Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Tetesi za soka Ulaya Jumatano 20.12.2017

MTEULE THE BEST

Mkufunzi wa Manchester United Jose Mourinho anapanga kutoa rekodi ya dau la Uingereza la £90m kumnunua mchezaji wa Chelsea na Ubelgiji ,26, Eden Hazard. (Sun)
Image captionMkufunzi wa Manchester United Jose Mourinho anapanga kutoa rekodi ya dau la Uingereza la £90m kumnunua mchezaji wa Chelsea na Ubelgiji ,26, Eden Hazard. (Sun)
Mkufunzi wa Manchester United Jose Mourinho anapanga kutoa rekodi ya dau la Uingereza la £90m kumnunua mchezaji wa Chelsea na Ubelgiji ,26, Eden Hazard. (Sun)
Mshambuliaji wa zamani wa Arsenal Ian Wright ameitaka klabu ya Manchester City kumnunua mshambuliaji wa Liverpool Mo Salah. (Sky Sports via the Daily Express)
Mkufunzi wa Everton Sam Allardyce anataka kumpatia mshambuliaji wa Uingereza na Arsenal Theo Walcott, 28, njia ya kuondoka Arsenal mbali na kumyakua kiungo wa kati wa Sevilla na Ufaransa Steven N'Zonzi, 29. (Daily Mirror)
Newcastle United imejiunga katika harakati za kumsajili beki wa Chelsea David Luiz katika dirisha la uhamisho la mwezi Januari , lakini inataka kumchukua mchezaji huyo wa Brazil kwa mkopo (Shields Gazette)
Atletico Madrid wako tayari kumuuza mshambuliaji wa Ufaransa Antoine Griezmann, 26, kwenda Manchester United baada ya kuiripoti Barcelona kwa Fifa kuhusu madai ya klabu hiyo ya kutaka saini ya mchezaji huyo kinyume na sheria. (Daily Mirror)
Leicester City inajiandaa kumsajili beki wa Ureno na Benfica Andre Almeida, 27. (Leicester Mercury)
Mshambuliaji wa Liverpool na Wales Ben Woodburn, 18, ataruhusiwa kuondoka kwa mkopo mwezi Januari ili kuweza kupata nafasi ya kucheza. (Daily Mail)
Brighton wanapanga kumnunua mshambuliaji wa Spartak Moscow na Cape Verde Ze Luis, 26. (Sun)
Klabu ya China ya Chongqing Dangdai Lifan haina haja ya kumsajili kiungo wa kati wa Barcelona Andreas Iniesta kwa kuwa wanaamini kwamba sio mzuri sana kucheza katika ligi ya Uchina ya Super League (Marca via the Chongqing Morning Post)
Real Madrid inajiandaa kumlipa kipa wa Athletic Bilbao na Uhispania Kepa Arrizabalaga's Yuro milioni 20 mwezi Januari na kuthibitisha usajili wake katika wiki ya kwanza ya mwaka mpya.. (AS)
Beki wa Barcelona Javier Mascherano, 33, anakaribia kujiunga na klabu ya China ya Hebei Fortune. (Sport)
Mkufunzi wa Aston Villa Steve Bruce ana hamu ya kumsajili mshambuliaji wa Burnley na Bermuda Nahki Wells, 27, na mshambuliaji wa Leicester na Argentina Leonardo Ulloa, 31. (Birmingham Mail)
Mkufunzi wa Stoke Mark Hughes anaendelea kuungwa mkono na bodi ya klabu hiyo kabla ya mechi ya Jumamosi dhidi ya West Brom licha ya klabu hiyo kuwa pointi moja juu ya eneo la kushushwa daraja. (Sky Sports)
Mwenyekiti wa Stoke Peter Coates anasema kuwa kutakuwa na fedha za kutumia katika dirisha la uhamisho la mwezi Januari licha ya kwamba haijulikani ni nani atakayekuwa mkufunzi.(Stoke Sentinel)
Aliyekuwa kiungo wa kati wa Arsenal Mikel Arteta ameorodheshwa miongoni mwa wakufunzi wa siku zijazo wa Arsenal huku klabu hiyo ikiendelea na mipango ya mkufunzi atakayemrithi Wenger baada ya kuondoka kwake. (Telegraph)
Winga wa Wales na Liverpool Harry Wilson, 20, amekataa kusaini kandarasi mpya katika klabu hiyo ya Anfield. (ESPN)
Mkufunzi wa West Ham David Moyes anataka klabu hiyo kuwanunua viungo wa kati katika dirisha la uhamisho la mwezi Januari baada ya kuwashirikisha kinda Declan Rice na Domingos Quina katika kombe la Carabao dhidi ya Arsenal. (the42.ie)
Manchester City inapigiwa upato kushinda mataji manne baada ya kufika nusu fainali ya kombe la Carabao , lakini meneja wa klabu hiyo anasema haiwezekani.(Telegraph)
Mashabiki wa Manchester United huenda wakalazimika kulipa hadi £133 kwa tiketi za kombe la vilabu bingwa ugenini dhidi ya Sevilla. (Manchester Evening News)
Manchester United, Real Madrid, Juventus na Bayern Munich wamezindua jezi mpya lakini katika mchezo wa kompyuta wa Fifa wa wachezaji wa miaka 18.(Daily Mail)
Akaunti ya Twitter ya klabu ya Manchester City nchini Ufaransa imedai kuwa kiungi wa kati wa Manchester United Marouane Fellaini sio mchezaji wa soka(Metro)
Mshambuliaji wa Real Madrid Cristiano Ronaldo anatarajiwa kujenga hospitali ya watoto nchini Chiole 2020. (Four Four Two) lakini ripoti nyengine zinasema kuwa hana mipango ya kujenga hospitali yoyote. (efe)

