Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Bunge la Seneti lapitisha mswada wa kupunguza kodi Marekani

MTEULE THE BEST

Makamu wa Rais Mike Pence alitangaza matokeo ya kura hizo
Image captionMakamu wa Rais Mike Pence alitangaza matokeo ya kura hizo
Bunge la Seneti la Marekani limepitisha mswada ambao ulidumu kwa kwa zaidi ya miongo mitatu.
Bunge la wawakilishi lilipitisha mswada huo mapema leo.Republican wana idadi kubwa ya wabunge nchini Marekani, hiyo ikitajwa kuwa sababu mojawapo ya kupitishwa kwake licha ya awali kupingwa na baadhi ya wabunge wa chama tawala.
Mswada huo sasa utarudishwa bungeni siku ya Jumatano kwa hatua za kuitambua na kuiidhinisha moja kwa moja.
Iwapo itapita kama ilivyotarajiwa, itakuwa mafanikio makubwa sana kwa Rais Trump tokea aingie madarakani.
Wakosoaji wanasema sheria hiyo itapendelea zaidi watu matajiri kuliko wale wa tabaka la kati ama la chini.
Mswada huo unatajwa kuleta usawa katika ulipaji wa kodi na kuongeza ajira zaidi
Image captionMswada huo unatajwa kuleta usawa katika ulipaji wa kodi na kuongeza ajira zaidi
Lakini chama cha Republican kinasema sheria hiyo itawanufaisha watu wote.
Makamu Rais Mike Pence alitoa matokeo ya kura hizo.
Katika mswada huu, kura 51 zinasema ndio na 48 hapana.kwa maana hiyo mswada huu utapitishwa kuwa sheria,''alisema.
Haya yanatajwa kuwa mafanikio makubwa kwa chama cha Republican haswa baada ya kushinwa kuondoa mfuko wa afya wa Obamacare.
Rais Trump ametuma ujimbe kwenye ukurasa wa Twitter akipongeza wabunge waliopiga kura
Image captionRais Trump ametuma ujumbe kwenye ukurasa wa Twitter akipongeza wabunge waliopiga kura
Kiongozi wa chama cha Democratic Chuck Schumer amesema chama cha Republican kimejiingiza kwenye mgogoro mkubwa ambao utawagharimu hususan kwenye uchaguzi mdogo wa mwakani.
Spika wa Bunge Paul Ryan alisema '' Leo tunawarudishia watu wa nchi hii fedha zao, hizi ni fedha zao kwa hakika!''
Mswada huo utapigiwa tena kura siku ya Jumatano kabla ya kusainiwa na Rais Trump na kuwa sheria kamili.
Jedwali likionyesha ni kundi gani litakalofaidi zaidi
Image captionJedwali likionyesha ni kundi gani litakalofaidi zaidi
Mswada huo utapunguza makato ya kodi kutoka asilimia 35 mpaka 21kwa makampuni makubwa na kupunguza pia kwa watu binafsi

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

MAPENZI: Kuna faida na ni muhimu Mpenzi wako kuwa rafiki yako pia

Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi.  Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria.  Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao.  Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...

Urusi: Vikwazo dhidi ya Korea Kaskazini havitafua dafu

MTEULE THE BEST Image caption Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Sergei Lavrov na mwenzeka wa Marekani Rex Tillerson Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Segei Lavrov amemwambia waziri wa ulinzi nchini Marekani Rex Tillerson kwamba kuiwekea vikwazo zaidi Korea Kaskazini hakutafua dafu. Taarifa iliochapishwa na wizara ya kigeni nchini Urusi inasema kuwa wawili hao walizungumza kwa njia ya simu na kushutumu majaribio ya makombora ya hivi karibuni yaliotekelezwa na Pyongyang . Lakini inasema kuwa bwana Lavrov alisisitiza kwamba diplomasia ndio njia ya pekee ya kumaliza wasiwasi katika rasi ya Korea, na kutaka hatua zozote dhidi ya taifa hilo kusitishwa akionya huenda zikasababisha madhara yasiojulikana. Waziri wa ulinzi nchini Marekani amesisitiza kuwa bado kuna fursa ya kidiplomasia katika kukabiliana na Korea Kaskazini. Mapema rais Trump alichapisha ujumbe katika akaunti yake ya Twitter akisema mazungumzo sio suluhisho.

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania Miaka 60 siku kama ya leo ugunduzi mkubwa ulifanyika katika eneo la Olduvai Gorge, kwenye kreta ya Ngorongoro. Wanaakiolojia Louis na Mary Leakey waligundua fuvu la mtu anayeaminika kuwa ni wa kale zaidi waliyompa jina la Zinjanthropus. Ugunduzi huo uliofanyika saa nne asubuhi Julai 22, 1959 kipindi hicho kwenye eneo la Tanganyika ulikuwa wa vipande zaidi ya 100 ukasaidia katika kutambua asili ya watu wa awali duniani. Kabla ya ugunduzi huo, wanasayansi na wanahistoria walikuwa wakiamini kuwa binadamu wa kale walitokea Uchina baada ya ugunduzi wa mafuvu ya kale baina ya 1923 na 1927 nchini humo ya Homo eractus, ama maarufu kama Peking Man. Mafuvu hayo ya Uchina yalikuwa na umri wa takribani miaka 750,000. Mafuvu ya Olduvai eneo ambalo kwa sasa lipo Tanzania wakati wa ugunduzi wake lilikuwa na umri wa takribani miaka milioni 1.75, na hakuna mabaki ya mtu wa kale zaidi ambayo mpaka sasa yamegundul...