Ruka hadi kwenye maudhui makuu

BANGI KUTUMIKA HADHARI SASA

Kwa nini mataifa mengi yameanza kuidhinisha matumizi ya bangi?



Sehemu mbalimbali duniani mtazamo kuhusiana na matumizi ya mmea wa cannabis yaani bangi unabadilika kwa kasi.


Serikali mpya ya Mexico ina mpango wa kuhalalisha matumizi ya bangi kama njia ya kujiburudisha, sawa na ilivyofanya utawala mpya wa Luxembourg. Wakati huo huo, viongozi wakuu nchini New Zealand, wanakusudia kuandaa kura ya maoni ya namna watakavyoshughulikia swala hilo.

Jinsi maoni ya umma - na yale ya serikali- yanavyobadilika, ni dhahiri kuwa mataifa mengi yatafuata mkondo huo. Maswali yanayoibuka ni kwa namna gani nchi hizo zitadhibiti matumizi na usambazaji wa mmea huo?

Ni nini hasa kinachopelekea mataifa mbalimbali katika kulegeza kamba kwenye sheria zake, au hata kuamua kuidhinisha ,matumizi ya bangi moja kwa moja?

Vita dhidi ya mihadarati

Ilikuwa mwaka 2012 ambapo Uruguay, ilipoandika historia kwa kuwa taifa la kwanza duniani kuruhusu matumizi ya bangi kwa minajili ya kujiburudisha. Hatua hiyo, kwa uhalisia, ilikuwa na nia ya kuiwezehsa serikali kushughulikia biashara haramu na magenge ya wahalifu waliokuwa wanaiongoza biashara hiyo.

Baadaye mwaka huo, wapiga kura katika majimbo mawili ya Washington na Colorado, wakawa wa kwanza kabisa nchini Marekani kuunga mkono uidhinishwaji wa matumizi ya bangi ambayo si ya kimatibabu.

Chini ya utawala wa Barack Obama, msisitizo uliwekwa kwenye majimbo kuwa huru katika kubadili sheria zake za kuratibu matumizi ya bangi.

Majimbo manane mengine kwa pamoja na Washington DC, yameunga mkono uhalalishwaji wa bangi kwa njia ya kujiburudisha huku hukumu ya kupatikana au kutumia kama dawa ikilegezwa kwingineko.

Matumizi ya bangi kwa minajili ya dawa, sasa yanakubaliwa katika majimbo 33 kati ya majimbo 50 nchini Marekani.


Uruguay na Canada wanaruhusu uvutwaji wa bangi hadharani

Sasa wimbi hilo limetanda kote Marekani na linakwenda kwa kasi mno, huku Canada ikihalalisha uuzaji, umiliki na matumizi ya bangi kwa njia ya kujiburudisha kote nchini humo mwezi Oktoba mwaka huu.

Kwa Mexico kuhalalisha bangi bila shaka ni jambo la hakika. Serikali mpya ya AndrĆ©s Manuel LĆ³pez Obrador imewasilisha muswada bungeni, ambao utahalalisha matumizi yake kama dawa na burudani, ilihali mahakama ya juu zaidi nchini humo, hivi majuzi iliamua kuwepo kwa marufuku ya matumizi ya bangi kwa njia ya burudani, kwamba ni kinyume cha sheria.

Mataifa mengine yanaongeza shinikizo. Ingawa uuzaji wa bangi unasalia kuwa haramu, kupatikana na kiwango kidogo sio tena uvunjaji wa sheria katika mataifa ya Brazil, Jamaica na Ureno.

Nchini Uhispania ni ruhusa kuvuta bangi japo kwa siri, ilihali dawa hizo zinauzwa wazi katika maduka yenye majina Coffee Shops nchini Uholanzi. Bado mataifa mengi yanakubalia matumizi ya cannabis kwa matibabu.

Nchini Uingereza, madaktari wamekubaliwa kuwapa wagonjwa bidhaa za cannabis tangu mwezi Novemba.Korea Kusini wamehalalisha matumizi ya bangi kama dawa lakini chini ya mazingira yenye sheria kali, licha ya kuwahukumu wakaazi wanaotumia dawa hizo hata nje ya nchi.

Hukumu ya kifo kwa mvulana mmoja aliyepatikana akiuza mafuta ya bangi, imesababisha mjadala mkali wa uhalalishaji wa bangi nchini Malaysia. Lebanon inadhamiria kuhalalisha uzalishaji wa cannabis kwa matibabu, na pia kusaidia kuboresha uchumi wa taifa.

