Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Ndege kubwa zaidi inayoweza kutua kwenye maji yapaa

MTEULE THE BEST

The AG600 or Kunlong in Zhuhai, 24 December
Ndege kubwa zaidi inayoweza kutua kwenye maji yafanya safari ya kwanza
Ndege mpya kubwa zaidi duniani inayoweza kutua na kupaa kutoka kwa maji ya china ya AG600, imefanya safari yake ya kwanza ya jumla ya saa moja.
Ndege hiyo ambayo ni kubwa kuweza kukaribiana na ndege ya Boeng ya 747 na yenye injini 4, ilipaa kutoka uwanja wa ndege wa Zhuhai katika mkoa ulio kusini wa Guangdong.
Ndege hiyo inaweza kubeba watu 50 na kusalia hewani kwa saa 12.
    Ina mitambo ya kuzima moto na inaweza kufanya shughuli na uokoaji baharini na pia inaweza kutumwa kwenda eneo linalozozaniwa kusini mwa habari ya China.
    Vyombo vya habari nchini China viliitaja ndege hiyo kama mlinzi wa bahari na visiwa.
    Map of South China Sea
    Eneo linalozazaniwa kusini mwa bahari ya China
    Kupaa kwa ndege hiyo kulitangazwa moja kwa moja katika runinga ya taifa na ililakiwa na umati wa watu waliopeperusha bendera wakati ilitua.
    Imechukua miaka minane kuunda ndege hiyo iliyo na uzito wa tani 53.3.
      Tayari kuna kandarasi 17 za kujengwa ndege hiyo kutoka ndani ya China.
      Sera ya China ya kusini mwa bahari mwa China inapingwa vikali na nchi kadhaa majirani

      Maoni

      Machapisho maarufu kutoka blogu hii

      MAPENZI: Kuna faida na ni muhimu Mpenzi wako kuwa rafiki yako pia

      Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi.  Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria.  Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao.  Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...

      Urusi: Vikwazo dhidi ya Korea Kaskazini havitafua dafu

      MTEULE THE BEST Image caption Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Sergei Lavrov na mwenzeka wa Marekani Rex Tillerson Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Segei Lavrov amemwambia waziri wa ulinzi nchini Marekani Rex Tillerson kwamba kuiwekea vikwazo zaidi Korea Kaskazini hakutafua dafu. Taarifa iliochapishwa na wizara ya kigeni nchini Urusi inasema kuwa wawili hao walizungumza kwa njia ya simu na kushutumu majaribio ya makombora ya hivi karibuni yaliotekelezwa na Pyongyang . Lakini inasema kuwa bwana Lavrov alisisitiza kwamba diplomasia ndio njia ya pekee ya kumaliza wasiwasi katika rasi ya Korea, na kutaka hatua zozote dhidi ya taifa hilo kusitishwa akionya huenda zikasababisha madhara yasiojulikana. Waziri wa ulinzi nchini Marekani amesisitiza kuwa bado kuna fursa ya kidiplomasia katika kukabiliana na Korea Kaskazini. Mapema rais Trump alichapisha ujumbe katika akaunti yake ya Twitter akisema mazungumzo sio suluhisho.

      Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania

      Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania Miaka 60 siku kama ya leo ugunduzi mkubwa ulifanyika katika eneo la Olduvai Gorge, kwenye kreta ya Ngorongoro. Wanaakiolojia Louis na Mary Leakey waligundua fuvu la mtu anayeaminika kuwa ni wa kale zaidi waliyompa jina la Zinjanthropus. Ugunduzi huo uliofanyika saa nne asubuhi Julai 22, 1959 kipindi hicho kwenye eneo la Tanganyika ulikuwa wa vipande zaidi ya 100 ukasaidia katika kutambua asili ya watu wa awali duniani. Kabla ya ugunduzi huo, wanasayansi na wanahistoria walikuwa wakiamini kuwa binadamu wa kale walitokea Uchina baada ya ugunduzi wa mafuvu ya kale baina ya 1923 na 1927 nchini humo ya Homo eractus, ama maarufu kama Peking Man. Mafuvu hayo ya Uchina yalikuwa na umri wa takribani miaka 750,000. Mafuvu ya Olduvai eneo ambalo kwa sasa lipo Tanzania wakati wa ugunduzi wake lilikuwa na umri wa takribani miaka milioni 1.75, na hakuna mabaki ya mtu wa kale zaidi ambayo mpaka sasa yamegundul...