Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Sera ya uhamiaji ya Ulaya itamfaa Merkel au Seehofer?


Mkutano mdogo wa kilele ambao ulioandaliwa Brussels kujadili sera ya uhamiaji na uliofanyika kwa ombi la Kansela wa Ujerumani Angela Merkel, ambaye alikuwa kwenye shinikizo nchini mwake, haukutoa maamuzi yoyote.


Lakini hotuba za viongozi wa nchi 16 waliohudhuria zinaashiria safari inakoelekea. Swali ni iwapo hatua zilizopangwa kuchukuliwa zitamsaidia Merkel katika mzozo na Waziri wake wa mambo ya ndani Horst Seehofer au iwapo mwanasiasa huyo wa chama cha Christian Social Union, CSU, atanufaika zaidi.


Seehofer anasisitiza suluhisho la muda mfupi la wanaotafuta hifadhi kukataliwa kuingia Ujerumani wanapofika mpakani. Angela Merkel naye matumaini yake ya suluhisho ni maafikiano yatakayotokana na mazungumzo baina ya nchi kuhusu suala la kuwarudisha wahamiaji hao walikotoka. Mkutano huo wa Brussels ulitoa mapendekezo kadhaa na je mapendekezo haya yatakuwa na athari gani kwa siasa za ndani za Ujerumani?


Baadhi ya nchi zinataka kubuniwe vituo vya mapokezi ya wakimbizi Libya


Pendekezo la kwanza lilikuwa kuongeza usalama wa mpaka mkubwa wa nchi za Umoja wa Ulaya. Kutimiza hili, walinzi wapya 10,000 wanastahili kusajiliwa kufikia mwaka 2021 kujiunga na shirika la ulinzi wa mipaka la Umoja wa Ulaya Frontex. Lakini swali ni je, walinzi hawa wanastahili kuilinda Ulaya dhidi ya nani?


Baadhi ya viongozi 16 waliohudhuria mkutano mdogo wa kilele Brussels


Je, wanastahili kuwazuia wakimbizi, wanaotafuta hifadhi na wahamiaji wote? Iwapo ni hivyo basi walinzi wengi zaidi watahitajika ili kuulinda mpaka wa majini katika bahari ya mediterenia. Pendekezo hili halitokuwa na athari kubwa katika mzozo unaoendelea katika serikali ya muungano ya Merkel kwani ni jambo linalohitaji muda na Horst Seehofer anataka hatua za haraka zichukuliwe.




Kuna wazo la kubuni vituo vya mapokezi ya wahamiaji vitakavyokuwa nje ya Ulaya. Austria na nchi nyengine zinalipigia debe wazo hili ambapo wanataka vituo hivyo viwekwe nchini Libya au kwengineko Kaskazini mwa Afrika ili kuwachukua wahamiaji, wakimbizi na watafuta hifadhi watakapookolewa kutoka bahari ya Mediterenia. Katika vituo hivyo watakaguliwa kubaini ni nani mwenye nafasi ya kupewa hifadhi na ni nani asiyestahili. Wazo hili si jipya kwa kuwa lilipendekezwa miaka 14 iliyopita na Otto Schily mwanasiasa wa chama cha Social Democratic, SPD hapa Ujerumani. Waziri Seehofer haoni kwamba wazo hili ni baya ingawa tatizo ni kwamba huenda likachukua miezi kama si miaka kutekelezwa.


Kuwarejesha wahamiaji walikotoka ni baadhi ya mapendekezo mengine


Mkutano huo wa Brussels pia ulitoa wazo la kurudishwa makwao wanaotafuta hifadhi. Lengo la wazo hili ni kuwarudisha angalau asilimia 70 ya wanaotafuta hifadhi katika nchi zao na Halmashauri Kuu ya Umoja wa Ulaya imekuwa ikitaka hili lifanyike.


Wahamiaji kutoka Afrika katika bahari ya Mediterenia


Ujerumani, Italia na nchi nyengine bado hazijatimiza hili. Nchini Ujerumani suala hili limejikokota kutokana na masuala ya kisheria. Mapendekezo mengine yalikuwa ni kuwarejesha wahamiaji walikotoka pindi tu wanapofika mpakani na nchi husika kufanya  mazungumzo baina yao ili kutafuta suluhu, hilo likiwa ndilo jambo linalopigiwa debe na Kansela Merkel. Huenda Seehofer akayapenda mapendekezo yote haya ila ni sharti yatekelezwe kwa haraka.


Kiujumla Kansela Merkel hajapata suluhu la "Umoja wa Ulaya". Sasa kinachosubiriwa ni Mkutano wa Kilele wa Umoja wa Ulaya utakaofanyika Alhamis na Ijumaa ambapo nchi zote 28 zitakuwepo. Baada ya hapo Seehofer wa chama cha CSU ataamua iwapo atajitenga na kuihatarisha serikali ya mseto ambapo vyama vya Christian Democratic Union, CDU, na SPD ndivyo vitakavyosalia


Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

MAPENZI: Kuna faida na ni muhimu Mpenzi wako kuwa rafiki yako pia

Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi.  Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria.  Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao.  Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...

Urusi: Vikwazo dhidi ya Korea Kaskazini havitafua dafu

MTEULE THE BEST Image caption Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Sergei Lavrov na mwenzeka wa Marekani Rex Tillerson Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Segei Lavrov amemwambia waziri wa ulinzi nchini Marekani Rex Tillerson kwamba kuiwekea vikwazo zaidi Korea Kaskazini hakutafua dafu. Taarifa iliochapishwa na wizara ya kigeni nchini Urusi inasema kuwa wawili hao walizungumza kwa njia ya simu na kushutumu majaribio ya makombora ya hivi karibuni yaliotekelezwa na Pyongyang . Lakini inasema kuwa bwana Lavrov alisisitiza kwamba diplomasia ndio njia ya pekee ya kumaliza wasiwasi katika rasi ya Korea, na kutaka hatua zozote dhidi ya taifa hilo kusitishwa akionya huenda zikasababisha madhara yasiojulikana. Waziri wa ulinzi nchini Marekani amesisitiza kuwa bado kuna fursa ya kidiplomasia katika kukabiliana na Korea Kaskazini. Mapema rais Trump alichapisha ujumbe katika akaunti yake ya Twitter akisema mazungumzo sio suluhisho.

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania Miaka 60 siku kama ya leo ugunduzi mkubwa ulifanyika katika eneo la Olduvai Gorge, kwenye kreta ya Ngorongoro. Wanaakiolojia Louis na Mary Leakey waligundua fuvu la mtu anayeaminika kuwa ni wa kale zaidi waliyompa jina la Zinjanthropus. Ugunduzi huo uliofanyika saa nne asubuhi Julai 22, 1959 kipindi hicho kwenye eneo la Tanganyika ulikuwa wa vipande zaidi ya 100 ukasaidia katika kutambua asili ya watu wa awali duniani. Kabla ya ugunduzi huo, wanasayansi na wanahistoria walikuwa wakiamini kuwa binadamu wa kale walitokea Uchina baada ya ugunduzi wa mafuvu ya kale baina ya 1923 na 1927 nchini humo ya Homo eractus, ama maarufu kama Peking Man. Mafuvu hayo ya Uchina yalikuwa na umri wa takribani miaka 750,000. Mafuvu ya Olduvai eneo ambalo kwa sasa lipo Tanzania wakati wa ugunduzi wake lilikuwa na umri wa takribani miaka milioni 1.75, na hakuna mabaki ya mtu wa kale zaidi ambayo mpaka sasa yamegundul...