Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Hizi ndiyo njia za kulinda mafanikio yako

Maeneo nane unayotakiwa kuyatawala kiuhakika ili ufanikiwe


Ushindi wowote katika mafanikio unapatikana kwa kutawala. Kwa mfano, Ili uweze kufanikiwa katika biashara unatakiwa kuitawala biashara hiyo katika kila eneo, kwa kuijua biashara hiyo ndani nje tena kwa uhakika. 

Hata katika mafanikio kwa ujumla vipo vitu ambavyo unatakiwa kuvitawala, kwa jinsi unavyovitawala vitu hivyo unapata uhakika wa mafanikio kwa asilimia kubwa sana. Je, ni mambo yapi ambayo unatakiwa kuyatawala ili kufanikiwa? 

1. Jitawale wewe kwanza. 
Kitu cha kwanza ambacho unatakiwa kukitawala vizuri ili ujijengee mafanikio ni kujua jinsi ya kujitawala wewe. Tambua jinsi ya kutawala fikra zako, matendo yako, vitu unavyosoma au kuangalia, imani na mitazamo uliyonayo juu ya maisha ya mafanikio. 

Kwa kujua jinsi ya kutawala hayo mambo inakusaidia sana wewe kuweza kufanikiwa na kupiga hatua. Watu wanaofanikiwa wanajua sana jinsi ya kujitawala wao wenyewe hasa kutokana na kumudu kutawala mambo kama hayo kila wakati. 

2. Tawala mihemko yako. 
Kujitawala wewe tu hiyo haitoshi, ni muhimu kujua jinsi ya kutawala mihemko yako. Huwezi kufanikiwa kama unashindwaa kutawala mihemko yako. Hapa inabidi ujue kutawala tamaa zako au kujizuia kwa mambo yanayokuangusha kimafanikio. 

Kama ukishindwa kutawala mihemko yako ni wazi utashindwa. Ipo mihemko ya aina tofauti kama mihemko ya kununua vitu hovyo, au mihemko anasa zisizo na mbele wala nyuma. Kikubwa jiangalie una mihemko ipi wewe inayokuangusha? 

3. Tawala visingizio vyako. 
Kila wakati fanya ufanyalo, lakini hakikisha  usiwe tu mtu wa visingizio, tawala visingizio vyako na kila aina ya visinguio weka pembeni. Usiwe mtu kila unaposhindwa jambo unasingizia kwamba umeshinsddwa kwa sababu hii au ile. 

Kama jambo umeshindwa kweli ni bora ukaa kimya na uache kusingizia singizia vitu kwani huwezi kukosa sababu. Ukiweza kutawala sababu zako, ukiweza kutawala visingizo vyako, basi anza kujihakikishia mafanikio yako. 

4. Tawala maono yako. 
Najau zipo ndoto au maono ambayo unayo na kila  siku unaomba Mungu hayo maono yako yaje yatimie. Sasa jifunze jinsi yakutawala maono yako. Maono hayo yaweke kwenye karatasi au picha na ikiwezekana uwe unayaona mara kwa mara. 

Weka utaratibu wa kujikumbusha kila siku na kwa kujikumbusha huko inakusaidia kutawala sana maono hayo kwa sehemu kubwa. Wengi wanaoshindwa kufanikiwa, ni watu ambao kiuhalisia wanashindwa kutawala maono yao kwa sehemu kubwa sana. 

5. Tawala sheria za mafanikio. 
Hata kama hujui lakini naomba nikwambie kwamba, zipo sheria zinazotawla mafanikio unayoyatafuta. Kwa bahati mbaya sana sheria hizo zinafanya kazi eidha uwe unajua au hujui lakini sheria hizo zipo kazini muda wote. 

Wale wanaoshindwa ni watu ambao wanashindwa sana pia kumudu kutumia sheria za mafanikio. Unatakiwa kujua jinsi ya kutawala sheria za mafanikio ili ziweze kukupa mafanikio ya uhakika. Ukishindwa kufanya hivyo ujue utakwama kufikia ndoto zako. 

6. Tawala watu wanaokushauri. 
Kila mtu ana mtu anayemshauri katika jambo fulani hivi liwe la mafanikio au la kawaida. Wengi sasa kwa bahati mbaya wana washauri wabovu, yaani wanashauriwa na watu wasio sahihi kwa lugha nyingine watu hao wanawapoteza. 

