Je, rais Zuma atang'atuliwa madarakani kufuatia mabadiliko ya uongozi wa ANC?
Pata kiungo
Facebook
X
Pinterest
Barua pepe
Programu Nyingine
-
MTEULE THE BEST
Image captionJacob Zuma amekuwa Rais wa ANC kwa miaka kumi sasa
Rais wa Afrika Kusini Jacob Zuma inawezekana asimalize muhula wake wa mwisho madarakani baada ya chama cha ANC kumchagua Cyril Ramaphosa kama kiongozi wake mkuu.
Kwa kipindi cha miaka kadhaa iliyopita, Ramaphosa alikua rafiki wa karibu wa Zuma na hata msaidizi wake, lakini uhusiano wao umekua wa mashaka siku za karibuni.
Ramaphosa anasema atapambana na rushwa jambo ambalo kwa Zuma limekua kama mzigo.
Hivi ni vitu vichache ambavyo vinaweza kujitokeza kuelekea uchaguzi mkuu wa mwaka 2019:
1.Zuma kutimuliwa
Image captionMuhula wa Rais Zuma kuiongoza Afrika Kusini unaisha mwaka 2019
Chama cha ANC kitapendelea kuona kiongozi mkuu wa chama akiwa pia Rais wa nchi, jambo ambalo kama litatokea litamfanya Zuma kuachia ngazi ama kutimuliwa.
Hii itafungua njia kwa Ramaphosa kuchukua madaraka na kujaribu kurudisha imani ya wengi iliyopotea juu ya chama hicho kinachotuhumiwa na ufisadi, huku asilimia 62 ya uwezo wa chama hicho ukiwa mashakani.
Lakini jambo hili linatajwa kuwa la hatari kwa sababu linaweza kusambaratisha chama.
Baadhi ya viongozi wakuu wa ANC akiwemo Rais mpya wa chama na katibu mkuu wake wanaweza pia kumtimua.
Hii haitakuwa mara ya kwanza kwa Rais kufukuzwa ndani ya chama , mwaka 2008 Rais wa wakati huo Thabo Mbeki alitimuliwa baada ya Zuma kuingia madarakani kama Rais wa chama.
Uamuzi wa kumfukuza Zuma unaweza kufanywa na kamati kuu ya ANC ambayo ina mamlaka makubwa ndani ya chama.
2.Zuma kujiuzulu
Image captionRais wa zamani Thabo Mbeki alijiuzulu baada ya kupata upinzani mkali ndani ya chama
Jambo jingine ambalo limetajwa na mchambuzi wa masuala ya siasa wa Afrika Kusini Somadoda Fikeni ni uwezekano wa viongozi wakuu wa chama kumshawishi Zuma kuachia madaraka.
''Viongozi wa ANC wanaelewa gharama watakazoweza kuzipata iwapo Zuma atakuwa madarakani mpaka uchaguzi ujao''alisema.
''Kuna uwezekano wa kupoteza kura nyingi ama kushindwa kabisa,'' Aliongeza.
''Kwa maana hiyo uongozi huo unaweza kuongea nae kwa amani na kumshawishi kuachia ngazi kwa manufaa ya chama'',alisema Fikeni.
3.Zuma kusalia madarakani.
Image captionANC ni chama kikongwe zaidi Afrika Kusini
Kuna wale wanaoamini kuwa litakua jambo lisilo na busara kwa Ramaphosa kumfukuza ndani ya chama Rais Zuma kwa sababu inawezakusababisha mgawanyiko katika chama hicho zaidi na kuharibu mipango yao juu ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2019.
Badala yake wanaona ni vyema kwa Ramaphosa kujiimarisha zaidi na kuwa karibu na Zuma ili kuongeza nguvu ya kushinda uchaguzi wa 2019.
NI kipi kitakachotokea? bila shaka huu ni wakati mgumu kwa Zuma
SHERIA 17 ZA SOKA ======================= Mchezo wa soka ni moja ya michezo maarufu sana duniani na ni biashara kubwa sana katika ulimwengu wa michezo na ukitaka kuamini hili angalia makampuni yaliyowekeza katika kudhamini soka – ni makampuni makubwa makubwa yenye hadhi ya kitaifa na kimataifa. Kwa kuzingatia aina hii ya wadhamini, waendeshaji wa mchezo wa soka, wameweka kanuni na miongozo ya kufuatwa ili kuhakikisha kuwa wale wanaowekeza pesa zao wanaona thamani ya uwekezaji wao. Kwa hiyo soka kama ilivyo katika michezo mingine inazo kanuni na tutajadili kanuni moja baada ya nyingine kama zilivobainishwa katika muongozo wa FIFA unaojulikana kwa jina la Law of the Game. Sheria Namba 1: Dimba ============== NYASI - Dimba la soka litakuwa la nyasi asilia au bandia kulingana na kanuni za masindano na nyasi hizo lazima ziwe za rangi ya kijani. Kwa dimba la nyasi bandia na kama mchezo unaochezwa utakuwa wa kutambuliwa na FIFA, basi nyasi hizo bandia lazima zikidhi viwango maalumu ...
Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi. Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria. Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao. Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...
MTEULE THE BEST TUMSIFU YESU KRISTO WAPENDWA KATIKA BWANA!!! MADA YA LEO: KUMTUMAINIA MUNGU SOMO; zaburi 11:1-7 Kwake MWENYEZI-MUNGU nakimbilia usalama; mnawezaje basi kuniambia "ruka kama ndege mpaka mlimani" Maana waovu wanavuta pinde wameweka mishale tayari juu ya uta wawapige mshale watu wema gizani! Kama misingi ikiaribiwa mtu mwadilifu atafanya nini? MWENYEZI-MUNGU yumo hekaluni mwake takatifu ; kiti cha enzi cha MWENYEZI-MUNGU kiko mbinguni Kwa macho yake huwachungulia wanadamu na kujua kila kitu wanachofanya MWENYEZI-MUNGU hupima waadilifu na waovu huwachukia kabisa watu wakatili Atawanyeshea waovu makaa ya moto na madini ya kiberti upepo wa hari ndiyo itakuwa adhabu yao MWENYEZI-MUNGU ni mwadilifu na apenda uadilifu watu wanyoofu watakaa pamoja naye NENO LA BWANA Unaruhusiwa kuchangia funguka tupate maoni yako MUNGU AKUBARIKI
Maoni