MTEULE THE BEST
Tunisia yapiga marufuku ndege za Emirates kutua mji mkuu Tunis
Tunisia imepiga marufuku ndege za shirika la Emirates kutua kwennye mji mkuu Tunis baada ya wanawake kadha raia wa Tunisia kuzuiwa kuabiri ndege za shirika hilo.
Hatua hiyo inakuja huku kukiwa na malalamiko makubwa nchini Tunisia kulaani hatua hiyo ya Emirates.
Wizara ya ulinzi ilisema kuwa marufuku hiyo itasalia hadi pale Emirates itakapoweka kuendesha shughuli zake kulingana na sheria na makubaliano ya kimataifa.
UAE ilisema kuwa tatizo la kuisalama lilisababisha hali hiyo.
Wanawake waislamu nchini Tunisia waruhusiwa kuolewa na wanaume wasio waislamu
Kifungo cha waliokamatwa wakibusu chadumishwa Tunisia
Maafisa wa serikali ya Tunisia walisema kuwa UAE ilikuwa imepiga marufuku wanawake wa Tunisia kupitia nchi yake.
Siku ya Ijumaa serikali ya Tunisia ilisema kuwa ilikuwa imemuuliza balozi wa UAE kueleza kile kilikuwa kikiendelea na alikuwa ameambiwa kuwa hatua hizo zilikuwa ni za muda na tayari zilikuwa zimeondolewa.
Vyombo vya habari viliripoti kuwa wanawake wa Tunisia walikuwa wamezuiwa kuabiri ndege za Emirate kwenda Dubai kwa siku kadhaa.
Tunisia imejaribu kuboresha uhusiano wake na UAE ulioharibika wakati wa mapinduzi mwaka 2011
KIMATAIFA
Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi. Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria. Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao. Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...
Maoni