Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Madaktari wa Mumbai mashakani kwa kuuza figo

MTEULE THE BEST


Uuzaji wa figo India
Image captionUhaba wa viungo ambavyo binadamu wanaweza kupeana umechochea mauzo ya siri ya viungo kote nchini India

Polisi nchini India wamewashtaki madaktari watano makosa yenye uhusiano na biashara ya Figo ya binadamu.Maafisa wa polisi wanasema madaktari hao walihuska katika kisa kimoja ambapo walihusika katika kutoa figo ya binadamu kinyume cha sheria katika Hospitali ya Hiranandani iliyopo magharibi mwa mji wa Mumbai.
Polisi walichunguza hospitali baada ya taarifa kuenea kwamba watu maskini, wengi wao kutoka maeneo ya vijijini, wamekua wakilipwa kuuza figo zao.
Figo jingine lilitolewa kwa binadamu mwezi Juni katika hospitari maarufu mjini Delhi.
Naibu kamishna wa polisi wa Mumbai, Ashok Dudhe, amesema kuwa madaktari walishtakiwa kwasababu "hawakufuata taratibu zilizopo".
"siku mbili zilizopita tulipata ripoti kutoka kwa mkurugenzi wa huduma za afya wa Mumbai. Katika ripoti hii kulikua na mashtaka yaliyotolewa dhidi yamadaktari hawa kama vile uzembe chini ya sheria ya mwaka 1994 ya upasuaji wa viungo vya binadam ," shirika la habari la Reuters lilimkariri Bw Dudhe akielezea.
Aliongeza kusema kuwa watu 14, akiwemo mtoaji wa figo, mpokeaji na aliewakutanisha, wamekamatwa kwa sasa.
Polisi walianza kufanya uchunguzi wa hospitali baada ya wahudumu wake kuwafahamisha kuhusu visa walivyovishuku vya upasuaji wa figo.
Ni wanafamilia pekee wanaoweza kujitolea kutoa viungo vya mwili kwa wagonjwa nchini India, na biashara yoyote ile ya viungo ni kinyume cha sheria.
Hata hivyo uhaba wa viungo vinavyoweza kuhamishwa kutoka kwa mtu mmoja kuelekea mwingine unachochea kushamiri mauzo ya siri ya viungo vya mwili kote nchini India.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

MAPENZI: Kuna faida na ni muhimu Mpenzi wako kuwa rafiki yako pia

Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi.  Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria.  Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao.  Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...

Urusi: Vikwazo dhidi ya Korea Kaskazini havitafua dafu

MTEULE THE BEST Image caption Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Sergei Lavrov na mwenzeka wa Marekani Rex Tillerson Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Segei Lavrov amemwambia waziri wa ulinzi nchini Marekani Rex Tillerson kwamba kuiwekea vikwazo zaidi Korea Kaskazini hakutafua dafu. Taarifa iliochapishwa na wizara ya kigeni nchini Urusi inasema kuwa wawili hao walizungumza kwa njia ya simu na kushutumu majaribio ya makombora ya hivi karibuni yaliotekelezwa na Pyongyang . Lakini inasema kuwa bwana Lavrov alisisitiza kwamba diplomasia ndio njia ya pekee ya kumaliza wasiwasi katika rasi ya Korea, na kutaka hatua zozote dhidi ya taifa hilo kusitishwa akionya huenda zikasababisha madhara yasiojulikana. Waziri wa ulinzi nchini Marekani amesisitiza kuwa bado kuna fursa ya kidiplomasia katika kukabiliana na Korea Kaskazini. Mapema rais Trump alichapisha ujumbe katika akaunti yake ya Twitter akisema mazungumzo sio suluhisho.

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania Miaka 60 siku kama ya leo ugunduzi mkubwa ulifanyika katika eneo la Olduvai Gorge, kwenye kreta ya Ngorongoro. Wanaakiolojia Louis na Mary Leakey waligundua fuvu la mtu anayeaminika kuwa ni wa kale zaidi waliyompa jina la Zinjanthropus. Ugunduzi huo uliofanyika saa nne asubuhi Julai 22, 1959 kipindi hicho kwenye eneo la Tanganyika ulikuwa wa vipande zaidi ya 100 ukasaidia katika kutambua asili ya watu wa awali duniani. Kabla ya ugunduzi huo, wanasayansi na wanahistoria walikuwa wakiamini kuwa binadamu wa kale walitokea Uchina baada ya ugunduzi wa mafuvu ya kale baina ya 1923 na 1927 nchini humo ya Homo eractus, ama maarufu kama Peking Man. Mafuvu hayo ya Uchina yalikuwa na umri wa takribani miaka 750,000. Mafuvu ya Olduvai eneo ambalo kwa sasa lipo Tanzania wakati wa ugunduzi wake lilikuwa na umri wa takribani miaka milioni 1.75, na hakuna mabaki ya mtu wa kale zaidi ambayo mpaka sasa yamegundul...