Kwa hiyo ili kufanikiwa kitu ambacho unatakiwa kukitawala vizuri na kukipe mafanikio ni kutawala washauri. Tafauta washauri ambao watakusaidia wewe kufanikiwa na si washauri watakokupoteza wewe na kukufanya uonekane hufai. 

7. Tawala muda wako. 
Kutawala muda ni jambo gumu sana kwa watu wengi kulifanya. Watu wengi wanashindwa kutawala muda wao na matokeo yake muda wanaupoteza sana kwa mambo ya hovyo ili mradi tu muda huo umepotezwa pasipo malengo. 

Kwa mfano; kuna wanaopoteza muda wao katika soga, kuna wanaopotezea muda wao kufanya kazi ambazo si zao badala wangefanya kazi zao ambazo zingewapeleka na kuwapa mafanikio makubwa ya kimaisha kwa sehemu kubwa sana. 

8. Tawala mipango yako. 
Ile mipango uliyonayo hautakiwi kuiacha tu hivi hivi hewani, unatakiwa kujua jinsi ya kuitawala mipango yako na ukapata mafanikio makubwa. Kila wakati jikumbushe mipango yako ni ipi na utaifatilia vipi hadi ifanikiwe. 

Unapokuwa unajua hatma kama hizi za mipango uliyonayo, hicho ni kichochezi cha kukupa wewe nguvu ya kuweza kusonga mbele zaidi kwenye mafanikio. Watu wengi wenye mafanikio wana uwezo wa kutawala pia mipango yao sana na kuimudu. 

Fanyia kazi haya na chukua hatua kuhakikisha ndoto zako zinatimia

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

MAPENZI: Kuna faida na ni muhimu Mpenzi wako kuwa rafiki yako pia

Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi.  Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria.  Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao.  Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...

Urusi: Vikwazo dhidi ya Korea Kaskazini havitafua dafu

MTEULE THE BEST Image caption Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Sergei Lavrov na mwenzeka wa Marekani Rex Tillerson Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Segei Lavrov amemwambia waziri wa ulinzi nchini Marekani Rex Tillerson kwamba kuiwekea vikwazo zaidi Korea Kaskazini hakutafua dafu. Taarifa iliochapishwa na wizara ya kigeni nchini Urusi inasema kuwa wawili hao walizungumza kwa njia ya simu na kushutumu majaribio ya makombora ya hivi karibuni yaliotekelezwa na Pyongyang . Lakini inasema kuwa bwana Lavrov alisisitiza kwamba diplomasia ndio njia ya pekee ya kumaliza wasiwasi katika rasi ya Korea, na kutaka hatua zozote dhidi ya taifa hilo kusitishwa akionya huenda zikasababisha madhara yasiojulikana. Waziri wa ulinzi nchini Marekani amesisitiza kuwa bado kuna fursa ya kidiplomasia katika kukabiliana na Korea Kaskazini. Mapema rais Trump alichapisha ujumbe katika akaunti yake ya Twitter akisema mazungumzo sio suluhisho.

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania Miaka 60 siku kama ya leo ugunduzi mkubwa ulifanyika katika eneo la Olduvai Gorge, kwenye kreta ya Ngorongoro. Wanaakiolojia Louis na Mary Leakey waligundua fuvu la mtu anayeaminika kuwa ni wa kale zaidi waliyompa jina la Zinjanthropus. Ugunduzi huo uliofanyika saa nne asubuhi Julai 22, 1959 kipindi hicho kwenye eneo la Tanganyika ulikuwa wa vipande zaidi ya 100 ukasaidia katika kutambua asili ya watu wa awali duniani. Kabla ya ugunduzi huo, wanasayansi na wanahistoria walikuwa wakiamini kuwa binadamu wa kale walitokea Uchina baada ya ugunduzi wa mafuvu ya kale baina ya 1923 na 1927 nchini humo ya Homo eractus, ama maarufu kama Peking Man. Mafuvu hayo ya Uchina yalikuwa na umri wa takribani miaka 750,000. Mafuvu ya Olduvai eneo ambalo kwa sasa lipo Tanzania wakati wa ugunduzi wake lilikuwa na umri wa takribani miaka milioni 1.75, na hakuna mabaki ya mtu wa kale zaidi ambayo mpaka sasa yamegundul...