Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Rais Mnangagwa wa Zimbabwe aizuru Tanzania kukuza uhusiano

Rais Mnangagwa alikaribishwa rasmi na mwenyeji wake rais John Magufuli

Rais wa Zimbabwe Emmerson Mnangagwa yuko Dar es salaam katika ziara ya kwanza nchini humo tangu aingie madarakani.


Ni ziara ya siku mbili ambayo imetajwa kulenga kuimarisha uhusiano wa kidiplomasia kati ya mataifa hayo mawili kwa mujibu wa wizara ya mambo ya nje.


Katika taarifa kwa vyombo vya habari, mwenyeji rais wa Tanzania John Pombe Magufuli na Rais Mnangagwa wamekubaliana kuimarisha biashara na uwekezaji baina ya mataifa hayo mawili yaliotajwa kuwa na udugu wa kihistoria.


Mnangagwa amewasili asubuhi hii na kupokewa na rais Magufuli katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.


Akiwa Tanzania kiongozi huyo anatarajiwa kutembelea chuo cha kilimo alikosomea miongoni mwa wapiganjiaji uhuru waliotoka nchi za kusini mwa Afrika.


Kukuza uhusiano wa Zimbabwe na Tanzania:


Tanzania ilikuwa na jukumu muhimu katika mataifa ya Afrika yaliojikomboa dhidi ya utawala wa wazungu.


Makao makuu ya muungano wa Afrika wakati huo ukijulikana kama (OAU), yalikuwa mjini Dar es Salaam ambapo mikakati iliidhinishwa kumegua utawala wa kikoloni katika nchi za Afrika.


Katika taarifa kutoka ikulu Tanzania, Rais Magufuli amesema wamekubaliana tume ya pamoja ya ushirikiano, iliyokutana mwisho mnamo 1998, ikutane mara baada ya uchaguzi mkuu wa Zimbabwe mwezi ujao ili kujadili vikwazo na kutafuta majawabu ya kukuza biashara na uwekezaji baina ya Mataifa haya mawili.


Mchambuzi wa masuala ya kisiasa Tanzania, Said Msonga anaamini huenda Rais Mnangagwa anatumia ziara hii kama mbinu ya kutaka kuibua hisia za wanamchi na kutaka kuonekana mzalendo na kumtengenezea mazingira ya kushinda uchaguzi.



Kadhalika anaeleza huenda hii ni fursa kwake kuweza kuyahifadhi mahusiano kati ya mataifa hayo mawili baada ya uchaguzi.


Rais Magufuli na Rais Mnangagwa wamekubaliana kuimarisha biashara na uwekezaji baina ya mataifa hayo mawili

Na kuwa na manufaaa ya kiuchumi na kidiplomasia kwa nchi zote mbili.


Itakumbukwa kwamba Rais Magufuli alikuwa miongoni mwa viongozi wa Afrika waliompongeza rais Mnangagwa kwa kuchukua uongozi wa nchi pasi kushuhudia ghasia za aina yoyote.


Ziara hii inafuata mualiko rasmi kwa Mnangagwa kutoka rais Magufuli uliowasilishwa na ujumbe wa chama tawala CCM ulioongozwa na aliyekuwa katibu mkuu Abdulrahman Kinana waliokwenda Zimbabwe mwezi uliopita.



Kinana alifanya ziara hii mwishoni mwa mwezi may kabla ya kuachia ngazi kama katibu mkuu wa CCM.


Mnangagwa, aliingia madarakani mnamo Novemba kufuatia mapinduzi ya jeshi dhidi ya kiongozi mkongwe Robert Mugabe.


Uchaguzi mkuu nchini Zimbabwe wa kwanza baada ya utawala wa Mugabe unatarajiwa Julai 30


Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

MAPENZI: Kuna faida na ni muhimu Mpenzi wako kuwa rafiki yako pia

Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi.  Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria.  Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao.  Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...

Urusi: Vikwazo dhidi ya Korea Kaskazini havitafua dafu

MTEULE THE BEST Image caption Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Sergei Lavrov na mwenzeka wa Marekani Rex Tillerson Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Segei Lavrov amemwambia waziri wa ulinzi nchini Marekani Rex Tillerson kwamba kuiwekea vikwazo zaidi Korea Kaskazini hakutafua dafu. Taarifa iliochapishwa na wizara ya kigeni nchini Urusi inasema kuwa wawili hao walizungumza kwa njia ya simu na kushutumu majaribio ya makombora ya hivi karibuni yaliotekelezwa na Pyongyang . Lakini inasema kuwa bwana Lavrov alisisitiza kwamba diplomasia ndio njia ya pekee ya kumaliza wasiwasi katika rasi ya Korea, na kutaka hatua zozote dhidi ya taifa hilo kusitishwa akionya huenda zikasababisha madhara yasiojulikana. Waziri wa ulinzi nchini Marekani amesisitiza kuwa bado kuna fursa ya kidiplomasia katika kukabiliana na Korea Kaskazini. Mapema rais Trump alichapisha ujumbe katika akaunti yake ya Twitter akisema mazungumzo sio suluhisho.

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania Miaka 60 siku kama ya leo ugunduzi mkubwa ulifanyika katika eneo la Olduvai Gorge, kwenye kreta ya Ngorongoro. Wanaakiolojia Louis na Mary Leakey waligundua fuvu la mtu anayeaminika kuwa ni wa kale zaidi waliyompa jina la Zinjanthropus. Ugunduzi huo uliofanyika saa nne asubuhi Julai 22, 1959 kipindi hicho kwenye eneo la Tanganyika ulikuwa wa vipande zaidi ya 100 ukasaidia katika kutambua asili ya watu wa awali duniani. Kabla ya ugunduzi huo, wanasayansi na wanahistoria walikuwa wakiamini kuwa binadamu wa kale walitokea Uchina baada ya ugunduzi wa mafuvu ya kale baina ya 1923 na 1927 nchini humo ya Homo eractus, ama maarufu kama Peking Man. Mafuvu hayo ya Uchina yalikuwa na umri wa takribani miaka 750,000. Mafuvu ya Olduvai eneo ambalo kwa sasa lipo Tanzania wakati wa ugunduzi wake lilikuwa na umri wa takribani miaka milioni 1.75, na hakuna mabaki ya mtu wa kale zaidi ambayo mpaka sasa yamegundul...