Ruka hadi kwenye maudhui makuu

AFCON 2019: Taifa Stars hati hati kufuzu baada ya kukubali kichapo dhidi ya Lesotho


Tanzania sasa itahitajika kuwafunga Uganda na kuomba Lesotho wafungwe na Cape Verde ili wao wafuzu

Ndoto za Tanzania kushiriki mashindano ya kandanda kwa timu za taifa bara la Afrika (Afcon) zimekumbana na dhoruba kali.

Timu ya Tanzania, maarufu kama Taifa Stars hapo jana jioni, Novemba 18 ilihitaji alama tatu dhidi ya Lesotho ili kufuzu katika fainali hizo zitakazopigwa mwakani Cameroon kwa mara ya kwanza toka mwaka 1980.

Stars inayonolewa na nyota wa zamani wa Nigeria Emmanuel Amunike iliingia dimbani huku mashabiki wake wakiwa na Imani kubwa juu ya timu yao.



Laiti Stars ingepata ushindi wa namna yeyote ile wangefikisha alama nane ambazo Cape Verde na Lesotho wasingeweza kuzifikia.

Tayari Uganda the Cranes wamefuzu kupitia kundi hilo la L kwa kufikisha alama 13 ambazo haziwezi kufikiwa na timu nyengine yeyote.

Uganda ilifuzu baada ya kuifunga Cape Verde goli 1 bila majibu. Hayo yalikuwa matokeo ambayo Watanzania walikuwa wakiyaombea sababu Cape Verde ilisalia na alama zake nne.

Kitumbua cha Tanzania kiliingia mchanga katika dakika ya 76 kwa goli la kichwa la Nkau Lerotholi.

Baada ya matokeo hayo, sasa Lesotho imefikisha alama 5 sawa na Tanzania huku Cape Verde akishuka mpaka mkiani kwa alama zao 4.

Ili Tanzania wafuzu itabidi waifunge Uganda katika mchezo wa mwisho wa kundi hilo utakaopigwa mwezi wa Machijijini Dar es Salaam na kuomba Cape Vede waifunge Lesotho.

Matokeo ya Tanzania kufungwa yameibua hisia tofauti japo si siri kuwa kila Mtanzania ameumizwa moyoni.

Baadhi wametaka watu kutulia na kuelekeza nguvu kwenye mchezo ujao dhidi ya Uganda.

Zitto Kabwe Ruyagwa


āœ”@zittokabwe

Kwa Watanzania na wapenzi wa soka, ninajua tumeumizwa sana na matokeo ya leo. Hata hivyo hatupaswi kuvunjika moyo kwani Bado tuna nafasi kubwa kwenda #AFCON2019. Kwa wachezaji wa #Taifastars mimi binafsi Bado nina matumaini nanyi. Mungu anataka tushindie nyumbani. Tutashinda

713

7:37 PM - Nov 18, 2018

Twitter Ads info and privacy


160 people are talking about this

Twitter Ads info and privacy

Mwisho wa ujumbe wa Twitter wa @zittokabwe

Wapo ambao wanataka Taifa Stars warudi na kwenda kubangua korosho. Mmoja anayetaka adhabu hiyo itekelezwa ni Mkuu wa Wilaya ya Kisarawe, Jokate Mwegelo.

Jokate Mwegelo


āœ”@jokateM

Kubangua korosho kunawahusu aisee.

1,040

7:11 PM - Nov 18, 2018 Ā· Dar es Salaam, Tanzania

Twitter Ads info and privacy


227 people are talking about this

Twitter Ads info and privacy

Mwisho wa ujumbe wa Twitter wa @jokateM

Mashabiki na baadhi ya wachambuzi wanambebesha mzigo wa lawama kocha Amunike wakiamini hakupanga kikosi kizuri ambacho kingeweza kuleta ushindi. Mmoja anayeamini hivyo ni Waziri wa Maliasili na Utalii Khamis Kigwangalla.


Dr. Kigwangalla, H.

āœ”@HKigwangalla

Leo nimechukua muda kwa shauku na uzalendo mkuu kufuatilia timu yangu ya Taifa, presha niliyokuwa nayo ni ya hatari, mara tunakoswa koswa, mara paap, tumelizwa; na hapa nipo namsubiria Bwana Emmanuel Amunike kama hivi...

484

8:38 PM - Nov 18, 2018 Ā· Dodoma, Tanzania


165 people are talking about this

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

MAPENZI: Kuna faida na ni muhimu Mpenzi wako kuwa rafiki yako pia

Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi.  Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria.  Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao.  Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...

Urusi: Vikwazo dhidi ya Korea Kaskazini havitafua dafu

MTEULE THE BEST Image caption Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Sergei Lavrov na mwenzeka wa Marekani Rex Tillerson Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Segei Lavrov amemwambia waziri wa ulinzi nchini Marekani Rex Tillerson kwamba kuiwekea vikwazo zaidi Korea Kaskazini hakutafua dafu. Taarifa iliochapishwa na wizara ya kigeni nchini Urusi inasema kuwa wawili hao walizungumza kwa njia ya simu na kushutumu majaribio ya makombora ya hivi karibuni yaliotekelezwa na Pyongyang . Lakini inasema kuwa bwana Lavrov alisisitiza kwamba diplomasia ndio njia ya pekee ya kumaliza wasiwasi katika rasi ya Korea, na kutaka hatua zozote dhidi ya taifa hilo kusitishwa akionya huenda zikasababisha madhara yasiojulikana. Waziri wa ulinzi nchini Marekani amesisitiza kuwa bado kuna fursa ya kidiplomasia katika kukabiliana na Korea Kaskazini. Mapema rais Trump alichapisha ujumbe katika akaunti yake ya Twitter akisema mazungumzo sio suluhisho.

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania Miaka 60 siku kama ya leo ugunduzi mkubwa ulifanyika katika eneo la Olduvai Gorge, kwenye kreta ya Ngorongoro. Wanaakiolojia Louis na Mary Leakey waligundua fuvu la mtu anayeaminika kuwa ni wa kale zaidi waliyompa jina la Zinjanthropus. Ugunduzi huo uliofanyika saa nne asubuhi Julai 22, 1959 kipindi hicho kwenye eneo la Tanganyika ulikuwa wa vipande zaidi ya 100 ukasaidia katika kutambua asili ya watu wa awali duniani. Kabla ya ugunduzi huo, wanasayansi na wanahistoria walikuwa wakiamini kuwa binadamu wa kale walitokea Uchina baada ya ugunduzi wa mafuvu ya kale baina ya 1923 na 1927 nchini humo ya Homo eractus, ama maarufu kama Peking Man. Mafuvu hayo ya Uchina yalikuwa na umri wa takribani miaka 750,000. Mafuvu ya Olduvai eneo ambalo kwa sasa lipo Tanzania wakati wa ugunduzi wake lilikuwa na umri wa takribani miaka milioni 1.75, na hakuna mabaki ya mtu wa kale zaidi ambayo mpaka sasa yamegundul...