UFARANSA IMEANZA VIZURI Euro2016

MTEULE THE BEST

 

 

Timu ya taifa ya soka nchini Ufaransa imeshinda mechi ya ufunguzi wa dimba la kombe la bara Ulaya baada ya kuinyuka Romania, mabao 2-1, katika uwanja wa Stade de France mjini Paris.

Dimitri Payet wa Ufaransa ambaye anaichezea klabu ya West Ham nchini Uingereza alifunga bao la ushindi katika muda wa lala salama.
Mshambuliaji wa Ufaransa Olivier Giroud alifunga bao la kwanza kwa kichwa muda mfupi tu baada ya kipindi cha pili kung'oa nanga, na baadaye Romania wakazawazisha kwa mkwaju wa penalti kutoka kwa Bogdan Stancu.
 

Euro2016
Usalama umeimarishwa mjini Paris na haswa karibu na uwanja wa Stade de France, ambapo shambulizi baya la kigaidi lilitekelezwa mwaka ulopita.


Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

ZIJUWE SHERIA 17 ZA SOKA

MAPENZI: Kuna faida na ni muhimu Mpenzi wako kuwa rafiki yako pia

KUMTUMAINIA MUNGU