Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Msichana apambana na malaria kwa mishumaa


Yumkini sasa ugonjwa hatari wa malaria unaweza ukawa historia nchini Tanzania, kutokana na mbinu mbalimbali zinazoibuliwa na wananchi wa kawaida kukabiliana na ugonjwa huu sugu katika taifa hilo la Afrika Mashariki.


Serikali imekuwa ikifanya juhudi katika kukabiliana na malaria kwa kunyunyizia dawa za kuuwa viluwiluwi vinavyosababisha ugonjwa huo kwenye makaazi ya watu, kugawa vyandarua vyenye dawa na kutoa elimu kwa wananchi kuhusu kujikinga na ugonjwa huu. 

Licha ya jitihada hizi kusaidia, lakini tatizo la msingi bado liliendelea kuwapo. Nalo ni uwelewa mdogo wa walengwa kwenye kampeni yenyewe. Lakini sasa matumaini ya kutokomeza malaria yamezaliwa upya baada ya kutengenezwa kwa mishumaa inayofukuza mbu, hatua itakayoongeza nguvu katika juhudi za kupambana na ugonjwa huu.

Beatrice Mkama ni mjasiriamali mwenye ndoto za kuisaidia jamii yake katika kuitokomeza malaria iliyosababisha kuondokewa na ndugu zake waliofariki baada ya kuugua ugonjwa huo.

Beatrice, ambaye kitaaluma amesomea uhazili ngazi ya stashahada katika chuo cha Utumishi wa Umma jijini Dar es Salaam, anasema alitamani kujifunza ujasiriamali lakini alishindwa kuamua nini asomee mpaka alipokutana na mkufunzi mmoja kupitia mitandao ya kijamii kutoka Shirika la Kuhudumia Viwanda Vidogo Vidogo (SIDO).


Mjasiriamali Beatrice Mkama akionesha mishumaa anayoitengeneza.


"Tuliambiwa mwalimu huyo alikuwa anafundisha kutengeneza mishumaa, kichwani nilijua nakwenda kupata kitu kipya. Nilivyokuwa naangalia mishumaa, nilikuwa napata maswali inakuwaje utambi unakaa katikati?"

Hata hivyo, Beatrice na wenzake sita hawakufahamu kama mwalimu huyo alikuwa akifundisha utengenezaji wa mishumaa ya mbu. 

"Alipotaja kufundisha mishumaa hiyo, wote tulivutiwa nayo. Tulijifunza kwa masaa mawili na tulielewa somo".

Tatizo la gharama

Beatrice anasema alianza kutengeneza mishumaa hiyo mwezi Disemba mwaka jana na kuiuza Januari mwaka huu, lakini hadi sasa jamii inayomzunguka imeshindwa kumudu gharama za mishumaa hiyo anayoiuza shilingi 1000 kutokana na familia hizo kuwa na uwezo duni kiuchumi.

"Wanasema bei ni kubwa. Huwa najitahidi kuwaelimisha kuhusu mishumaa hii, ila wanataka iwe bei sawa na mishumaa ya kawaida".
Kutokana na changamoto hiyo, Beatrice huamua kugawa bure baadhi ya mishumaa anayoitengeneza kwa familia hizo ili wajiridhishe jinsi inavyofanya kazi.


Mishumaa ya kupambana na mbu.


"Wanasifu tu, wakiwasha mbu hakuna. Wengine wanahoji mbona hatuoni mbu wakifa? Hii dawa inafukuza mbu sio kila muda utakuwa kwenye chandarua".

Kama ulivyo usemi wa "Nabii hakubaliki kwao", naye Beatrice amefanikiwa kupata wateja nje ya eneo analoishi baada ya kufungua ukurasa wake katika mitandao ya kijamii kujitangaza kwa jina la ā€˜Moonlight_business:ā€™ 


Beatrice Mkama akiweka uji uji wa nta katika kifaa chenye maumbo ya mishumaa katika eneo lake la kazi.


Kutokana na kufanya kazi katika mazingira ambayo sio rasmi na mtaji mdogo, Beatrice hutengeneza mishumaa 100 tu kwa siku, ambapo hutumia dawa aina ya ā€˜stronelaā€™ yenye uwezo wa kuuwa mbu kisha huchanganywa na nta inayotokana na mafuta ya petroli. 

Lengo la Beatrice ni kuona jamii yake ikiondokana na adha ya mbu na kupunguza idadi ya wagonjwa wanaougua malaria mara kwa mara


Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

MAPENZI: Kuna faida na ni muhimu Mpenzi wako kuwa rafiki yako pia

Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi.  Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria.  Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao.  Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...

Urusi: Vikwazo dhidi ya Korea Kaskazini havitafua dafu

MTEULE THE BEST Image caption Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Sergei Lavrov na mwenzeka wa Marekani Rex Tillerson Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Segei Lavrov amemwambia waziri wa ulinzi nchini Marekani Rex Tillerson kwamba kuiwekea vikwazo zaidi Korea Kaskazini hakutafua dafu. Taarifa iliochapishwa na wizara ya kigeni nchini Urusi inasema kuwa wawili hao walizungumza kwa njia ya simu na kushutumu majaribio ya makombora ya hivi karibuni yaliotekelezwa na Pyongyang . Lakini inasema kuwa bwana Lavrov alisisitiza kwamba diplomasia ndio njia ya pekee ya kumaliza wasiwasi katika rasi ya Korea, na kutaka hatua zozote dhidi ya taifa hilo kusitishwa akionya huenda zikasababisha madhara yasiojulikana. Waziri wa ulinzi nchini Marekani amesisitiza kuwa bado kuna fursa ya kidiplomasia katika kukabiliana na Korea Kaskazini. Mapema rais Trump alichapisha ujumbe katika akaunti yake ya Twitter akisema mazungumzo sio suluhisho.

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania Miaka 60 siku kama ya leo ugunduzi mkubwa ulifanyika katika eneo la Olduvai Gorge, kwenye kreta ya Ngorongoro. Wanaakiolojia Louis na Mary Leakey waligundua fuvu la mtu anayeaminika kuwa ni wa kale zaidi waliyompa jina la Zinjanthropus. Ugunduzi huo uliofanyika saa nne asubuhi Julai 22, 1959 kipindi hicho kwenye eneo la Tanganyika ulikuwa wa vipande zaidi ya 100 ukasaidia katika kutambua asili ya watu wa awali duniani. Kabla ya ugunduzi huo, wanasayansi na wanahistoria walikuwa wakiamini kuwa binadamu wa kale walitokea Uchina baada ya ugunduzi wa mafuvu ya kale baina ya 1923 na 1927 nchini humo ya Homo eractus, ama maarufu kama Peking Man. Mafuvu hayo ya Uchina yalikuwa na umri wa takribani miaka 750,000. Mafuvu ya Olduvai eneo ambalo kwa sasa lipo Tanzania wakati wa ugunduzi wake lilikuwa na umri wa takribani miaka milioni 1.75, na hakuna mabaki ya mtu wa kale zaidi ambayo mpaka sasa yamegundul...