugunduzi wake lilikuwa na umri wa takribani miaka milioni 1.75, na hakuna mabaki ya mtu wa kale zaidi ambayo mpaka sasa yamegundul...