Rais wa Tanzania John Pombe Magufuli ni miongoni mwa viongozi mbali mbali duniani watakaohudhuria kuapishwa kwa rais wa Kenya Uhuru Kenyatta
Rais Uhuru Kenyatta wa Kenya na mwenzake wa Tanzania John Pombe Magufuli
Rais wa Tanzania John Pombe Magufuli ni miongoni mwa viongozi mbali mbali duniani watakaohudhuria kuapishwa kwa rais wa Kenya Uhuru Kenyatta.
Katika taarifa iliotiwa sahihi na mkurugenzi wa idara ya habari, maelezo na msemaji mkuu wa serikali Hassan Abbas, Magufuli atajumuika na viongozi wengine katika kushuhudia kuapishwa kwa rais Kenyatta aliyeibuka mshindi katika uchaguzi wa marudio uliofanyika tarehe 26 mwezi Novemba.
''Serikali inautaarifu umma kuwa rais wa Jamhuri ya Tanzania John Pombe magufuli ataungana na viongozi wa mataifa mbalimbali kuhudhuria sherehe za kuapishwa kwa mheshimiwa Uhuru Kenyatta kuwa rais wa kipindi cha awamu ya pili'', ilisema taarifa hiyo.
Iliongezea kwamba '' Muheshimiwa Kenyatta ataapishwa siku ya Jumanne Novemba 28 2017 jijini Nairobi baada ya ushindi alioupata katika uchaguzi wa marudio uliofanyika Oktoba 26 mwaka huu nchini humo''
Maandilizi ya kuapishwa kwa Uhuru Kenyatta siku ya Jumanne yamekamilika na usalama utawekwa kwa wale watakaoshiriki kulingana na kamati ya maandalizi.
Sherehe hiyo inatarajiwa kugharimu shilingi milioni 300 za Kenya huku ikidaiwa kuwa kiwango kikubwa cha fedha hizo kitawekwa katika kuimarisha usalama.
Mwaka 2013 wakati ambapo rais Kenyatta alikuwa akiapishwa kwa mara ya kwanza, kamati ya maandalizi ya sherehe hiyo ilitaka kupewa shilingi bilioni 1.2 ambazo wizara ya fedha baadaye ilizipunguza na kufikia shilingi milioni 374 huku shilingi milioni 64 zikitolewa na idara ya mahakama.
Rais Magufuli ni rafiki wa karibu wa kiongozi wa upinzani nchini Kenya ambaye alisusia uchaguzi huo Raila Amolo Odinga.
Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi. Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria. Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao. Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...
Maoni