Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Mtandao wa JamiiForums wafunguliwa tena Tanzania


Mwanzilishi mwenza wa Jamii Forums Maxence Melo

Jukwaa maarufu nchini Tanzania JamiiForums hatimaye limefunguliwa baada ya kufungwa kwa takriban wiki mbili, kufuatia kuanza kutekelezwa kwa sheria mpya za mtandaoni nchini humo.


Kulingana na ujumbe uliosambazwa katika ukurasa wa Twitter wa tovuti hiyo, kwa sasa ujumbe ambao ulikuwa umepakiwa awali unaweza kusomwa.


Mkurugenzi wa mtandao huo Maxence Melo aliyekuwa akijibu ujumbe wa mmoja wa wateja wake katika mtandao wa Twitter amenukuliwa katika ujumbe huo akisema hata hivyo kwamba watumiaji wa mtandao huo hawawezi kuchapisha ujumbe mpya kwa sasa.


Aliongezea kusema kwamba hatua za kurejesha operesheni zote kama ilivyokuwepo mwanzo zinaendelea.



Kwa sasa habari za mtandao huo ambazo zilikuwa zimechapishwa kuanzia 10 Juni kwenda nyuma kabla ya kufungwa kwa jukwaa hilo zinaweza kusomwa.


Hata hivyo haijajulikana ni lini operesheni kamili za mtandao huo zitaanza ili wasomaji kuanza kuchangia.


Walipofunga mtandao huo, taarifa zote zilizokuwa zimepakiwa kwenye mtandao huo zilikuwa hazipatikana.


Wasimamizi wake walikuwa wameweka tangazo la kuwajulisha kuhusu kuathiriwa kwa mtandao huo na kanuni mpya za serikali.


"Kwa wateja wetu walio nchi nyingine, huduma hii itarejea mapema zaidi lakini kwa walio Tanzania kurejea kwa huduma kutategemeana na matokeo ya hatma ya jitihada za wawakilishi wetu walio Tanzania," walikuwa wameandika.


"Tunasikitika kuwa tunalazimika kufikia hatua hii ghafla lakini ni matumaini yetu kuwa wateja wetu mtaendelea kuwa wavumilivu katika kipindi hiki."


Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania TCRA ilikuwa imetoa agizo kwa kwa wahudumu wote ambao bado walikuwa hawajapata leseni kukoma kutoa huduma zenye maudhui mtandaoni.



Mwisho wa ujumbe wa Twitter wa @NevilleMeena

Mtandao huo wa Tanzania ni maarufu kwa kufichua mambo mbalimbali na kama jukwaa la watu kutoa maoni haswa wale walio nchini Tanzania na nchi za kigeni.


Sheria hizo mpya za TCRA ziliwahitaji wachapishaji wa mitandao na wanablogi kufichua wachangiaji na wamiliki kitu ambacho Bw Melo anasema kuwa ni kizingiti kwa kazi yao.


Hivi majuzi mtandao huo ulijitenga na mtandao mwengine unaotumia jina kama hilo nchini Kenya.


Mike Mushi, mwanzilishi mwenza wa Jamii Forums alikuwa awali ameambia BBC kwamba kanuni hizo za TCRA, ambazo zinawataka wachapishaji wa taarifa zenye maudhui mtandaoni kuhifadhi maelezo ya wachangiaji kwa miezi 12 huenda zikaathiri mtandao wa Jamii Forums.


"Sheria hizi zinaenda kinyume na jinsi sisi huendesha shughuli zetu. Huwa twawaruhusu watumiaji wetu kuandika ujumbe bila majina yao kutambulishwa, hivyo itatulazimu kufikiria kwa kina iwapo tutaweza kuendeleza kuendesha shughuli zetu."




Alisema mtandao huo kufikia Aprili ulikuwa na watumiaji 3.7 milioni kwa mwezi na walikuwa wanapokea ujumbe takriban 20,000 kila siku.