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

MAPENZI: Kuna faida na ni muhimu Mpenzi wako kuwa rafiki yako pia

Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi.  Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria.  Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao.  Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...

Urusi: Vikwazo dhidi ya Korea Kaskazini havitafua dafu

MTEULE THE BEST Image caption Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Sergei Lavrov na mwenzeka wa Marekani Rex Tillerson Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Segei Lavrov amemwambia waziri wa ulinzi nchini Marekani Rex Tillerson kwamba kuiwekea vikwazo zaidi Korea Kaskazini hakutafua dafu. Taarifa iliochapishwa na wizara ya kigeni nchini Urusi inasema kuwa wawili hao walizungumza kwa njia ya simu na kushutumu majaribio ya makombora ya hivi karibuni yaliotekelezwa na Pyongyang . Lakini inasema kuwa bwana Lavrov alisisitiza kwamba diplomasia ndio njia ya pekee ya kumaliza wasiwasi katika rasi ya Korea, na kutaka hatua zozote dhidi ya taifa hilo kusitishwa akionya huenda zikasababisha madhara yasiojulikana. Waziri wa ulinzi nchini Marekani amesisitiza kuwa bado kuna fursa ya kidiplomasia katika kukabiliana na Korea Kaskazini. Mapema rais Trump alichapisha ujumbe katika akaunti yake ya Twitter akisema mazungumzo sio suluhisho.

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania Miaka 60 siku kama ya leo ugunduzi mkubwa ulifanyika katika eneo la Olduvai Gorge, kwenye kreta ya Ngorongoro. Wanaakiolojia Louis na Mary Leakey waligundua fuvu la mtu anayeaminika kuwa ni wa kale zaidi waliyompa jina la Zinjanthropus. Ugunduzi huo uliofanyika saa nne asubuhi Julai 22, 1959 kipindi hicho kwenye eneo la Tanganyika ulikuwa wa vipande zaidi ya 100 ukasaidia katika kutambua asili ya watu wa awali duniani. Kabla ya ugunduzi huo, wanasayansi na wanahistoria walikuwa wakiamini kuwa binadamu wa kale walitokea Uchina baada ya ugunduzi wa mafuvu ya kale baina ya 1923 na 1927 nchini humo ya Homo eractus, ama maarufu kama Peking Man. Mafuvu hayo ya Uchina yalikuwa na umri wa takribani miaka 750,000. Mafuvu ya Olduvai eneo ambalo kwa sasa lipo Tanzania wakati wa ugunduzi wake lilikuwa na umri wa takribani miaka milioni 1.75, na hakuna mabaki ya mtu wa kale zaidi ambayo mpaka sasa yamegundul...