Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Rais Magufuli kuhudhuria kuapishwa kwa Uhuru Kenyatta


Rais wa Tanzania John Pombe Magufuli ni miongoni mwa viongozi mbali mbali duniani watakaohudhuria kuapishwa kwa rais wa Kenya Uhuru Kenyatta

Rais Uhuru Kenyatta wa Kenya na mwenzake wa Tanzania John Pombe Magufuli
Rais wa Tanzania John Pombe Magufuli ni miongoni mwa viongozi mbali mbali duniani watakaohudhuria kuapishwa kwa rais wa Kenya Uhuru Kenyatta.
Katika taarifa iliotiwa sahihi na mkurugenzi wa idara ya habari, maelezo na msemaji mkuu wa serikali Hassan Abbas, Magufuli atajumuika na viongozi wengine katika kushuhudia kuapishwa kwa rais Kenyatta aliyeibuka mshindi katika uchaguzi wa marudio uliofanyika tarehe 26 mwezi Novemba.
''Serikali inautaarifu umma kuwa rais wa Jamhuri ya Tanzania John Pombe magufuli ataungana na viongozi wa mataifa mbalimbali kuhudhuria sherehe za kuapishwa kwa mheshimiwa Uhuru Kenyatta kuwa rais wa kipindi cha awamu ya pili'', ilisema taarifa hiyo.
Iliongezea kwamba '' Muheshimiwa Kenyatta ataapishwa siku ya Jumanne Novemba 28 2017 jijini Nairobi baada ya ushindi alioupata katika uchaguzi wa marudio uliofanyika Oktoba 26 mwaka huu nchini humo''
Maandilizi ya kuapishwa kwa Uhuru Kenyatta siku ya Jumanne yamekamilika na usalama utawekwa kwa wale watakaoshiriki kulingana na kamati ya maandalizi.
Sherehe hiyo inatarajiwa kugharimu shilingi milioni 300 za Kenya huku ikidaiwa kuwa kiwango kikubwa cha fedha hizo kitawekwa katika kuimarisha usalama.
Mwaka 2013 wakati ambapo rais Kenyatta alikuwa akiapishwa kwa mara ya kwanza, kamati ya maandalizi ya sherehe hiyo ilitaka kupewa shilingi bilioni 1.2 ambazo wizara ya fedha baadaye ilizipunguza na kufikia shilingi milioni 374 huku shilingi milioni 64 zikitolewa na idara ya mahakama.
Rais Magufuli ni rafiki wa karibu wa kiongozi wa upinzani nchini Kenya ambaye alisusia uchaguzi huo Raila Amolo Odinga.


Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

MAPENZI: Kuna faida na ni muhimu Mpenzi wako kuwa rafiki yako pia

Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi.  Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria.  Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao.  Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...

Urusi: Vikwazo dhidi ya Korea Kaskazini havitafua dafu

MTEULE THE BEST Image caption Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Sergei Lavrov na mwenzeka wa Marekani Rex Tillerson Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Segei Lavrov amemwambia waziri wa ulinzi nchini Marekani Rex Tillerson kwamba kuiwekea vikwazo zaidi Korea Kaskazini hakutafua dafu. Taarifa iliochapishwa na wizara ya kigeni nchini Urusi inasema kuwa wawili hao walizungumza kwa njia ya simu na kushutumu majaribio ya makombora ya hivi karibuni yaliotekelezwa na Pyongyang . Lakini inasema kuwa bwana Lavrov alisisitiza kwamba diplomasia ndio njia ya pekee ya kumaliza wasiwasi katika rasi ya Korea, na kutaka hatua zozote dhidi ya taifa hilo kusitishwa akionya huenda zikasababisha madhara yasiojulikana. Waziri wa ulinzi nchini Marekani amesisitiza kuwa bado kuna fursa ya kidiplomasia katika kukabiliana na Korea Kaskazini. Mapema rais Trump alichapisha ujumbe katika akaunti yake ya Twitter akisema mazungumzo sio suluhisho.

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania Miaka 60 siku kama ya leo ugunduzi mkubwa ulifanyika katika eneo la Olduvai Gorge, kwenye kreta ya Ngorongoro. Wanaakiolojia Louis na Mary Leakey waligundua fuvu la mtu anayeaminika kuwa ni wa kale zaidi waliyompa jina la Zinjanthropus. Ugunduzi huo uliofanyika saa nne asubuhi Julai 22, 1959 kipindi hicho kwenye eneo la Tanganyika ulikuwa wa vipande zaidi ya 100 ukasaidia katika kutambua asili ya watu wa awali duniani. Kabla ya ugunduzi huo, wanasayansi na wanahistoria walikuwa wakiamini kuwa binadamu wa kale walitokea Uchina baada ya ugunduzi wa mafuvu ya kale baina ya 1923 na 1927 nchini humo ya Homo eractus, ama maarufu kama Peking Man. Mafuvu hayo ya Uchina yalikuwa na umri wa takribani miaka 750,000. Mafuvu ya Olduvai eneo ambalo kwa sasa lipo Tanzania wakati wa ugunduzi wake lilikuwa na umri wa takribani miaka milioni 1.75, na hakuna mabaki ya mtu wa kale zaidi ambayo mpaka sasa yamegundul...