Obama akutana na Sanders amsifu Hillary

MTEULE THE BEST

 

 Rais Barrack Obama wa Marekani amesema kwenye mahojiano na runinga moja kuwa anatarajia chama chake cha Democratic kitaungana zaidi katika kipindi cha wiki chache zijazo.

Matamshi yake yamejiri baada ya Hillary Clinton kushinda uteuzi wa chama hicho kuwania kiti cha urais, baada ya kushinda idadi ya wajumbe katika uteuzi wa mashinani.
Obama ametaja Bi Clinton kama 'Kiranja shupavu' na wakati huo huo kumpongeza mpinzani wake Bernie Sanders kwa kuendesha kampeini na kujadili masuala muhimu ya kijamii.
Sanders ambaye hajakubali kushindwa, anatarajiwa kukutana na rais Obama baadaye hii leo.
SANDERS  & HILLARY

Sanders ambaye hajakubali kushindwa
Wakati huo huo Obama amesema jukumu lake kuu wakati wa kampeini za uchaguzi mkuu ni kuwakumbusha wapiga kura nchini Marekani, kuwa rais wa Marekani ni kazi ngumu na sio maonyesho ya runinga, hili likimlenga mgombea wa chama cha Republican Donald Trump.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

ZIJUWE SHERIA 17 ZA SOKA

MAPENZI: Kuna faida na ni muhimu Mpenzi wako kuwa rafiki yako pia

KUMTUMAINIA MUNGU