RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, ATEMBELEA BANDARINI, LEO JUMAPILI NOVEMBA 26,2017.
_______________________________
RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Joseph Magufuli, mapema Leo Jumapili Novemba 26,2017, ametembelea na kukagua Sehemu ya Bandari na kukuta mrudikano wa magari zaidi ya 50, yanayodaiwa kuwa ni ya Polisi, na kwamba yaliagizwa na Ofisi ya Rais miaka miwili(02) iliyopita, tangu Juni,2015 na mtu asiyejulikana, huku Viongozi wote wakuu wa Mamlaka ya Bandari, POLISI, TAKUKURU, TRA na Vikosi mbalimbali wakikana kuyafahamu magari hayo.
Baada ya sintofahamu hiyo, Mhe. Rais Dkt. John Pombe Joseph Magufuli, amesema magari hayo yaliingizwa kinyemela nchini, kupitia uagizaji wa magari ya Polisi, na hivyo kuliagiza Jeshi la Polisi kuyatoa haraka, magari hayo, na kuwataka Mawaziri wake kushirikiana na kuwasiliana katika ufanyaji kazi wao.
......."Naomba haya magari ikibidi yagawiwe kwenye Mawizara ya Serikali ikibidi"........ Mhe. Rais Dkt. John Pombe Joseph Magufuli, huku akimpa maelezo zaidi IGP,
........."IGP kwenye ofisi yako kuna madudu sana, ila nimekuweka wewe pale ili uyafukue na kuondoa madudu pale ofisini kwako hata kama ni rafiki yako"..............
Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi. Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria. Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao. Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...
Maoni