Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Mchina apigwa na butwaa kujipata 'alinyongwa'

MTEULE THE BEST

Cheti cha kuthibitisha Chen alinyongwa

Image copyrightGUANGZHOU RADIO AND TELEVISION NETWORK
Image captionDaftari la serikali ya China limemuorodhesha Chen kuwa aliuawa muongo mmoja uliyopita.
Mwanaume mmoja Mchina alipigwa na butwaa alipokwenda kuomba cheti cha nidhamu kwa polisi na kugundua kuwa 'alinyongwa' miaka 10 iliyopita!
Mtu huyo anayejulikana kwa jina moja tu Chen aliachwa kinywa wazi alipojipata katika orodha ya wale waliokufa.
Chen mwenye umri wa miaka 45 aliviambia vyombo vya habari kuwa daftari maalum ya serikali ilimuoredhesha kuwa alinyongwa mwaka wa 2006 kwa makosa ya kumteka nyara mtu na akahukumiwa kinyonga!
kituo cha polisi cha GuangzhouImage copyrightGUANGZHOU RADIO AND TELEVISION NETWORK
Image captionChen alikuwa amepata kazi mjini Guangzhou na alihitaji cheti cha polisi kudhibitisha kuwa alikuwa na nidhamu nzuri kabla ya kupewa kazi.
Chen alikuwa amepata kazi mjini Guangzhou na alihitaji cheti cha kudhibitisha kuwa alikuwa na nidhamu nzuri kabla ya kupewa kazi.
Hata hivyo upekuzi uliofanywa na waandishi habari wapekuzi wa kituo cha runinga cha Guangdong uligundua kuwa kulikuwa na mtu mwenye jina hilo na nambari sawa na zake za kitambulisho aliyehukumiwa kifo.
Chen aliwashangaza wengi alipoelezea jinsi maisha yake yamekuwa shwari hadi hapo alipojipata ''mfu kwa muongo mmoja''
''Mimi hata nilipata cheti cha kusafiria kwenda Hong Kong na Macau sijawahi kushuhudia kitu kama hichi maishani mwangu.''
Maafisa wa polisi katika jimbo la Guangzhou walikiri hitilafu hiyo na kumpa cheti alichohitaji iliaendelee kusukuma gurudumu la maisha.
Bw ChenImage copyrightGUANGZHOU RADIO AND TELEVISION NETWORK
Image captionChen hakutaka kupigwa picha asije akadhulumiwa
Masaibu ya Chen ni mfano tu ya baadhi ya makosa katika daftari la watu nchini China ambayo yameruhusu watu kupewa vitambulisho vilivyotolewa tayari.
Hata hivyo wizara ya usalama wa umma unasema kuwa hiyo ni hitilafu ambayo inaendelea kusahihishwa katika kampeini iliyoanza mwaka wa 2009.
Mwaka huo kulikuwa na watu milioni moja waliokuwa wakitumia vipande bandia bila kujua.


Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

MAPENZI: Kuna faida na ni muhimu Mpenzi wako kuwa rafiki yako pia

Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi.  Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria.  Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao.  Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...

Urusi: Vikwazo dhidi ya Korea Kaskazini havitafua dafu

MTEULE THE BEST Image caption Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Sergei Lavrov na mwenzeka wa Marekani Rex Tillerson Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Segei Lavrov amemwambia waziri wa ulinzi nchini Marekani Rex Tillerson kwamba kuiwekea vikwazo zaidi Korea Kaskazini hakutafua dafu. Taarifa iliochapishwa na wizara ya kigeni nchini Urusi inasema kuwa wawili hao walizungumza kwa njia ya simu na kushutumu majaribio ya makombora ya hivi karibuni yaliotekelezwa na Pyongyang . Lakini inasema kuwa bwana Lavrov alisisitiza kwamba diplomasia ndio njia ya pekee ya kumaliza wasiwasi katika rasi ya Korea, na kutaka hatua zozote dhidi ya taifa hilo kusitishwa akionya huenda zikasababisha madhara yasiojulikana. Waziri wa ulinzi nchini Marekani amesisitiza kuwa bado kuna fursa ya kidiplomasia katika kukabiliana na Korea Kaskazini. Mapema rais Trump alichapisha ujumbe katika akaunti yake ya Twitter akisema mazungumzo sio suluhisho.

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania Miaka 60 siku kama ya leo ugunduzi mkubwa ulifanyika katika eneo la Olduvai Gorge, kwenye kreta ya Ngorongoro. Wanaakiolojia Louis na Mary Leakey waligundua fuvu la mtu anayeaminika kuwa ni wa kale zaidi waliyompa jina la Zinjanthropus. Ugunduzi huo uliofanyika saa nne asubuhi Julai 22, 1959 kipindi hicho kwenye eneo la Tanganyika ulikuwa wa vipande zaidi ya 100 ukasaidia katika kutambua asili ya watu wa awali duniani. Kabla ya ugunduzi huo, wanasayansi na wanahistoria walikuwa wakiamini kuwa binadamu wa kale walitokea Uchina baada ya ugunduzi wa mafuvu ya kale baina ya 1923 na 1927 nchini humo ya Homo eractus, ama maarufu kama Peking Man. Mafuvu hayo ya Uchina yalikuwa na umri wa takribani miaka 750,000. Mafuvu ya Olduvai eneo ambalo kwa sasa lipo Tanzania wakati wa ugunduzi wake lilikuwa na umri wa takribani miaka milioni 1.75, na hakuna mabaki ya mtu wa kale zaidi ambayo mpaka sasa yamegundul...