Ruka hadi kwenye maudhui makuu

NDOA SIYO MCHEZO

NDOA ni shule pekee ambayo unapata cheti kabla ya kuanza masomo. Ni shule ambayo kamwe hauwezi kuhitimu.
Ni shule ambayo unatakiwa kuhudhuria siku zote za uhai wako. Ni shule ambayo hakuna likizo ya kuumwa au sikukuu.
Ni shule ambayo iligunduliwa na Mungu katika misingi ifuatayo;
1. Msingi wa upendo.
2. Kuta za shule zimejengwa kwa "uaminifu"
3. Madirisha yametengenezwa kwa "uvumilivu"
4. Samani zimetengenezwa kwa "msamaha"
5. Na ikaizekwa kwa "Imani"
Ukumbuke kuwa wewe ni mwanafunzi tu na sio mkuu wa shule ya NDOA. Mungu ndio Mkuu wa Shule.
Hata wakati wa mapito, majaribu, kimbunga na misukosuko ya hapa na pale usikimbie nje ya shule.
Kamwe usiende kulala kabla hujamaliza homework yako. Kamwe usisahau kusoma somo la mawasiliano. Wasiliana na mwanafunzi mwenzio pamoja na Mwalimu mkuu.
Kama utaona kuna kitu kwa mwanafunzi mwenzako ambacho kimsingi haukipendi, basi ukumbuke mwenzako nae ni mwanafunzi na sio mhitimu mwalimu Mkuu bado hajamalizana nae. Hivyo ichukulie ni changamoto na muifanyie kazi kwa pamoja.
Msisahau kusoma kitabu kitakatifu kilicho kwenye mtaala wa shule ya Ndoa (Biblia na quran). Najua kuna muda unaweza ukajisikia kutokuhudhuria darasani lakini unatakiwa uhudhurie tu.
Utakapojaribiwa kuacha shule jipe ujasiri wa kuendelea na shule. Najua mitihani mingine ya muhula au nusu muhula inaweza kuwa migumu isiyo na majibu kwako.
Lakini kumbuka Mwalimu Mkuu anayo majibu tayari na anafahamu unaweza ukakabiliana nayo na anaona hiyo ndio shule nzuri kwako kuzidi nyingine.
Ni moja ya shule nzuri kabisa katika ulimwengu huu. Furaha, amani, na upendo husindikiza masomo ya kila siku.
Masomo mbalimbali hutolewa katika shule hii, ila somo kuu kuliko yote ni UPENDO.
Baada ya miaka yote ya kusoma kwa nadharia, ukijiunga na shule hii utasoma kwa vitendo.
Kupendwa ni kitu kizuri, lakini kupenda ni upendeleo wa vyote. Ndoa ni sehemu ya furaha. Inatakiwa kufurahia tofauti zenu na sio tofauti zenu ziwe chanzo cha kutoelewana.
Mimi Tweve Hezron nawatakia kila la kheri wote mliopo kwenye hii shule takatifu. Na sisi ambao bado tumuombe mwenyezi Mungu ambae ni Mkuu wa Shule akatuchagulie wanafunzi wenzetu walio bora ambao tutaweza kujiunga nao katika hii shule nzuri hapa Duniani.
Mkuu wa Shule (MUNGU) awabariki.
MTEULE THE BEST


Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

MAPENZI: Kuna faida na ni muhimu Mpenzi wako kuwa rafiki yako pia

Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi.  Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria.  Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao.  Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...

Urusi: Vikwazo dhidi ya Korea Kaskazini havitafua dafu

MTEULE THE BEST Image caption Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Sergei Lavrov na mwenzeka wa Marekani Rex Tillerson Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Segei Lavrov amemwambia waziri wa ulinzi nchini Marekani Rex Tillerson kwamba kuiwekea vikwazo zaidi Korea Kaskazini hakutafua dafu. Taarifa iliochapishwa na wizara ya kigeni nchini Urusi inasema kuwa wawili hao walizungumza kwa njia ya simu na kushutumu majaribio ya makombora ya hivi karibuni yaliotekelezwa na Pyongyang . Lakini inasema kuwa bwana Lavrov alisisitiza kwamba diplomasia ndio njia ya pekee ya kumaliza wasiwasi katika rasi ya Korea, na kutaka hatua zozote dhidi ya taifa hilo kusitishwa akionya huenda zikasababisha madhara yasiojulikana. Waziri wa ulinzi nchini Marekani amesisitiza kuwa bado kuna fursa ya kidiplomasia katika kukabiliana na Korea Kaskazini. Mapema rais Trump alichapisha ujumbe katika akaunti yake ya Twitter akisema mazungumzo sio suluhisho.

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania Miaka 60 siku kama ya leo ugunduzi mkubwa ulifanyika katika eneo la Olduvai Gorge, kwenye kreta ya Ngorongoro. Wanaakiolojia Louis na Mary Leakey waligundua fuvu la mtu anayeaminika kuwa ni wa kale zaidi waliyompa jina la Zinjanthropus. Ugunduzi huo uliofanyika saa nne asubuhi Julai 22, 1959 kipindi hicho kwenye eneo la Tanganyika ulikuwa wa vipande zaidi ya 100 ukasaidia katika kutambua asili ya watu wa awali duniani. Kabla ya ugunduzi huo, wanasayansi na wanahistoria walikuwa wakiamini kuwa binadamu wa kale walitokea Uchina baada ya ugunduzi wa mafuvu ya kale baina ya 1923 na 1927 nchini humo ya Homo eractus, ama maarufu kama Peking Man. Mafuvu hayo ya Uchina yalikuwa na umri wa takribani miaka 750,000. Mafuvu ya Olduvai eneo ambalo kwa sasa lipo Tanzania wakati wa ugunduzi wake lilikuwa na umri wa takribani miaka milioni 1.75, na hakuna mabaki ya mtu wa kale zaidi ambayo mpaka sasa yamegundul...