Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Vyama 15 vya upinzani vyaungana

Vyama vya upinzani 15 nchini vimeungana kupinga muswada wa marekebisho ya sheria ya vyama vya siasa ambao ulisomwa kwa mara ya kwanza bungeni mwezi uliopita wakati wa mkutano wa 13 wa Bunge.


Baadhi ya viongozi wa vyama vilivyoshiriki kutoa tamko la pamoja


Vyama vilivyoshiriki katika kutoa tamko la pamoja kupinga muswada huo ni CHADEMA, CUF, DP, ACT Wazalendo, NLD, ADC, CCK, UPDP, Chauma, NCCR Mageuzi vikiongozwa na Mwenyekiti wa Chama cha Umma (Chauma), Hashim Rungwe.

Akisoma tamko la pamoja katika mkutano huo, Mwenyekiti wa muungano huo, Hashim Rungwe amesema kuwa wameamua kuichagua siku ya leo ya Uhuru kwakuwa ni siku muhimu ya kukumbukwa kwa nchi japokuwa haijasheherekewa kama ilivyozoeleka.

"Tumeitumia siku ya leo ya Uhuru kutoa tamko hili kwani ni siku muhimu kwa taifa letu na serikali ya awamu ya tano kuendelea kufuta sherehe za Uhuru ambazo Duniani kote ni siku ambayo taifa husheherekea kuzaliwa kwake, " amesema.

Kuhusu msimamo wa umoja huo kwenye sheria hiyo wanayoipinga, Hashim Rungwe ameesema hawatokubali kurudi nyuma katika kupigania haki yao hasa katika suala hili kwani wameona dalili za wazi za kutaka kupokonywa demokrasia yao waliyokuwa nayo.

ā€œTumeona nchi nyingi zimeingia katika vurugu kutokana na wao kudai haki zao kwa nguvu ila sisi hatutaki kufanya hivyo ndiyo maana tumeamua kuudai Uhuru huu kabla hatujapokwa na kuliingiza taifa katika matatizo".

"Tunatoa wito kwa watanzania wote bila kujali rangi, kabila na itikadi zao watuunge mkono katika kuzuia sheria hii kandamizi ili kuzuia vurugu kubwa zinazoweza kutokea siku za usoni," ameongeza.

Pia Rungwe ametaja sababu za kuipinga muswada huo kuwa ni pamoja na kutokuwepo kwa uhuru wa kujiamulia na kutoshirikishwa kikamilifu katika mchakato wa kuandaa muswada huo.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

MAPENZI: Kuna faida na ni muhimu Mpenzi wako kuwa rafiki yako pia

Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi.  Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria.  Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao.  Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...

Urusi: Vikwazo dhidi ya Korea Kaskazini havitafua dafu

MTEULE THE BEST Image caption Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Sergei Lavrov na mwenzeka wa Marekani Rex Tillerson Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Segei Lavrov amemwambia waziri wa ulinzi nchini Marekani Rex Tillerson kwamba kuiwekea vikwazo zaidi Korea Kaskazini hakutafua dafu. Taarifa iliochapishwa na wizara ya kigeni nchini Urusi inasema kuwa wawili hao walizungumza kwa njia ya simu na kushutumu majaribio ya makombora ya hivi karibuni yaliotekelezwa na Pyongyang . Lakini inasema kuwa bwana Lavrov alisisitiza kwamba diplomasia ndio njia ya pekee ya kumaliza wasiwasi katika rasi ya Korea, na kutaka hatua zozote dhidi ya taifa hilo kusitishwa akionya huenda zikasababisha madhara yasiojulikana. Waziri wa ulinzi nchini Marekani amesisitiza kuwa bado kuna fursa ya kidiplomasia katika kukabiliana na Korea Kaskazini. Mapema rais Trump alichapisha ujumbe katika akaunti yake ya Twitter akisema mazungumzo sio suluhisho.

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania Miaka 60 siku kama ya leo ugunduzi mkubwa ulifanyika katika eneo la Olduvai Gorge, kwenye kreta ya Ngorongoro. Wanaakiolojia Louis na Mary Leakey waligundua fuvu la mtu anayeaminika kuwa ni wa kale zaidi waliyompa jina la Zinjanthropus. Ugunduzi huo uliofanyika saa nne asubuhi Julai 22, 1959 kipindi hicho kwenye eneo la Tanganyika ulikuwa wa vipande zaidi ya 100 ukasaidia katika kutambua asili ya watu wa awali duniani. Kabla ya ugunduzi huo, wanasayansi na wanahistoria walikuwa wakiamini kuwa binadamu wa kale walitokea Uchina baada ya ugunduzi wa mafuvu ya kale baina ya 1923 na 1927 nchini humo ya Homo eractus, ama maarufu kama Peking Man. Mafuvu hayo ya Uchina yalikuwa na umri wa takribani miaka 750,000. Mafuvu ya Olduvai eneo ambalo kwa sasa lipo Tanzania wakati wa ugunduzi wake lilikuwa na umri wa takribani miaka milioni 1.75, na hakuna mabaki ya mtu wa kale zaidi ambayo mpaka sasa yamegundul...