Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Marekani yadaiwa kuwatesa Wasomalia 92 waliohamia nchini humo

MTEULE THE BEST


Rais Trump aliwalaumu raia wa Kisomali nchini humo kwa kueneza itikadi kaliHaki miliki ya pichaREUTERS
Image captionRais Trump aliwalaumu raia wa Kisomali nchini humo kwa kueneza itikadi kali

Mbunge wa Marekani ameitisha uchunguzi kuangalia unyanyasaji wa watu 92 wenye uraia wa Somalia wakati walipokuwa wanafukuzwa nchini humo.
Keith Ellison, ni mwakilishi wa wilaya kwenye jimbo la Minnesota, ambalo lina idadi kubwa ya watu wa jamii ya Wasomali, aliyasema hayo wakati wa mkutano baina yake na waandishi wa habari ya kwamba, maafisa wa uhamiaji waliwafungia wahamiaji hao, na kuwanyima chakula , huduma ya kwanza na huduma za afya kwa ujumla.
Kituo cha habari cha Minnesota Radio (MPR) kimearifu kuwa ndege iliyowabeba watu hao waliowekwa kizuizini , iliondoka Marekani tarehe 7 Disemba mwaka huu lakini ikarudi Miami siku iliyofuata.
Inaarifiwa kwamba safari yao ilichukua saa 40 ikiwa ni pamoja na saa 23 ikiweka kituo katika mji mkuu wa Senegal.
Ripoti hiyo, ikinukuu kesi iliyotolewa na wanasheria wa wafungwa, inasema kuwa wahamiaji haramu 92 walisalia kizuizini , ilhali mikono yao ikiwa imeshikamana na viuno vyao, na miguu yao, iliunganishwa kwa saa 48.



Mbona Wakenya na Wasomali wametimuliwa Marekani?

Bw. Ellison alitoa wito kwa shirika la Uhamiaji na Utekelezaji wa Forodha (ICE) kujibu mfululizo wa maswali ndani ya saa 48, ikiwa ni pamoja na kwa nini ndege ilirudi Marekani.
Shirika la ICE , lilitaarifu kuwa ndege hiyo ilirejea Marekani, kutokana na 'wahudumu wa ndege kukosa muda wa mapumziko ya kutosha kutokana na hitilafu kwenye hoteli waliyokuwa wamefikia jijini Dakar,' .
Shirika hilo pia limekana shutuma za unyanyasaji na kusema kuwa hakukuwa na mtu aliyeumizwa hisia zake wakati wote wa safari hiyo.
Na kuongeza utetezi wao kwa kutanabahisha kuwa wafungwa hao 92, walifungwa kutokana na sababu za usalama dhidi ya abiria wengine waliokuwemo katika ndege hiyo.
Wafungwa wapatao 61, waliwahi kuhukumiwa kutokana na makosa kama vile uhalifu, ubakaji na mauaji.
Wanasheria wa wafungwa hao, wamepokea agizo la mahakama linalozuia wafungwa hao kutolewa nchini Marekani hadi tarehe 8 Januari mwaka ujao.
Hakimu wa mahakama hiyo ametoa agizo hilo kwa kusema kuwa watu hao walioko kizuizini katika jimbo la Florida waendelee kupewa huduma za kibinaadamu ikiwemo huduma za afya

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

MAPENZI: Kuna faida na ni muhimu Mpenzi wako kuwa rafiki yako pia

Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi.  Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria.  Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao.  Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...

Urusi: Vikwazo dhidi ya Korea Kaskazini havitafua dafu

MTEULE THE BEST Image caption Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Sergei Lavrov na mwenzeka wa Marekani Rex Tillerson Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Segei Lavrov amemwambia waziri wa ulinzi nchini Marekani Rex Tillerson kwamba kuiwekea vikwazo zaidi Korea Kaskazini hakutafua dafu. Taarifa iliochapishwa na wizara ya kigeni nchini Urusi inasema kuwa wawili hao walizungumza kwa njia ya simu na kushutumu majaribio ya makombora ya hivi karibuni yaliotekelezwa na Pyongyang . Lakini inasema kuwa bwana Lavrov alisisitiza kwamba diplomasia ndio njia ya pekee ya kumaliza wasiwasi katika rasi ya Korea, na kutaka hatua zozote dhidi ya taifa hilo kusitishwa akionya huenda zikasababisha madhara yasiojulikana. Waziri wa ulinzi nchini Marekani amesisitiza kuwa bado kuna fursa ya kidiplomasia katika kukabiliana na Korea Kaskazini. Mapema rais Trump alichapisha ujumbe katika akaunti yake ya Twitter akisema mazungumzo sio suluhisho.

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania Miaka 60 siku kama ya leo ugunduzi mkubwa ulifanyika katika eneo la Olduvai Gorge, kwenye kreta ya Ngorongoro. Wanaakiolojia Louis na Mary Leakey waligundua fuvu la mtu anayeaminika kuwa ni wa kale zaidi waliyompa jina la Zinjanthropus. Ugunduzi huo uliofanyika saa nne asubuhi Julai 22, 1959 kipindi hicho kwenye eneo la Tanganyika ulikuwa wa vipande zaidi ya 100 ukasaidia katika kutambua asili ya watu wa awali duniani. Kabla ya ugunduzi huo, wanasayansi na wanahistoria walikuwa wakiamini kuwa binadamu wa kale walitokea Uchina baada ya ugunduzi wa mafuvu ya kale baina ya 1923 na 1927 nchini humo ya Homo eractus, ama maarufu kama Peking Man. Mafuvu hayo ya Uchina yalikuwa na umri wa takribani miaka 750,000. Mafuvu ya Olduvai eneo ambalo kwa sasa lipo Tanzania wakati wa ugunduzi wake lilikuwa na umri wa takribani miaka milioni 1.75, na hakuna mabaki ya mtu wa kale zaidi ambayo mpaka sasa yamegundul...