Lesotho ilikuwa nchi ya kwanza Afrika kuruhusu kilimo na matumizi ya bangi kwa sababu za kiafya tu. Tayari wakulima wamegeukia zao hilo na wanapata pesa maradufu.

Mwezi Aprili mwaka huu, Zimbabwe ilikuwa nchi ya pili Afrika kuhalalisha uzalishaji wa bagi kwa matumizi ya kiafya na kisayansi.

Septemba mwaka huu Mahakama ya Kikatiba nchini Afrika Kusini ilihalalisha utumiaji wa bangi kwa watu wazima katika maeneo faragha.

Watoto wagonjwa

Mwanzo wa kuhalalisha bangi umekuwa ni huruma ya jamii. Nchini Marekani na Canada, picha za watoto ambao ni wagonjwa na uzima wao ni dawa zenye vimelea vya bangi zilitumika kufanya kampeni ya kuhalalisha bangi.

Canada iliruhusu matumizi ya bangi kimatibabu mwanzoni mwa miaka ya 2000 kabla ya kuruhusu kuwa kiburudisho mwaka huu.

Mtazamo kama huo pia umeshuhudiwa nchini Uingereza.

Mwezi Juni, Billy Gladwell mwenye umri wa miaka 12, aliyekuwa akiugua kifafa, alilazwa hospitalini, baada ya dawa yake mafuta ya bangi ilipokamatwa. Mwezi mmoja baadaye, leseni maalum ya kutumia mafuta ya bangi ikatolewa kwa Alfie Dingley mwenye umri wa miaka 7, aliyekuwa akiugua pia kifafa.


Mamake Alfie Dingley anasema mafuta ya cannabis imemsaidia mwanawe dhidi ya kifafa

Mwezi Juni, Billy Gladwell mwenye umri wa miaka 12, aliyekuwa akiugua kifafa, alilazwa hospitalini, baada ya dawa yake mafuta ya bangi ilipokamatwa. Mwezi mmoja baadaye, leseni maalum ya kutumia mafuta ya bangi ikatolewa kwa Alfie Dingley mwenye umri wa miaka 7, aliyekuwa akiugua pia kifafa.

Kufuatia kampeni ya nguvu, serikali ya Uingereza iliamua kubadilisha sheria ili kuwakubalia madaktari kuwapa wagonjwa matibabu yanayotokana na bidhaa za bangi.

Lakini nchini Uingereza, Wizara ya mambo ya ndani, inasema matumizi ya bangi kwa njia ya burudani, itasalia kupigwa marufuku, hata ingawa maafisa wakuu, akiwemo kiongozi mmoja mkuu wa chama cha Conservative, William Hague, akipendekeza hatua hiyo ifikiriwe upya.

Mexico pia ina kesi ya watoto wanaokatazwa kupewa bangi kwa matibabu, lakini pia inakabiliwa na changamoto ya ghasia zinazohusishwa na vita vya ulanguzi wa mihadarati.

Hata ingawa bangi ni sehemu ndogo mno ya asilimia kubwa ya magenge yanayojihusisha na uuzaji wa dawa za kulevya, marufuku dhidi yake inaonekana kuchochea zaidi kuongezeka kwake kuliko hali ilivyo.

Wanadiplomasia wa Mexico, wanaionya Marekani kuwa, ni vigumu mno kukabiliana na bangi huku jimbo jirani la California limeidhinisha matumizi yake.

Masoko ya Bangi


Huku mataifa mengi duniani yakielekea katika hali ya kuleta mabadiliko ya uhalalishaji wa bangi, ni wazi soko la zao hilo litazidi kupanuka.

Serikali za nchi za Amerika ya Kusini zinataka wakulima wao kuyafikia masoko hayo ya biashara kubwa ya ukulima wa bangi kwa minajili ya matibabu, ambayo yanaszidi kukua kila uchao.

Nchini Lesotho, wakulima tayari wameanza kuvuna faida ya kilimo hicho.

Mashirika makubwa pia yameonyesha hitaji la kujiunga nayo. Kampuni ya Altria, ambayo ni wazalishaji wa chapa maarufu ya sigara za Marlboro wapo katika mazungumzo na kampuni moja ya kuzalisha bangi nchini Canada ili wawekeze mtaji wao wa dola bilioni 1.86.

