Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Watanzania washauriwa kukopa

Dkt. Mwakyembe : Woga wa kukopa ni tatizo kubwa kwa Watanzania




Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dk. Harrison Mwakyembe amesema Watanzania waache kuogopa kukopa lakini benki nazo zibadilike. 

Dkt. Mwakyembe amesema, woga wa kukopa ni tatizo kubwa kwa Watanzania na ni la kihistoria kwa kuwa zamani kuliko na sheria iliyowazuia wazawa wasikope kwa sababu iliwatambua kuwa ni watoto. 

Waziri Mwakyembe amewaeleza wajumbe wa Jukwaa la Fursa za Biashara Mkoa wa Tabora hali sasa imebadilika hivyo wananchi wakope wawekeze. 

Tabora inabidi ibadilike hasa, isiwe Tabora ile ya maembe tunagawana na wadudu” amesema na pia amewaeleza viongozi kuwa uongozi si umasikini. 

Dkt. Mwakyembe amesema, viongozi hawazuiwi kuwa matajiri ila watapaswa kueleza wameupata vipi utajiri huo na ndiyo maana kuna suala la maadili kwa viongozi wa umma. 

Mwakyembe alikuwa Mwenyekiti wa Jukwaa la Fursa za Biashara Tabora lililofanyika kwa siku tatu mjini Tabora. Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa alilifungua jukwaa hilo juzi. 

Viongozi mbalimbali wamehudhuria jukwaa la Tabora akiwemo Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji Joseph Kakunda, wabunge kutoka mkoani humo, Mwenyekiti wa Bodi ya Kampuni ya Magazeti ya Serikali, Hab Mkwizu, na Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Tabora, Hassan Wakasuvi.

Viongozi wengine waliohudhuria jukwaa hilo ni wakuu wa wilaya, watendaji wakuu wa mkoa huo, wakurugenzi watendaji wa Halmashauri, makatibu tawala wa wilaya, wenyeviti wa halmashauri za wilaya, wakuu wa taasisi na waendai wengine mkoani humo

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

MAPENZI: Kuna faida na ni muhimu Mpenzi wako kuwa rafiki yako pia

Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi.  Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria.  Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao.  Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania Miaka 60 siku kama ya leo ugunduzi mkubwa ulifanyika katika eneo la Olduvai Gorge, kwenye kreta ya Ngorongoro. Wanaakiolojia Louis na Mary Leakey waligundua fuvu la mtu anayeaminika kuwa ni wa kale zaidi waliyompa jina la Zinjanthropus. Ugunduzi huo uliofanyika saa nne asubuhi Julai 22, 1959 kipindi hicho kwenye eneo la Tanganyika ulikuwa wa vipande zaidi ya 100 ukasaidia katika kutambua asili ya watu wa awali duniani. Kabla ya ugunduzi huo, wanasayansi na wanahistoria walikuwa wakiamini kuwa binadamu wa kale walitokea Uchina baada ya ugunduzi wa mafuvu ya kale baina ya 1923 na 1927 nchini humo ya Homo eractus, ama maarufu kama Peking Man. Mafuvu hayo ya Uchina yalikuwa na umri wa takribani miaka 750,000. Mafuvu ya Olduvai eneo ambalo kwa sasa lipo Tanzania wakati wa ugunduzi wake lilikuwa na umri wa takribani miaka milioni 1.75, na hakuna mabaki ya mtu wa kale zaidi ambayo mpaka sasa yamegundul...

Urusi: Vikwazo dhidi ya Korea Kaskazini havitafua dafu

MTEULE THE BEST Image caption Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Sergei Lavrov na mwenzeka wa Marekani Rex Tillerson Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Segei Lavrov amemwambia waziri wa ulinzi nchini Marekani Rex Tillerson kwamba kuiwekea vikwazo zaidi Korea Kaskazini hakutafua dafu. Taarifa iliochapishwa na wizara ya kigeni nchini Urusi inasema kuwa wawili hao walizungumza kwa njia ya simu na kushutumu majaribio ya makombora ya hivi karibuni yaliotekelezwa na Pyongyang . Lakini inasema kuwa bwana Lavrov alisisitiza kwamba diplomasia ndio njia ya pekee ya kumaliza wasiwasi katika rasi ya Korea, na kutaka hatua zozote dhidi ya taifa hilo kusitishwa akionya huenda zikasababisha madhara yasiojulikana. Waziri wa ulinzi nchini Marekani amesisitiza kuwa bado kuna fursa ya kidiplomasia katika kukabiliana na Korea Kaskazini. Mapema rais Trump alichapisha ujumbe katika akaunti yake ya Twitter akisema mazungumzo sio suluhisho.