Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Mapambano makali kuwania mji wa Aleppo

MTEULE THE BEST

Wapiganaji wa Jaish al-Fatah katika mapambano mjini Aleppo


Kila upande katika vita vya kuwania mji wa Aleppo, serikali na waasi, umejiimarisha kwa wapiganaji zaidi na silaha, katika kile kinachochukuliwa kuwa mapambano ya mwisho kuudhibiti mji huo muhimu wa Kaskazini mwa Syria.
Wapiganaji wa Jaish al-Fatah katika mapambano mjini Aleppo
Mkuu wa Shirika la Kuchunguza Haki za Binadamu nchini Syria lenye makao nchini Uingereza, Rami Abdel Rahman amesema wapiganaji wapya wapatao 2000, wakiwemo wasyria, wairaq, Wairan na wanamgambo wa Hezbollah kutoka Lebanon wameingia mjini Aleppo jana usiku, kushiriki katika mapambano yanayozidi kupamba moto mjini humo.
Aidha, gazeti la al-Watan linaloegemea upande wa serikali ya Syria limeandika leo kuwa jeshi na washirika wake wamepata msaada wa kutosha kukomboa maeneo lililoyaachia. Gazeti hilo limesema kundi la wanamgambo wa kipalestina lenye mafungamano na serikali ya mjini Damascus limepeleka msaada mkubwa kusaidia wanajeshi wanaokilinda kiwanda cha seruji Kusini mwa Aleppo.
Al-Watan limevinukuu vyanzo kutoka uwanja wa vita, ambavyo vimesema kuwa ndege za kivita zimefanya mfululizo wa mashambulizi dhidi ya ngome za waasi.
Kila upande wajizatiti
Waasi wa Syria wanasema wako chini ya shinikizo kubwa la mashambulizi ya anga
Waasi wa Syria wanasema wako chini ya shinikizo kubwa la mashambulizi ya anga
Vikosi vitiifu kwa rais wa Syria Bashar al-Assad vinasonga mbele kukabiliana na muungano wa wapiganaji wa kijihadi, ambao Jumamosi waliyakamata maeneo yanayozunguka chuo cha kijeshi cha Aleppo, na kuuvunja mzingiro wa serikali kwenye wilaya za Mashariki wanakoishi watu takribani 250,000.
Abdel Rahman wa shirika la kuchunguza haki za binadamu nchini Syria, amesema pia kuwa mamia ya wapiganaji waasi kutoka kundi la Fateh al Sham, ambao zamani walikuwa tawi la mtandao wa al-Qaida, wamewasili mjini Aleppo wakitokea sehemu nyingine za mkoa na pia kutoka mkoa wa Idlib.
Fateh al-Sham ambayo siku za nyuma ilijulikana kama al-Nusra Front kabla ya kujitenga na al-Qaida, inaongoza Jeish al-Fateh, au Jeshi la Ushindi linachangia pakubwa katika vita mjini Aleppo.
Aleppo, Mji uliogawika
Mji wa Aleppo ambao kabla ya kuanza kwa vita vya wenyewe kwa wenyewe ulikuwa ndi wenye idadi kubwa zaidi ya wakazi nchini Syria hivi sasa umetengwa katika sehemu mbili, moja ikiwa chini ya udhibiti wa serikali, nyingine ikiwa imechukuliwa na waasi.
Mji wa Aleppo umetengwa katika sehemu mbili; ile iliyo chini ya serikali, na ile inayodhibitiwa na waasi
Mji wa Aleppo umetengwa katika sehemu mbili; ile iliyo chini ya serikali, na ile inayodhibitiwa na waasi
Rais Bashar al-Assad amepania kuukomboa kabisa mji huo,akisaidiwa na ndege za kijeshi za Urusi na wanamgambo wa Hezbollah kutoka Lebanon.
Hatua ya waasi kuyakamata maeneo zaidi ya mji huo inaweza kubadilisha urari wa nguvu za kijeshi, baada ya mafanikio ya jeshi la serikali mwanzoni mwa mwezi Julai, ambayo yalichukuliwa kama mwanzo wa kuukomboa kabisa mji wa Aleppo.
Kamanda mmoja wa cheo cha juu wa wa kundi la Fateh Halab Abu al-Hasanien, amesema wamejichimbia katika mahandaki kwenye eneo la Ramousah, wakikabiliwa na mashambulizi makali ya anga.
Ikiwa serikali ya Syria itaweza kuukomboa mji wa Aleppo, hilo litakuwa pigo kubwa kwa waasi.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

MAPENZI: Kuna faida na ni muhimu Mpenzi wako kuwa rafiki yako pia

Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi.  Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria.  Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao.  Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...

Urusi: Vikwazo dhidi ya Korea Kaskazini havitafua dafu

MTEULE THE BEST Image caption Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Sergei Lavrov na mwenzeka wa Marekani Rex Tillerson Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Segei Lavrov amemwambia waziri wa ulinzi nchini Marekani Rex Tillerson kwamba kuiwekea vikwazo zaidi Korea Kaskazini hakutafua dafu. Taarifa iliochapishwa na wizara ya kigeni nchini Urusi inasema kuwa wawili hao walizungumza kwa njia ya simu na kushutumu majaribio ya makombora ya hivi karibuni yaliotekelezwa na Pyongyang . Lakini inasema kuwa bwana Lavrov alisisitiza kwamba diplomasia ndio njia ya pekee ya kumaliza wasiwasi katika rasi ya Korea, na kutaka hatua zozote dhidi ya taifa hilo kusitishwa akionya huenda zikasababisha madhara yasiojulikana. Waziri wa ulinzi nchini Marekani amesisitiza kuwa bado kuna fursa ya kidiplomasia katika kukabiliana na Korea Kaskazini. Mapema rais Trump alichapisha ujumbe katika akaunti yake ya Twitter akisema mazungumzo sio suluhisho.

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania Miaka 60 siku kama ya leo ugunduzi mkubwa ulifanyika katika eneo la Olduvai Gorge, kwenye kreta ya Ngorongoro. Wanaakiolojia Louis na Mary Leakey waligundua fuvu la mtu anayeaminika kuwa ni wa kale zaidi waliyompa jina la Zinjanthropus. Ugunduzi huo uliofanyika saa nne asubuhi Julai 22, 1959 kipindi hicho kwenye eneo la Tanganyika ulikuwa wa vipande zaidi ya 100 ukasaidia katika kutambua asili ya watu wa awali duniani. Kabla ya ugunduzi huo, wanasayansi na wanahistoria walikuwa wakiamini kuwa binadamu wa kale walitokea Uchina baada ya ugunduzi wa mafuvu ya kale baina ya 1923 na 1927 nchini humo ya Homo eractus, ama maarufu kama Peking Man. Mafuvu hayo ya Uchina yalikuwa na umri wa takribani miaka 750,000. Mafuvu ya Olduvai eneo ambalo kwa sasa lipo Tanzania wakati wa ugunduzi wake lilikuwa na umri wa takribani miaka milioni 1.75, na hakuna mabaki ya mtu wa kale zaidi ambayo mpaka sasa yamegundul...