MTEULE THE BEST
Luke Shaw
Meneja wa Tottenham Mauricio Pochettino anasema yuko tayari kutoa afa mara mbili kwa mchezaji wa kiungo cha kati wa Everton Ross Barkley, 24, na mlinzi wa Manchester United Luke Shaw, 22. (Sunday Express).
Manchester United wamekawaia kumpa Mourinho mkataba mpya wakati Man U ikishuka katika ligi. (Mirror).
Ajenti wa Olivier Giroud atasafiri kwenda London wiki hii kwa mazungumzo kuhusu hatma ya mshambuliaji huyo wa Arsenal wa miaka 30. (Mirror)
Jack Wilshere
Mchezaji wa kiungo cha kati wa Arsenal, Jack Wilshere, 25, yuko kwa orodha kwenye orodha ya kombe la dunia yake Gareth Southgate baada ya kurudi katika kikosi cha kwanza cha Gunners. (The Sun)
Meneja wa Manchester City Pep Guardiola anammezea mate mchezaji wa safu ya kati wa Shakhtar Donetsk, Fred 24 wakati City wanataka kuimarisha kikosi chao msimu ujao. (Mail on Sunday)
Henrikh Mkhitaryan
Arsenal wamepiga hatua mbele ya Manchester United na Chelsea katika mbio za kumpata wing'a wa Bayer Leverkusen Leon Bailey 29. (Mirror)
Inter Milan wanataka kuchukua mchezaji wa safu ya kati wa Henrikh Mkhitaryan, 28, kwa mkopo kutoka Manchester United. (Mail on Sunday)
Bournemouth imekataa ofa kutoka kwa West Ham ya pauni milioni 8 kwa mchezaji wa miaka 27 Harry Arter. (Sunday Express
Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi. Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria. Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao. Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...
Maoni