Haki miliki ya pichaREUTERSImage captionRais Trump aliwalaumu raia wa Kisomali nchini humo kwa kueneza itikadi kali
Mbunge wa Marekani ameitisha uchunguzi kuangalia unyanyasaji wa watu 92 wenye uraia wa Somalia wakati walipokuwa wanafukuzwa nchini humo.
Keith Ellison, ni mwakilishi wa wilaya kwenye jimbo la Minnesota, ambalo lina idadi kubwa ya watu wa jamii ya Wasomali, aliyasema hayo wakati wa mkutano baina yake na waandishi wa habari ya kwamba, maafisa wa uhamiaji waliwafungia wahamiaji hao, na kuwanyima chakula , huduma ya kwanza na huduma za afya kwa ujumla.
Kituo cha habari cha Minnesota Radio (MPR) kimearifu kuwa ndege iliyowabeba watu hao waliowekwa kizuizini , iliondoka Marekani tarehe 7 Disemba mwaka huu lakini ikarudi Miami siku iliyofuata.
Inaarifiwa kwamba safari yao ilichukua saa 40 ikiwa ni pamoja na saa 23 ikiweka kituo katika mji mkuu wa Senegal.
Ripoti hiyo, ikinukuu kesi iliyotolewa na wanasheria wa wafungwa, inasema kuwa wahamiaji haramu 92 walisalia kizuizini , ilhali mikono yao ikiwa imeshikamana na viuno vyao, na miguu yao, iliunganishwa kwa saa 48.
Bw. Ellison alitoa wito kwa shirika la Uhamiaji na Utekelezaji wa Forodha (ICE) kujibu mfululizo wa maswali ndani ya saa 48, ikiwa ni pamoja na kwa nini ndege ilirudi Marekani.
Shirika la ICE , lilitaarifu kuwa ndege hiyo ilirejea Marekani, kutokana na 'wahudumu wa ndege kukosa muda wa mapumziko ya kutosha kutokana na hitilafu kwenye hoteli waliyokuwa wamefikia jijini Dakar,' .
Shirika hilo pia limekana shutuma za unyanyasaji na kusema kuwa hakukuwa na mtu aliyeumizwa hisia zake wakati wote wa safari hiyo.
Na kuongeza utetezi wao kwa kutanabahisha kuwa wafungwa hao 92, walifungwa kutokana na sababu za usalama dhidi ya abiria wengine waliokuwemo katika ndege hiyo.
Wafungwa wapatao 61, waliwahi kuhukumiwa kutokana na makosa kama vile uhalifu, ubakaji na mauaji.
Wanasheria wa wafungwa hao, wamepokea agizo la mahakama linalozuia wafungwa hao kutolewa nchini Marekani hadi tarehe 8 Januari mwaka ujao.
Hakimu wa mahakama hiyo ametoa agizo hilo kwa kusema kuwa watu hao walioko kizuizini katika jimbo la Florida waendelee kupewa huduma za kibinaadamu ikiwemo huduma za afya
SHERIA 17 ZA SOKA ======================= Mchezo wa soka ni moja ya michezo maarufu sana duniani na ni biashara kubwa sana katika ulimwengu wa michezo na ukitaka kuamini hili angalia makampuni yaliyowekeza katika kudhamini soka – ni makampuni makubwa makubwa yenye hadhi ya kitaifa na kimataifa. Kwa kuzingatia aina hii ya wadhamini, waendeshaji wa mchezo wa soka, wameweka kanuni na miongozo ya kufuatwa ili kuhakikisha kuwa wale wanaowekeza pesa zao wanaona thamani ya uwekezaji wao. Kwa hiyo soka kama ilivyo katika michezo mingine inazo kanuni na tutajadili kanuni moja baada ya nyingine kama zilivobainishwa katika muongozo wa FIFA unaojulikana kwa jina la Law of the Game. Sheria Namba 1: Dimba ============== NYASI - Dimba la soka litakuwa la nyasi asilia au bandia kulingana na kanuni za masindano na nyasi hizo lazima ziwe za rangi ya kijani. Kwa dimba la nyasi bandia na kama mchezo unaochezwa utakuwa wa kutambuliwa na FIFA, basi nyasi hizo bandia lazima zikidhi viwango maalumu ...
Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi. Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria. Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao. Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...
MTEULE THE BEST TUMSIFU YESU KRISTO WAPENDWA KATIKA BWANA!!! MADA YA LEO: KUMTUMAINIA MUNGU SOMO; zaburi 11:1-7 Kwake MWENYEZI-MUNGU nakimbilia usalama; mnawezaje basi kuniambia "ruka kama ndege mpaka mlimani" Maana waovu wanavuta pinde wameweka mishale tayari juu ya uta wawapige mshale watu wema gizani! Kama misingi ikiaribiwa mtu mwadilifu atafanya nini? MWENYEZI-MUNGU yumo hekaluni mwake takatifu ; kiti cha enzi cha MWENYEZI-MUNGU kiko mbinguni Kwa macho yake huwachungulia wanadamu na kujua kila kitu wanachofanya MWENYEZI-MUNGU hupima waadilifu na waovu huwachukia kabisa watu wakatili Atawanyeshea waovu makaa ya moto na madini ya kiberti upepo wa hari ndiyo itakuwa adhabu yao MWENYEZI-MUNGU ni mwadilifu na apenda uadilifu watu wanyoofu watakaa pamoja naye NENO LA BWANA Unaruhusiwa kuchangia funguka tupate maoni yako MUNGU AKUBARIKI
Maoni