Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Tetesi za Soka Ulaya Jumanne 11.12.2018:

Eden HazardHaki miliki ya pichaGETTY IMAGES
Image captionEden Hazard

Mchezaji wa Chelsea Eden Hazard, 27, tena amezungumzia kuhama kwenda Real Madrid na anasema kuwa hajui ni lini ataamua hatma yake. Lakini Mbelgiji huyo amekiri kuwa mazungumzo kuhusu mkataba mpya huko Stamford Bridge yamekwama. (RMC Sport via Express)

Mkurugenbzi wa michezo wa AC Milan Leonardo amethibitisha kuwa klabu hiyo ya Serie A imezungumza Chelsea kuhusu uwezekano wa kumsaini kiungo wa kati Cesc Fabregas, 31. (London Evening Standard)

Tottenham wamejiunga na Manchester United katika kumwinda mshambuliaji raia wa Romania Dennis Man, mchezaji huyo mwenye miaka 20 aiyechezea FCSB ambayo awali ilikuwa inajulikana kama Steaua Bucharest. (Sun)

Cesc FabregasHaki miliki ya pichaGETTY IMAGES
Image captionCesc Fabregas

Spurs wanachelewa zaidi kuufungua uwanja wao mpya kutokana na ugumu wa kuandaa warsha wakati huu wa msimu wa krismasi. (Times)

Meneja wa Fulham Claudio Ranieri yuko tayari kumsaini mchezaji wa pili Islam Slimani mwezi Januari. Ranieri alimsaini mchezaji huyo wa miaka 30 raia wa Algeria wakati akiwa meneia wa Foxes. (Telegraph)

Ajenti wa kiungo wa kati wa Wolves mreno Ruben Neves anatakana mchenzia huyo mwenye miaka 21 kuhamia Juventus. (Calciomercato - in Italian)

Ruben NevesHaki miliki ya pichaGETTY IMAGES
Image captionRuben Neves

Baba yake Miguel Almiron amesema Newcastle wako nafasi nzuri ya kumsaini mtoto wake huyo mwenye miaka 24 kutoka Atlanta United mwezi Januari. (Newcastle Chronicle)

Leeds na Aston Villa watajaribu kumsaini kipa Karl Darlow mwezi ujao. Mchezaji huyo mwenye miaka 28 alipoteza nafasi yake huko Newcastle na amecheza mechi moja peke yake msimu huu. (Sun)


Mlinzi wa zamani wa England na BT Sport pundit Rio Ferdinand alimtaja mlinzi wa Manchester City mwenye miaka 28 Kyle Walker kuwa tegemeo kubwa wakati City walishindwa na Chelsea siku ya Jumamozi kwa mabao 2-0. (Independent)

Kyle WalkerHaki miliki ya pichaGETTY IMAGES
Image captionKyle Walker

Mlinzi wa zamani wa Cardiff Greg Halford, 34, amekuwa akifanya mazoezi na West Brom na atapewa mkataba wa muda mfupi na klabu hiyo. (WalesOnline)

Meneja wa Liverpool Jurgen Klopp amethibitisha kuwa hataifunza Italia hivi karibuni na kupuuza maswali kuwa Nopoli wanataka huduma zake wakati akiwa huko Dortmund. (Liverpool Echo)

Wing'a wa Bayern Munich Mholanzi Arjen Robben, 34, anasema atastaafu ikiwa ofa ya sasa haitafanikiwa wakati mkataba wake utamalizika msimu huu. (Goal)

West Bromwich Albion wanataka kumsaini kuiungo wa kati wa Leicester na Wales Andy King, 30, kwa mkopo mwezi Januari. (Mail)

Victor MosesHaki miliki ya pichaGETTY IMAGES
Image captionVictor Moses

Chelsea watamuuza Victor Moses mwezi ujao huku Crystal Palace na Fulham wakitaka kutoa ofa zao kwa mchezaji huyo anayewekewa thamani ya pauni milioni 12 mwenye miaka 27 ambaye mchezaji wa zamani wa kimataifa wa Nigeria. (Sun)

