Duru ya pili ya uchaguzi wa urais Liberia kati ya George Weah (kushoto) na Joseph Boakai
Watu nchini Liberia wanapiga kura katika duru ya pili kati ya makamu wa rais Joseph Boakai na nyota wa zamani wa kandanda George Weah.
Bwana Weah, 51, alishinda duru ya kwanza lakini hakufanikiwa kupata asilimia 50 ya kura kumwezesha kuwa mshindi.
Duru ya pili ya uchaguzi wa urais kuchukua mahala pake Ellen Johnson Sirleaf, ilichelewa kufuatia kesi iliyokuwa mahakamani.
Vituo vya kupigia kura vinafunguliwa saa mbili asubuhi na kufungwa saa kumi na mbili.
Zaidi ya watu milioni mbili wamejiandikisha kama wapiga kura.
Wagombea ni nani?
Bw. Boakai 73, amekuwa makamu wa rais nchini Liberia kwa miaka 12 lakini haonekani kunufaika na uungwaji mkono kutoka kwa rais.
Naye Weah, ambaye ni nyota wa zamani wa kandanda ana matumaini ya kushinnda baada ya kuwania kwa mara ya tatu.
Alimshinda Bi Johnson Sirleaf wakati wa duru ya kwanza mwaka 2005, lakini akashindwa wakati wa duru ya pili.
Wakati wa uchaguzi ulioafuata akiwa mgombea mwenza, muungano wake ulisusia duru ya pili ukidai kuwepo udanganyifu
Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi. Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria. Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao. Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...
Maoni