Bondia, Ibrahim Class wa Tanzania

Bondia, Ibrahim Class wa Tanzania  amepeperusha vyema bendera ya taifa baada ya kutetea ubingwa wake wa dunia katika uzito Mwepesi kwa kumtandika Koos Sebia wa Afrika kusini kwa alama katika pambano lilofanyika uwanja wa Uhuru jijini Dar es salaam .
Mgeni rasmi katika pambano hilo alikuwa Waziri wa Habari,Utamaduni, Sanaa na Michezo Dkt. Harrison Mwakyembe, ambaye amewataka vijana kote nchini kujiandaa vyema kabla ya kushiriki mchezo wowote  kama wanataka kushinda kama alivyofanya Ibrahim Class.
Kwa upande wake Ibrahim Class amesema,ataendelea kucheza kwa bidii katika mapambano yake ili aendelee kutamba katika anga za kimataifa.


Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

ZIJUWE SHERIA 17 ZA SOKA

MAPENZI: Kuna faida na ni muhimu Mpenzi wako kuwa rafiki yako pia

KUMTUMAINIA MUNGU