Image caption
Somalia Hassan Sheikh Mohamoud alilakiwa na waziri wa usalama wa ndani wa Kenya bwana Joseph Nkaisserry
Alipowasili Daadab rais wa Somalia Hassan Sheikh
Mohamoud alilakiwa na waziri wa usalama wa ndani wa Kenya bwana Joseph
Nkaisserry waziri wa maswala ya nje wa Somalia na Balozi wa Somalia
nchini Kenya miongoni mwa viongozi wengine.
Mwandishi wa BBC
Bashkash Jugsoday aliyeko Garissa nchini Kenya anaelezea alivyopokewa
kwa furaha na bashasha huko Garissa siku ya mwanzo wa mfungo wa
Ramadhan. Image caption
Ziara ya Rais wa Somalia Hassan Sheikh Mohamoud inafuatia shinikizo la kenya kutaka kuifunga kambi hiyo
Kambi hiyo ilizinduliwa yapata miaka ishirini na
tano iliyopita ilikuwapa uhifadhi raia wa Somalia ambao walikuwa
wakitoroka mapigano ya wenyewe kwa wenyewe.
Hata hivyo, hivi karibuni, serikali ya Kenya imesema wakati umefika kwa kambi hiyo kufungwa. Image caption
Rais wa somalia alipokewa na viongozi
Kenya inalalamikia utovu wa usalama kufuatia
habari za kijasusi zilizodai kuwa wanamgambo wa Al Shabaab wanatumia
kambi hiyo ya wakimbizi kubwa zaidi nchini Kenya kupanga mashambulizi ya
kigaidi nchini Kenya.
Awali mpango sawa na huu wa kuwarejesha
kwao wakimbizi haukufaulu huku serikali ya Kenya ikilaumu washirika wake
yaani Serikali ya Somalia naShirika la Umoja wa mataifa
linaloshughulikia maswala ya wakimbizi,UNHCR kwa utepetevu. Image caption
Kambi hiyo ilizinduliwa yapata miaka ishirini na tano iliyopita
Kenya inasisitiza kuwa ina haki ya kimsingi ya
kuwalinda raia wake mbali na kuwa na jukumu la kuwapa hifadhi wakimbizi
ambao sasa wamanza kuhujumu usalama wake.
Aidha Serikali ya Kenya inasema kuwa mazingira yameharibiwa sana katika eneo hilo lenye ukame. Image caption
Kambi hiyo ilizinduliwa yapata miaka ishirini na tano
Juma lililopita Waziri wa usalama wa ndani wa Kenya
bwana Joseph Nkaisserry alikariri kauli ya serikali yake kuwa hakutakuwa
na mazungumzo zaidi kuhusiana na hilo.
Waziri huyo aliambia BBC
kuwa serikali kwa ushirikiano na serikali ya Somalia na kitengo
kinachoshughulikia maswala ya wakimbizi cha Umoja wa Mataifa UNHCR
zitahakikisha uhamisho huo inafanyika kwa njia nzuri. Image caption
Kenya inalalamikia utovu wa usalama
Kenya tayari imetenga takriban dola milioni kumi
kufanikisha shughuli hiyo ambayo inasema kuwa inalenga kuihakikishia
usalama wake kufuatia msururu wa mashambulizi ya kigaidi yanayotekelezwa
na wapiganaji wa kundi la al Shabaab.
SHERIA 17 ZA SOKA ======================= Mchezo wa soka ni moja ya michezo maarufu sana duniani na ni biashara kubwa sana katika ulimwengu wa michezo na ukitaka kuamini hili angalia makampuni yaliyowekeza katika kudhamini soka – ni makampuni makubwa makubwa yenye hadhi ya kitaifa na kimataifa. Kwa kuzingatia aina hii ya wadhamini, waendeshaji wa mchezo wa soka, wameweka kanuni na miongozo ya kufuatwa ili kuhakikisha kuwa wale wanaowekeza pesa zao wanaona thamani ya uwekezaji wao. Kwa hiyo soka kama ilivyo katika michezo mingine inazo kanuni na tutajadili kanuni moja baada ya nyingine kama zilivobainishwa katika muongozo wa FIFA unaojulikana kwa jina la Law of the Game. Sheria Namba 1: Dimba ============== NYASI - Dimba la soka litakuwa la nyasi asilia au bandia kulingana na kanuni za masindano na nyasi hizo lazima ziwe za rangi ya kijani. Kwa dimba la nyasi bandia na kama mchezo unaochezwa utakuwa wa kutambuliwa na FIFA, basi nyasi hizo bandia lazima zikidhi viwango maalumu ...
Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi. Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria. Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao. Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...
MTEULE THE BEST TUMSIFU YESU KRISTO WAPENDWA KATIKA BWANA!!! MADA YA LEO: KUMTUMAINIA MUNGU SOMO; zaburi 11:1-7 Kwake MWENYEZI-MUNGU nakimbilia usalama; mnawezaje basi kuniambia "ruka kama ndege mpaka mlimani" Maana waovu wanavuta pinde wameweka mishale tayari juu ya uta wawapige mshale watu wema gizani! Kama misingi ikiaribiwa mtu mwadilifu atafanya nini? MWENYEZI-MUNGU yumo hekaluni mwake takatifu ; kiti cha enzi cha MWENYEZI-MUNGU kiko mbinguni Kwa macho yake huwachungulia wanadamu na kujua kila kitu wanachofanya MWENYEZI-MUNGU hupima waadilifu na waovu huwachukia kabisa watu wakatili Atawanyeshea waovu makaa ya moto na madini ya kiberti upepo wa hari ndiyo itakuwa adhabu yao MWENYEZI-MUNGU ni mwadilifu na apenda uadilifu watu wanyoofu watakaa pamoja naye NENO LA BWANA Unaruhusiwa kuchangia funguka tupate maoni yako MUNGU AKUBARIKI
Maoni