Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Mourinho: £300m nilizopewa kununua wachezaji hazitoshi









Mkufunzi wa Man United Jose Mourinho

Mkufunzi wa Manchester United Jose Mourinho anasema kuwa dau la £300m alilotumia kuimarisha kikosi chake halitoshi baada ya timu yake kutoka sare ya 2-2 na klabu ya Burnley siku ya Jumanne.



Jesse Lingard alifunga katika dakika za lala salama kusawazisha, na sasa sare hiyo inaiwacha Man United ikiwa pointi 12 nyuma ya viongozi wa ligi ManCity.

''Tuko katika mwaka wa pili kujaribu kujenga timu ambayo unajua sio miongoni mwa timu bora duniani'', alisema raia huyo wa Ureno.

''Manchester City inanunua mabeki wa kushoto na kulia kwa gharama ya washambuliaji, aliongezea''.

Mourinho ambaye aliteuliwa kuwa mufunzi wa United mnamo mwezi Mei 2016 na kuvunja rekodi ya dunia alipomnunua kiungo wa kati Paul Pogba kwa kitita cha £89m, Eric Bailly kwa kitita cha £30m na kiungo wa kati Henrikh Mkhitaryan kwa £26.3m.

Mwaka huu alimnunua Romelu Lukaku kwa £75m ,beki Victor Lindelof kwa £31m na Nemanja Matic kwa £41m.

''Kutumia £300m hazitoshi.Gharama ya vilabu vikubwa ni tofauti na vilabu vyengine''.

''Klabu kubwa za zamani huadhibiwa katika soko kutokana na historia hiyo.Vijana wanafanya kile wanachoweza kufanya na wanaendelea vyema''.

Mourinho aliulizwa iwapo alama nane katika mechi tano zinatosha kwa klabu kama Man United.

Alijibu: Unaposema klabu kama United , je nadhani Milan sio klabu kubwa kama sisi?Unadhani Real Madrid sio klabu kubwa kama yetu?.

''Najua klabu kubwa ni gani.Kitu kimoja ni klabu kubwa na chengine ni ni klabu kubwa ya soka. Ni vitu tofauti''.

''Unazungumzia kuhusu jukumu la kutaka kushinda ligi ya Uingereza, Tottenham haina jukumu kama hilo kwa sababu sio klabu yenye historia kama yetu. Arsenal haina jukumu la kushinda. Chelsea haina jukumu la kushinda. Unapozungumzia kuhusu vilabu vikubwa unazungumzia kuhusu historia ya klabu


Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

MAPENZI: Kuna faida na ni muhimu Mpenzi wako kuwa rafiki yako pia

Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi.  Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria.  Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao.  Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...

Urusi: Vikwazo dhidi ya Korea Kaskazini havitafua dafu

MTEULE THE BEST Image caption Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Sergei Lavrov na mwenzeka wa Marekani Rex Tillerson Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Segei Lavrov amemwambia waziri wa ulinzi nchini Marekani Rex Tillerson kwamba kuiwekea vikwazo zaidi Korea Kaskazini hakutafua dafu. Taarifa iliochapishwa na wizara ya kigeni nchini Urusi inasema kuwa wawili hao walizungumza kwa njia ya simu na kushutumu majaribio ya makombora ya hivi karibuni yaliotekelezwa na Pyongyang . Lakini inasema kuwa bwana Lavrov alisisitiza kwamba diplomasia ndio njia ya pekee ya kumaliza wasiwasi katika rasi ya Korea, na kutaka hatua zozote dhidi ya taifa hilo kusitishwa akionya huenda zikasababisha madhara yasiojulikana. Waziri wa ulinzi nchini Marekani amesisitiza kuwa bado kuna fursa ya kidiplomasia katika kukabiliana na Korea Kaskazini. Mapema rais Trump alichapisha ujumbe katika akaunti yake ya Twitter akisema mazungumzo sio suluhisho.

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania Miaka 60 siku kama ya leo ugunduzi mkubwa ulifanyika katika eneo la Olduvai Gorge, kwenye kreta ya Ngorongoro. Wanaakiolojia Louis na Mary Leakey waligundua fuvu la mtu anayeaminika kuwa ni wa kale zaidi waliyompa jina la Zinjanthropus. Ugunduzi huo uliofanyika saa nne asubuhi Julai 22, 1959 kipindi hicho kwenye eneo la Tanganyika ulikuwa wa vipande zaidi ya 100 ukasaidia katika kutambua asili ya watu wa awali duniani. Kabla ya ugunduzi huo, wanasayansi na wanahistoria walikuwa wakiamini kuwa binadamu wa kale walitokea Uchina baada ya ugunduzi wa mafuvu ya kale baina ya 1923 na 1927 nchini humo ya Homo eractus, ama maarufu kama Peking Man. Mafuvu hayo ya Uchina yalikuwa na umri wa takribani miaka 750,000. Mafuvu ya Olduvai eneo ambalo kwa sasa lipo Tanzania wakati wa ugunduzi wake lilikuwa na umri wa takribani miaka milioni 1.75, na hakuna mabaki ya mtu wa kale zaidi ambayo mpaka sasa yamegundul...