Ruka hadi kwenye maudhui makuu

HENRY, NEVILLE, CARAGHER WATABIRI BINGWA WA EPL, TOP FOUR

MTEULE THE BEST


CaragherKuelekea kuanza kwa msimu mpya wa ligi, wachambuzi wa soka katika kituo cha runinga cha Sky Sports wametoa utabiri wao timu itakayotwaa ubingwa na zile zitakazomaliza katika nafasi nne za juu.
Katika utabiri wao, wachambuzi hao ambao ni Thierry Henry, Gary Neville na Jamie Carragher wameiondoa kabisa Leicester katika kinyangā€™anyiro hicho.
Badala yake, wametupia karata yao ya ubingwa kwa vilabu vya jiji la Manchester. Kitu ambacho kimsingi si cha kushangaza, ukizingatia namna walivyofanya usajili wao kuanzia makocha mpaka wachezaji.
THIERRY HENRY
  1. Man City 2. Man Utd. 3. Chelsea 4. Arsenal
ā€œSiku zote matumaini yangu yapo kwa Arsenal. Lakini nadhani ubingwa utachukuliwa na kati ya City au United. Lakini kwasababu natakiwa kutaja timu moja basi naipa City.
ā€œChelsea hawatakuwa na Michuano yoyote ya Ulaya, hivyo itakuwa faida kwao, lakini inaweza kuchukua muda kidogo kuendana na kile anachowafundisha Conte.
ā€œVivyo hivyo kwa Mourinho na Man Utd. Vilevile City na Guardiola- hivyo basi, labda kuna upenyo kwa Liverpool, Arsenal na Tottenham ā€“ ambao wamekuwa na vikosi vyao vile vile pamoja na makocha wale wale.ā€
GARY NEVILLE
  1. Man Utd 2. Arsenal 3. Man City 4. Liverpool
ā€œUnited wana meneja na wachezaji wawili ambao wana ari kubwa ya ushindi. Uwepo wa Jose Mourinho, Zlatan Ibrahimovic na Paul Pogba ā€“ na wachezaji wengine ambao walikuwepo awali, basi naiona United ikirejea kwenye uimara wake.
ā€œKuna wachezaji ambao wanavaa tisheti za United na kuwaingia kwenye mioyo yao na kupambana kwa nguvu ā€“ na hiyo sasa ndiyo Manchester United inavyopaswa kuwa.
ā€œKwangu mimi, bingwa atakuwa Man Utd, Arsenal nafasi ya pili Arsenal, Manchester City nafasi ya tatu na Liverpool nafasi ya nne.
JAMIE CARRAGHER
  1. Man City 2. Chelsea 3. Man Utd 4. Liverpool
ā€œKwa miaka mingi sana nimekuwa nikisema kwamba City wana kikosi bora, lakini hawafanyi kile kinachotakiwa na nadhani njaa ya mafanikio itarudi tena chini ya utawala wa Pep Guardiola.
ā€œBila shaka, wanahitaji kusajili zaidi, lakini tayari wana wachezaji ambao wako vizuri tangu hapo awali kama David Silva, Sergio Aguero na Kevin De Bruyne. Hawa watatu watakuwa ni mwanga kwa wengine watakaokuja.
ā€œKwa kuwa hawashiriki kwenye michuano yoyote ya Ulaya, nadhani Chelsea watafanya vizuri kwasababu watakuwa na muda mwingi wa kuzoeana mazoezini. Na tukumbuke kwamba ni miezi 12 tu imepita tangu wawe mabingwa, vilvile Antonio Conte ni kocha wa kiwango cha juu.
ā€œNadhani Liverpool pia watanufaika kutokana na kutokuwa na Mashindano ya Ulaya.ā€

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

MAPENZI: Kuna faida na ni muhimu Mpenzi wako kuwa rafiki yako pia

Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi.  Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria.  Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao.  Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...

Urusi: Vikwazo dhidi ya Korea Kaskazini havitafua dafu

MTEULE THE BEST Image caption Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Sergei Lavrov na mwenzeka wa Marekani Rex Tillerson Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Segei Lavrov amemwambia waziri wa ulinzi nchini Marekani Rex Tillerson kwamba kuiwekea vikwazo zaidi Korea Kaskazini hakutafua dafu. Taarifa iliochapishwa na wizara ya kigeni nchini Urusi inasema kuwa wawili hao walizungumza kwa njia ya simu na kushutumu majaribio ya makombora ya hivi karibuni yaliotekelezwa na Pyongyang . Lakini inasema kuwa bwana Lavrov alisisitiza kwamba diplomasia ndio njia ya pekee ya kumaliza wasiwasi katika rasi ya Korea, na kutaka hatua zozote dhidi ya taifa hilo kusitishwa akionya huenda zikasababisha madhara yasiojulikana. Waziri wa ulinzi nchini Marekani amesisitiza kuwa bado kuna fursa ya kidiplomasia katika kukabiliana na Korea Kaskazini. Mapema rais Trump alichapisha ujumbe katika akaunti yake ya Twitter akisema mazungumzo sio suluhisho.

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania Miaka 60 siku kama ya leo ugunduzi mkubwa ulifanyika katika eneo la Olduvai Gorge, kwenye kreta ya Ngorongoro. Wanaakiolojia Louis na Mary Leakey waligundua fuvu la mtu anayeaminika kuwa ni wa kale zaidi waliyompa jina la Zinjanthropus. Ugunduzi huo uliofanyika saa nne asubuhi Julai 22, 1959 kipindi hicho kwenye eneo la Tanganyika ulikuwa wa vipande zaidi ya 100 ukasaidia katika kutambua asili ya watu wa awali duniani. Kabla ya ugunduzi huo, wanasayansi na wanahistoria walikuwa wakiamini kuwa binadamu wa kale walitokea Uchina baada ya ugunduzi wa mafuvu ya kale baina ya 1923 na 1927 nchini humo ya Homo eractus, ama maarufu kama Peking Man. Mafuvu hayo ya Uchina yalikuwa na umri wa takribani miaka 750,000. Mafuvu ya Olduvai eneo ambalo kwa sasa lipo Tanzania wakati wa ugunduzi wake lilikuwa na umri wa takribani miaka milioni 1.75, na hakuna mabaki ya mtu wa kale zaidi ambayo mpaka sasa yamegundul...