AY Athibitisha Kumiliki Mjengo Calabasas, Marekani



Loading...

Mwanamuziki mkongwe wa muziki wa Bongo fleva Ambwene Yesaya maarufu kama AY amethibitisha kumiliki mjengo wa kifahari nchini Marekani katika maeneo ya Calabasas.

Katika mahojiano aliyofanya na Global Publishers AY  amethibitisha kwamba akili yake inafikiri mbali zaidi nay eye ni wa anga za kimataifa, naye aka­nunua Mjengo maeneo ya Calabasas ingawa hajataka kufafanua gharama zake.



Ni kweli nimefanikiwa kupata nyumba Calaba­sas na ndipo yatakuwa makazi yangu, ninamiliki nyumba mbili ikiwemo hiyo ya Marekani na moja Tanzania,na pia ninamiliki magari manne“.


AY anakuwa Kama ametisha hivi kwani eneo ambalo amenunua mjengo Wake ni eneo wanalokaa washua na mastaa wakubwa wenye pesa zao Kama vile Kim Kardashian, Kanye West, Drake Justin Bieber na wengineo wengi.

 

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

ZIJUWE SHERIA 17 ZA SOKA

MAPENZI: Kuna faida na ni muhimu Mpenzi wako kuwa rafiki yako pia

KUMTUMAINIA MUNGU