Barcelona wanamfuatilia mshambualjia wa Everton raia Brazil Richarlison, 21. (Star)

Kiungo wa kati wa kisosi cha Manchester City cha chini ya miaka 21 Phil Foden, 18, anatarajiwa kusaini mkataba wa miaka sita. (Telegraph)

Phil FodenHaki miliki ya pichaGETTY IMAGES
Image captionPhil Foden

Chelsea wanataka kumuongezea mkataba wa miaka 12 mlinzi raia wa Brazil David Luiz, 31, baada ya msimu huu ambao utamwezesha kutafuta kwingine. (Mirror)

Mlinzi wa kikosi cha chini ya miaka 21 wa Everton raia wa England Mason Holgate, 22, ameambiwa kuwa anaweza kuondoka kwa mkopo mwezi Januari. (Mirror)

Marseille wanawatafuta mabeki wawili - Nacho Monreal, 32, wa Arsenal na Alberto Moreno, 26 wa Liverpool wakati wanapanga kuboresha kikosi chao mwezi Januari. (France Football, via Mirror)

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

MAPENZI: Kuna faida na ni muhimu Mpenzi wako kuwa rafiki yako pia

Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi.  Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria.  Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao.  Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...

Urusi: Vikwazo dhidi ya Korea Kaskazini havitafua dafu

MTEULE THE BEST Image caption Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Sergei Lavrov na mwenzeka wa Marekani Rex Tillerson Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Segei Lavrov amemwambia waziri wa ulinzi nchini Marekani Rex Tillerson kwamba kuiwekea vikwazo zaidi Korea Kaskazini hakutafua dafu. Taarifa iliochapishwa na wizara ya kigeni nchini Urusi inasema kuwa wawili hao walizungumza kwa njia ya simu na kushutumu majaribio ya makombora ya hivi karibuni yaliotekelezwa na Pyongyang . Lakini inasema kuwa bwana Lavrov alisisitiza kwamba diplomasia ndio njia ya pekee ya kumaliza wasiwasi katika rasi ya Korea, na kutaka hatua zozote dhidi ya taifa hilo kusitishwa akionya huenda zikasababisha madhara yasiojulikana. Waziri wa ulinzi nchini Marekani amesisitiza kuwa bado kuna fursa ya kidiplomasia katika kukabiliana na Korea Kaskazini. Mapema rais Trump alichapisha ujumbe katika akaunti yake ya Twitter akisema mazungumzo sio suluhisho.

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania Miaka 60 siku kama ya leo ugunduzi mkubwa ulifanyika katika eneo la Olduvai Gorge, kwenye kreta ya Ngorongoro. Wanaakiolojia Louis na Mary Leakey waligundua fuvu la mtu anayeaminika kuwa ni wa kale zaidi waliyompa jina la Zinjanthropus. Ugunduzi huo uliofanyika saa nne asubuhi Julai 22, 1959 kipindi hicho kwenye eneo la Tanganyika ulikuwa wa vipande zaidi ya 100 ukasaidia katika kutambua asili ya watu wa awali duniani. Kabla ya ugunduzi huo, wanasayansi na wanahistoria walikuwa wakiamini kuwa binadamu wa kale walitokea Uchina baada ya ugunduzi wa mafuvu ya kale baina ya 1923 na 1927 nchini humo ya Homo eractus, ama maarufu kama Peking Man. Mafuvu hayo ya Uchina yalikuwa na umri wa takribani miaka 750,000. Mafuvu ya Olduvai eneo ambalo kwa sasa lipo Tanzania wakati wa ugunduzi wake lilikuwa na umri wa takribani miaka milioni 1.75, na hakuna mabaki ya mtu wa kale zaidi ambayo mpaka sasa yamegundul...