Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Rais Trump aishutumu China kwa kusafirisha mafuta Korea Kaskazini





Korea Kaskazini inahitaji mafuta lakini vikwazo vinazidi kuilemea





Rais wa Marekani Donald Trump amesema kuwa amevunjwa moyo na China kufuatia ripoti kwamba iliruhusu mafuta kusafirishwa hadi nchini Korea Kaskazini.





Katika Ujumbe wa twitter, bwana Trump alisema kuwa China ilionekana ''hadharani'' ikiruhusu mafuta hayo kwenda Korea Kaskazini.





Amesema hakuwezi kuwa na suluhu ya kirafiki katika mgogoro wa Korea Kaskazini iwapo mafuta yataruhusiwa kusafirishwa hadi Pyongyang.





China mapema ilikana kwamba kumekuwa na ukiukaji wowote wa azimio la Umoja wa mataifa la mafuta kati ya China na Korea Kaskazini.





Wiki iliopita , Beijing iliunga mkono azimio la Umoja wa Mataifa lililoandikwa na Marekani ambalo lilishirikisha hatua za kupunguza kiwango cha mafuta kinacheolekea Korea Kaskazini kwa asilimia 90.







Ujumbe wa twitter uliochapishwa na rais Donald Trump





Vikwazo hivyo vikali ni jaribio jipya kuzuia majaribio ya silaha yanyotekelezwa na Pyongyang.





Matamshi hayo ya rais Trump dhidi ya China yanajiri baada ya gazeti moja la Korea Kusini Chosun IIbo kuripoti kwamba meli za China zimekuwa zikisafirisha mafuta kwa siri kupitia baharini kuelekea Korea Kaskazini.





Likiwanukuu maafisa wa serikali ya Korea Kusini, limesema kuwa usafirishaji huo unaenda kinyume na sheria kutoka meli moja hadi nyingine ulipigwa picha na Satellite za Marekani za ujasusi takriban mara 30 tangu mwezi Oktoba.





Maafisa wa Marekani hawakuthibitisha ripoti hiyo lakini afisa ya idara moja ya serikali aliyenukuliwa na reuters alisema kuwa usafirishaji huo huenda unaendelea.





Usafrishaji wa mafuta kutoka meli moja hadi nyingine unaendelea kuleta wasiwasi ikiwa miongoni mwa njia za Korea Kaskazini kukwepa vikwazo hivyo.





China ambayo ni mshirika mkubwa wa kibiashara wa taifa la Korea Kaskazini , imesema kuwa inatekeleza vikwazo vyote vilivyowekwa na UN dhidi ya Korea Kaskazini.







Kiongozi wa korea Kaskazini Kim Jong un amepuuzilia mbali shinikizo za kimataifa





Alipoulizwa maswali kuhusu ripoti za usafirishaji wa mafuta kutoka meli moja hadi nyingine, msemaji wa wizara ya ulinzi nchini China Ren Guoqiang aliambia maripota kwamba: hali ulioitaja haipo.





Msemaji wa wizara ya maswala ya kigeni nchini Marekani Michael Cavey alisisitiza kuhusu wito wa mataifa yote kusitisha uhusiano wa kiuchumi na Korea Kaskazini.





''Tunatoa wito kwa China kusitisha uhusiano wowote wa kiuchumi na Jamhuri ya kidemokrasi ya Korea Kaskazini ikiwemo utalii pamoja na uuzaji wa mafuta ama bidhaa za mafuta'', alisema




Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

MAPENZI: Kuna faida na ni muhimu Mpenzi wako kuwa rafiki yako pia

Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi.  Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria.  Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao.  Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...

Urusi: Vikwazo dhidi ya Korea Kaskazini havitafua dafu

MTEULE THE BEST Image caption Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Sergei Lavrov na mwenzeka wa Marekani Rex Tillerson Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Segei Lavrov amemwambia waziri wa ulinzi nchini Marekani Rex Tillerson kwamba kuiwekea vikwazo zaidi Korea Kaskazini hakutafua dafu. Taarifa iliochapishwa na wizara ya kigeni nchini Urusi inasema kuwa wawili hao walizungumza kwa njia ya simu na kushutumu majaribio ya makombora ya hivi karibuni yaliotekelezwa na Pyongyang . Lakini inasema kuwa bwana Lavrov alisisitiza kwamba diplomasia ndio njia ya pekee ya kumaliza wasiwasi katika rasi ya Korea, na kutaka hatua zozote dhidi ya taifa hilo kusitishwa akionya huenda zikasababisha madhara yasiojulikana. Waziri wa ulinzi nchini Marekani amesisitiza kuwa bado kuna fursa ya kidiplomasia katika kukabiliana na Korea Kaskazini. Mapema rais Trump alichapisha ujumbe katika akaunti yake ya Twitter akisema mazungumzo sio suluhisho.

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania Miaka 60 siku kama ya leo ugunduzi mkubwa ulifanyika katika eneo la Olduvai Gorge, kwenye kreta ya Ngorongoro. Wanaakiolojia Louis na Mary Leakey waligundua fuvu la mtu anayeaminika kuwa ni wa kale zaidi waliyompa jina la Zinjanthropus. Ugunduzi huo uliofanyika saa nne asubuhi Julai 22, 1959 kipindi hicho kwenye eneo la Tanganyika ulikuwa wa vipande zaidi ya 100 ukasaidia katika kutambua asili ya watu wa awali duniani. Kabla ya ugunduzi huo, wanasayansi na wanahistoria walikuwa wakiamini kuwa binadamu wa kale walitokea Uchina baada ya ugunduzi wa mafuvu ya kale baina ya 1923 na 1927 nchini humo ya Homo eractus, ama maarufu kama Peking Man. Mafuvu hayo ya Uchina yalikuwa na umri wa takribani miaka 750,000. Mafuvu ya Olduvai eneo ambalo kwa sasa lipo Tanzania wakati wa ugunduzi wake lilikuwa na umri wa takribani miaka milioni 1.75, na hakuna mabaki ya mtu wa kale zaidi ambayo mpaka sasa yamegundul...