Uteuzi wa Alan Pardew (kulia) una maana kwamba sasa yeye na Tony Pulis wamekuwa wakufunzi wa West Brom na Crystal Palace Ligi ya Premia
West Brom wamemteua meneja wa zamani wa Newcastle na Crystal Palace Alan Pardew kuwa meneja wao mpya.
West Brom walimfuta kazi Tony Pulis mnamo 20 Novemba baada yao kucheza mechi 10 Ligi ya Premia bila kushinda mechi hata moja.
Walikuwa alama moja pekee juu ya eneo la kushushwa daraja.
Pardew, 56, amekuwa bila kazi tangu alipofutwa na Crystal Palace Desemba 2016.
Ametia saini mkataba wa kudumu hadi msimu wa 2019-20, na sasa amekuwa meneja wa sita kuteuliwa Albion tangu 2011.
"Nimefurahishwa sana na fursa hii ambayo nimepewa na Albion na nasubiri kwa hamu kuanza kazi na kikosi ambacho ninaamini kina wachezaji wenye vipaji sana," Pardew amesema.
"Kibarua cha kwanza kitakuwa kupata matokeo yatakayotuinua kwenye jedwali."
Mechi yake ya kwanza usukani itakuwa dhidi ya Palace ligini uwanjani Hawthorns Jumamosi, 2 Desemba (15:00 GMT).
Albion kisha watasafiri Liverpool na Swansea kabla ya kucheza nyumbani dhidi ya Manchester United.
Pardew, ambaye amewahi kuwa mkufunzi Reading, West Ham, Charlton na Southampton katika kipindi cha miaka 18 alishindwa fainali Kombe la FA mara mbili akiwa meneja.
Alitawazwa meneja bora wa mwaka na mameneja 2012 baada ya Newcastle kumaliza nafasi ya tano ligini.
Pardew Ligi ya Premia
Pardew alishinda 34.3% ya mechi Ligi ya Premia akiwa Palace, ukilinganisha na 37.4% akiwa Newcastle, 36.4% akiwa West Ham na 26.3% Charlton
Ushindi wake kwa jumla Ligi ya Premia ni 35.8%
Akiwa na Palace, Pardew aliibuka meneja wa kwanza Ligi ya Premia kuongoza klabu kumaliza nusu ya juu kwenye jedwali baada ya kuwa sehemu ya kushushwa daraja Krismasi.
Pardew amesimamia mechi 302.
Utata wa Pardew
Akiwa na West Ham mwaka 2006, Pardew alizozana na meneja wa Arsenal Arsene Wenger.
Januari 2014, alimtusi meneja wa Manchester City Manuel Pellegrini akiwa meneja Newcastle.
Everton wanakaribia kumteua Sam Allardyce kuwa meneja wao mpya.
2017-11-29T13:42:03+00:00
Everton wanakaribia kumteua Sam Allardyce kuwa meneja wao mpya.
Mazungumzo kati ya klabu hiyo na meneja huyo yanaendelea vyema na yanaaminika kuwa karibu kuzaa matunda.
Hii ni licha ya taarifa Ureno kudokeza kwamba Everton wamevutiwa na meneja wa Shakhtar Donetsk Paulo Fonseca.
Meneja wa muda wa Everton David Unsworth anatarajiwa kuongoza klabu hiyo mechi yao ya nyumbani Ligi ya Premia dhidi ya West Ham leo usiku.
Lakini klabu hiyo huenda ikathibitisha Allardyce kuwa mrithi wa Ronald Koeman kabla ya mechi hiyo.
Koeman alifutwa na Everton mnamo 23 Oktoba baada ya klabu hiyo kushuka hadi nafasi ya 18 baada ya kuchapwa 5-2 na Arsenal nyumbani.
Allardyce, 63, alikuwa amejiondoa kutoka kwneye kinyang'anyiro cha kutaka kumrithi Koeman baada ya kukosa kupokea ofa kutoka kwa Everton mapema Novemba.
Lakini baada ya kwenda mechi saba - wakishinda moja pekee - chini ya Unsworth, ikiwa ni pamoja na kuchapwa 5-1 nyumbani na Atalanta na kushindwa 4-1 ugenini Southampton Jumapili, Everton walifufua mazungumzo na Allardyce wikendi
Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi. Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria. Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao. Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...
Maoni