Wazalishaji wa bia ya Corona, kampuni ya Constellation Brands imesema itawekeza dola bilioni 4 kwenye kampuni kubwa zaidi ya uzalishaji bangi nchini Cananda, Canopy Growth. Uwekezaji huo ndio mkubwa zaidi mpaka sasa katika biashara ya bangi duniani.

Kampuni maarufu ya vinywaji ya Coca-Cola ni maarufu zaidi kwa kutengeneza soda, lakini sasa inapanga kufanyia majaribio aina mpya ya kinywaji ambacho kitakuwa na bangi.

Changamoto kubwa kwa sasa, ni matumizi ya cannabis kwa burudani, haiwezi kuwa biashara kutoka taifa moja hadi nyingine. Mataifa tu yatanunua bidhaa hiyo kutoka nje au kuuza nje ya nchi kama tiba chini ya mfumo wa leseni inayopigiwa msasa na Bodi ya Kimataifa ya Kudhibiti Mihadarati.

Wakulima katika mataifa kama vile Morocco na Jamaica, wanasifika kwa kuzalisha bangi nzuri lakini hawataweza kuyafikia masoko ambayo wakulima wake wa ndani si wazuri kama ilivyotokea nchini Canada mara tu baada ya kuhalalisha.

Madhara ya Bangi

Unaweza kusababisha kuchanganyikiwa na wasiwasi usio wa kawaida


Ikivutwa na tumbaku, inaweza kuongeza hatari ya ugonjwa kama vile saratani ya mapafu


Matumizi ya mara kwa mara yamehusishwa na hatari ya kupatwa na magonjwa ya kiakili


Upungufu wa kudumu wa kiwango cha mtu kufikiria na kufahamu mambo, baada ya kutumia kwa muda mrefu


Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

MAPENZI: Kuna faida na ni muhimu Mpenzi wako kuwa rafiki yako pia

Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi.  Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria.  Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao.  Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania Miaka 60 siku kama ya leo ugunduzi mkubwa ulifanyika katika eneo la Olduvai Gorge, kwenye kreta ya Ngorongoro. Wanaakiolojia Louis na Mary Leakey waligundua fuvu la mtu anayeaminika kuwa ni wa kale zaidi waliyompa jina la Zinjanthropus. Ugunduzi huo uliofanyika saa nne asubuhi Julai 22, 1959 kipindi hicho kwenye eneo la Tanganyika ulikuwa wa vipande zaidi ya 100 ukasaidia katika kutambua asili ya watu wa awali duniani. Kabla ya ugunduzi huo, wanasayansi na wanahistoria walikuwa wakiamini kuwa binadamu wa kale walitokea Uchina baada ya ugunduzi wa mafuvu ya kale baina ya 1923 na 1927 nchini humo ya Homo eractus, ama maarufu kama Peking Man. Mafuvu hayo ya Uchina yalikuwa na umri wa takribani miaka 750,000. Mafuvu ya Olduvai eneo ambalo kwa sasa lipo Tanzania wakati wa ugunduzi wake lilikuwa na umri wa takribani miaka milioni 1.75, na hakuna mabaki ya mtu wa kale zaidi ambayo mpaka sasa yamegundul...

Urusi: Vikwazo dhidi ya Korea Kaskazini havitafua dafu

MTEULE THE BEST Image caption Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Sergei Lavrov na mwenzeka wa Marekani Rex Tillerson Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Segei Lavrov amemwambia waziri wa ulinzi nchini Marekani Rex Tillerson kwamba kuiwekea vikwazo zaidi Korea Kaskazini hakutafua dafu. Taarifa iliochapishwa na wizara ya kigeni nchini Urusi inasema kuwa wawili hao walizungumza kwa njia ya simu na kushutumu majaribio ya makombora ya hivi karibuni yaliotekelezwa na Pyongyang . Lakini inasema kuwa bwana Lavrov alisisitiza kwamba diplomasia ndio njia ya pekee ya kumaliza wasiwasi katika rasi ya Korea, na kutaka hatua zozote dhidi ya taifa hilo kusitishwa akionya huenda zikasababisha madhara yasiojulikana. Waziri wa ulinzi nchini Marekani amesisitiza kuwa bado kuna fursa ya kidiplomasia katika kukabiliana na Korea Kaskazini. Mapema rais Trump alichapisha ujumbe katika akaunti yake ya Twitter akisema mazungumzo sio suluhisho.