Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Berlin: maelfu waunga mkono na kupinga maandamano ya AfD


Wafuasi 5,000 wa  chama mbadala kwa Ujerumani (AfD) wameandamana mjini Berlin Jumapili, lakini idadi hiyo ilikuwa ndogo ikilinganishwa na walioandama kuipinga AfD.
Maelfu ya watu wameandamana Jumapili katika mji mkuu wa Ujerumani Berlin. Ni maandamano yanayohusisha pande mbili tofauti. Upande wa wafuasi wa chama cha siasa kali za mrengo wa kulia kinachojiita chama mbadala kwa Ujerumani AfD, kinachopinga uhamiaji pamoja na Uislamu. Na waandamanaji wanaoipinga AfD wakitumia kauli mbiu ya "Wacha chuki.”
Maafisa zaidi wa polisi walishika doria kutenganisha pande hizo mbili za waandamanaji ili kuepusha vurugu.
Katika ukurasa wao wa Twitter, idara ya polisi imesema wametumia kemikali ya pilipili ya kutoa machozi kuwazuia waandamanaji wasivunje mpaka uliowekwa kuwatenganisha.
Beatrix von Storch, mwanachama muhimu wa AfD, amewaambia wafuasi wapatao 2,000 waliokusanyika katika maandamano hayo kwamba mchezaji soka wa timu ya taifa ya Ujerumani Mesut Ozil licha ya kuwa na uraia wa Ujerumani sio Mjerumani. Mchezaji soka huyo, mwenye asili ya Kituruki, amekosolewa vikali hivi karibuni kwa kukutana na Rais wa Uturuki Recep Tayyip Erdogan.


AfD inaipinga serikali ya Kansela Angela Merkel kwa kuruhusu idadi kubwa ya wahamiaji na wakimbizi kuingia Ujerumani. Kama ilivyo katika maandamano ya nyuma ya AfD ya kupinga Uislam nchini Ujerumani, kulikuwapo na watu waliokuwa wakipiga mayowe "Merkel lazima aondoke," wakimaanisha kansela wa Ujerumani Angela Merkel.
Maandamano hayo ya AfD ni ya kwanza kuonesha umma nguvu yao tangu ilipoingia bungeni kwa mara ya kwanza na kuwa chama kikuu cha upinzani.
Maandamano dhidi ya AfD, Berlin
AfD: baadhi ya wafuasi waogopa kujitokeza
Wanaotarajiwa kuhutubia katika maandamanohayo ni viongozi wa ngazi ya juu wa chama hicho, ikiwa ni pamojana Joerg Meuthen and Alexander Gauland.
Viongozi hao wana kawaida ya kupinga uamuzi wa Kansela Merkel wa kuruhusu idadi kubwa ya wahamiaji kuingia nchini Ujerumani wengi wao wakiwa Waislam, wakati wa kilele wa mgogoro wa wahamiaji barani Ulaya mwaka 2015.
"Merkel amesababisha taharuki kubwa," amesema mwanachama wa AfD, Christine Moessl mwenye umri wa miaka 41. "Na sasa tunajua kwamba Waislam wengi wenye misimamo mikali walikuwa miongoni mwa wakimbizi, na hawaheshimu wanawake. Tunahitaji kujihisi tuko salama," ameongeza Moessl.
Baada ya awali kutabiri wafuasi 10,000 wa AfD watajitokeza, waandaaji baadaye walisema watafurahi hata wakijitokeza 5,000.
Mkuu wa AfD mjini Berlin, Georg Pazderski alisema kabla ya maandamano kwamba wengi bado wanaogopa kujidhihirisha kuwa ni wafuasi wa AfD. Hata baada ya chama hicho kuchukua asilimia 13 ya kura, na kushinda viti vyao vya kwanza katika bunge la kitaifa wakati wa uchaguzi wa mwaka jana.
Lakini pia kulikuwa na watu wapatao 20,000 walioandamana kuyapinga maandamano hayo ya AfD - kulingana na makadirio ya polisi - wengi wao wakiwa vijana, jambo linaloashiria mgawanyiko unaoshuhudiwa nchini Ujerumani tokea mgogoro wa wahamiaji wa mwaka 2015.
Maandamano hayo ya Jumapili yalikuwa ni ya amani. Mtu mmoja tu ameripotiwa kupata jeraha dogo, huku kukiwa na ulinzi mkali wa polisi

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

MAPENZI: Kuna faida na ni muhimu Mpenzi wako kuwa rafiki yako pia

Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi.  Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria.  Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao.  Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...

Urusi: Vikwazo dhidi ya Korea Kaskazini havitafua dafu

MTEULE THE BEST Image caption Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Sergei Lavrov na mwenzeka wa Marekani Rex Tillerson Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Segei Lavrov amemwambia waziri wa ulinzi nchini Marekani Rex Tillerson kwamba kuiwekea vikwazo zaidi Korea Kaskazini hakutafua dafu. Taarifa iliochapishwa na wizara ya kigeni nchini Urusi inasema kuwa wawili hao walizungumza kwa njia ya simu na kushutumu majaribio ya makombora ya hivi karibuni yaliotekelezwa na Pyongyang . Lakini inasema kuwa bwana Lavrov alisisitiza kwamba diplomasia ndio njia ya pekee ya kumaliza wasiwasi katika rasi ya Korea, na kutaka hatua zozote dhidi ya taifa hilo kusitishwa akionya huenda zikasababisha madhara yasiojulikana. Waziri wa ulinzi nchini Marekani amesisitiza kuwa bado kuna fursa ya kidiplomasia katika kukabiliana na Korea Kaskazini. Mapema rais Trump alichapisha ujumbe katika akaunti yake ya Twitter akisema mazungumzo sio suluhisho.

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania Miaka 60 siku kama ya leo ugunduzi mkubwa ulifanyika katika eneo la Olduvai Gorge, kwenye kreta ya Ngorongoro. Wanaakiolojia Louis na Mary Leakey waligundua fuvu la mtu anayeaminika kuwa ni wa kale zaidi waliyompa jina la Zinjanthropus. Ugunduzi huo uliofanyika saa nne asubuhi Julai 22, 1959 kipindi hicho kwenye eneo la Tanganyika ulikuwa wa vipande zaidi ya 100 ukasaidia katika kutambua asili ya watu wa awali duniani. Kabla ya ugunduzi huo, wanasayansi na wanahistoria walikuwa wakiamini kuwa binadamu wa kale walitokea Uchina baada ya ugunduzi wa mafuvu ya kale baina ya 1923 na 1927 nchini humo ya Homo eractus, ama maarufu kama Peking Man. Mafuvu hayo ya Uchina yalikuwa na umri wa takribani miaka 750,000. Mafuvu ya Olduvai eneo ambalo kwa sasa lipo Tanzania wakati wa ugunduzi wake lilikuwa na umri wa takribani miaka milioni 1.75, na hakuna mabaki ya mtu wa kale zaidi ambayo mpaka sasa yamegundul...