Ikiwa leo Wakristo duniani kote wanaadhimisha sikukuu ya Krismas, Waziri wa Mambo ya Ndani Mh. Mwigulu Chemba amewataka Watanzania kusherekea sikukuu za mwisho wa mwaka kwa Amani na Upendo.
Waziri Mwigulu ambaye wizara yake ndio ina dhamana ya kusimamia amani na usalama wa raia na mali zao nchini ametoa salamu zake za sikukuu huku akiwakumbusha wananchi kuzingatia Amani.
Kupitia Ukurasa wake wa mtandao wa Twitter, Mh Mwigulu ameandika, āMerry Christmass & Happy New Year, tusherekee kwa Amani na Upendoā.
Mbali na Waziri Mwigulu kusisitiza Amani kipindi hiki cha sikukuu, hivi karibuni pia Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini IGP Simon Sirro aliwataka Watanzania kusherehekea sikukuu bila kuvunja sheria za nchi
Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi. Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria. Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao. Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...
Maoni