Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Mnangagwa:Uchaguzi utafanyika kama ilivyopangwa


Mnangagwa amesema uchaguzi uko palepale

Rais wa Zimbabwe, Emmerson Mnangagwa amesema uchaguzi utafanyika kama ilivyopangwa tarehe 30 mwezi Julai, ingawa kulitokea alichokiita jaribio la kukatiza uhai wake lililotokea siku ya Jumamosi.


Katika hatua nyingine, msemaji wa Polisi, Charity Charamba amevitaka vyombo vya habari na Umma kujitokeza iwapo wana picha za video za tukio la mlipuko wakati huu ambapo uchunguzi unafanyika.


Amwewaambia wanahabari mjini Harare kuwa zawadi nono itatolewa kwa taarifa itakayotolewa kusaidia kwenye uchunguzi wao.Idadi ya waliojeruhiwa sasa imefika 49 na Polisi na idara za usalama ziko katika uwanja wa White City eneo ambalo mlipuko ulitokea.


Watu walijeruhiwa kutokana na mlipuko uliotokea kwenye mkutano wa hadhara mjini Bulawayo, tukio lililotokea karibu kabisa na Mnangagwa wakati akiondoka jukwaani.


Maafisa wamesema masuala ya usalama yataangaliwa tena.


mchakato wa uchaguzi unaotarajiwa ni wa kwanza tangu aliyekuwa Rais wa nchi hiyo Robert Mugabe kuondolewa madarakani na kurithiwa na Mnangagwa.


Mnangagwa alisema kuwa mlipuko ulitokea baada ya kitu ''kulipuka hatua chache na nilipokuwa-lakini muda wangu haujafika''.


amesema kuwa ghasia hazina maana na ametoa wito wa kuwepo umoja.




Kiongozi wa upinzani, Nelson Chamisa pia amekemea shambulio hilo,akisema kuwa machafuko ya kisiasa ''hayakubaliki''.


Waliojeruhiwa kwenye shambulio hilo ni pamoja na makamu wa rais wawili, Mwenyekiti wa Chama cha Zanu-PF, wanahabari wa Televisheni ya taifa na maafisa wa usalama.


Rais wa nchi hiyo alikuwa mjini Bulawayo, mji wa pili wa nchini humo na ngome ya upinzani, kwa ajili ya kufanya kampeni kwa ajili ya chama chake cha Zanu-PF wakelekea kwenye uchaguzi wa mwezi Julai


Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

MAPENZI: Kuna faida na ni muhimu Mpenzi wako kuwa rafiki yako pia

Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi.  Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria.  Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao.  Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...

Urusi: Vikwazo dhidi ya Korea Kaskazini havitafua dafu

MTEULE THE BEST Image caption Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Sergei Lavrov na mwenzeka wa Marekani Rex Tillerson Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Segei Lavrov amemwambia waziri wa ulinzi nchini Marekani Rex Tillerson kwamba kuiwekea vikwazo zaidi Korea Kaskazini hakutafua dafu. Taarifa iliochapishwa na wizara ya kigeni nchini Urusi inasema kuwa wawili hao walizungumza kwa njia ya simu na kushutumu majaribio ya makombora ya hivi karibuni yaliotekelezwa na Pyongyang . Lakini inasema kuwa bwana Lavrov alisisitiza kwamba diplomasia ndio njia ya pekee ya kumaliza wasiwasi katika rasi ya Korea, na kutaka hatua zozote dhidi ya taifa hilo kusitishwa akionya huenda zikasababisha madhara yasiojulikana. Waziri wa ulinzi nchini Marekani amesisitiza kuwa bado kuna fursa ya kidiplomasia katika kukabiliana na Korea Kaskazini. Mapema rais Trump alichapisha ujumbe katika akaunti yake ya Twitter akisema mazungumzo sio suluhisho.

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania Miaka 60 siku kama ya leo ugunduzi mkubwa ulifanyika katika eneo la Olduvai Gorge, kwenye kreta ya Ngorongoro. Wanaakiolojia Louis na Mary Leakey waligundua fuvu la mtu anayeaminika kuwa ni wa kale zaidi waliyompa jina la Zinjanthropus. Ugunduzi huo uliofanyika saa nne asubuhi Julai 22, 1959 kipindi hicho kwenye eneo la Tanganyika ulikuwa wa vipande zaidi ya 100 ukasaidia katika kutambua asili ya watu wa awali duniani. Kabla ya ugunduzi huo, wanasayansi na wanahistoria walikuwa wakiamini kuwa binadamu wa kale walitokea Uchina baada ya ugunduzi wa mafuvu ya kale baina ya 1923 na 1927 nchini humo ya Homo eractus, ama maarufu kama Peking Man. Mafuvu hayo ya Uchina yalikuwa na umri wa takribani miaka 750,000. Mafuvu ya Olduvai eneo ambalo kwa sasa lipo Tanzania wakati wa ugunduzi wake lilikuwa na umri wa takribani miaka milioni 1.75, na hakuna mabaki ya mtu wa kale zaidi ambayo mpaka sasa yamegundul...