Na muda mfupi baada ya kufungwa kwa mtandao huo pamoja na tovuti nyengine tofauti nchini humo, Chama cha upinzani Tanzania ACT Wazalendo kilisema mwenendo wa serikali kudhibiti mitandao ya kijamii unaonesha nia ya kutaka kuminya haki zote za msingi za raia.


Akizungumza na waandishi wa habari makao makuu ya chama hicho jijini Dar es Salaam, Katibu Mwenezi wa chama hicho Ado Shaibu alisema ''taratibu kila mtu, haijalishi ni wa chama au cheo gani, atafikiwa na ukandamizaji huu wa serikali''.


Chama cha Upinzanzi nchini Tanzania, ACT Wazalendo, kilisema kuanza kwa kutekelezwa kwa kanuni za maudhui mtandaoni ni ishara nyingine ya jinsi ambavyo serikali nchini humo inaendelea kuminya uhuru wa habari na watu kujieleza.



Mambo muhimu kuhusu kanuni za mitandao Tanzania

Rais Magufuli alitoa agizo la kumchukulia hatua kali za kisheria mtu yeyote atakayechapisha habari za uongozi kuhusu serikali katika mitandao ya kijamii.


Idadi ya watumiaji wa mitandao nchini Tanzania ilipanda hadi asilimia 16 (watu 23 milioni) mwaka 2017. Hiyo ni sawa na asilimia 44 ya raia wa Tanzania.


Wengi hutumia simu kupata huduma za mtandao.


Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

MAPENZI: Kuna faida na ni muhimu Mpenzi wako kuwa rafiki yako pia

Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi.  Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria.  Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao.  Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...

Urusi: Vikwazo dhidi ya Korea Kaskazini havitafua dafu

MTEULE THE BEST Image caption Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Sergei Lavrov na mwenzeka wa Marekani Rex Tillerson Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Segei Lavrov amemwambia waziri wa ulinzi nchini Marekani Rex Tillerson kwamba kuiwekea vikwazo zaidi Korea Kaskazini hakutafua dafu. Taarifa iliochapishwa na wizara ya kigeni nchini Urusi inasema kuwa wawili hao walizungumza kwa njia ya simu na kushutumu majaribio ya makombora ya hivi karibuni yaliotekelezwa na Pyongyang . Lakini inasema kuwa bwana Lavrov alisisitiza kwamba diplomasia ndio njia ya pekee ya kumaliza wasiwasi katika rasi ya Korea, na kutaka hatua zozote dhidi ya taifa hilo kusitishwa akionya huenda zikasababisha madhara yasiojulikana. Waziri wa ulinzi nchini Marekani amesisitiza kuwa bado kuna fursa ya kidiplomasia katika kukabiliana na Korea Kaskazini. Mapema rais Trump alichapisha ujumbe katika akaunti yake ya Twitter akisema mazungumzo sio suluhisho.

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania Miaka 60 siku kama ya leo ugunduzi mkubwa ulifanyika katika eneo la Olduvai Gorge, kwenye kreta ya Ngorongoro. Wanaakiolojia Louis na Mary Leakey waligundua fuvu la mtu anayeaminika kuwa ni wa kale zaidi waliyompa jina la Zinjanthropus. Ugunduzi huo uliofanyika saa nne asubuhi Julai 22, 1959 kipindi hicho kwenye eneo la Tanganyika ulikuwa wa vipande zaidi ya 100 ukasaidia katika kutambua asili ya watu wa awali duniani. Kabla ya ugunduzi huo, wanasayansi na wanahistoria walikuwa wakiamini kuwa binadamu wa kale walitokea Uchina baada ya ugunduzi wa mafuvu ya kale baina ya 1923 na 1927 nchini humo ya Homo eractus, ama maarufu kama Peking Man. Mafuvu hayo ya Uchina yalikuwa na umri wa takribani miaka 750,000. Mafuvu ya Olduvai eneo ambalo kwa sasa lipo Tanzania wakati wa ugunduzi wake lilikuwa na umri wa takribani miaka milioni 1.75, na hakuna mabaki ya mtu wa kale zaidi ambayo mpaka sasa yamegundul...