Bondia, Ibrahim Class wa Tanzania amepeperusha vyema bendera ya taifa baada ya kutetea ubingwa wake wa dunia katika uzito Mwepesi kwa kumtandika Koos Sebia wa Afrika kusini kwa alama katika pambano lilofanyika uwanja wa Uhuru jijini Dar es salaam .
Mgeni rasmi katika pambano hilo alikuwa Waziri wa Habari,Utamaduni, Sanaa na Michezo Dkt. Harrison Mwakyembe, ambaye amewataka vijana kote nchini kujiandaa vyema kabla ya kushiriki mchezo wowote kama wanataka kushinda kama alivyofanya Ibrahim Class.
Kwa upande wake Ibrahim Class amesema,ataendelea kucheza kwa bidii katika mapambano yake ili aendelee kutamba katika anga za kimataifa.
Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi. Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria. Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao. Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...
Maoni