Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Tetesi za soka Ulaya 01.06.2018


Kocha wa Real Madrid anayeondoka Zinedine Zidane na Mshambuliaji Gareth Bale

Chelsea itajaribu kumshawishi Zidane kuwa mkufunzi wake mpya . (sun)


Matumaini ya klabu ya Manchester United ya kumsajili Gareth Bale, 28, huenda yakafifia huku mchezaji huyo wa taifa la Wales akitarajiwa kusalia kufuatia kuondoka kwa Zidane. (Daily Mirror)



Kocha wa Tottenham Mauricio Pochettino

Real Madrid huenda ikamnyatia mkufunzi wa Tottenham Mauricio Pochettino - ambaye alitia saini mkataba mpya wa miaka mitano na timu yake wiki iliopita- ili kuchukua mahala pake Zinedine Zidane aliyeondoka. (Daily Mirror)


Lakini Real pia inamtaka kocha wa Liverpool Jurgen Klopp, amaye aliiongoza The Reds kufika fainali ya kombe la vilabu bingwa Ulaya. (Sun)



Kandarasi ya Pochettino katika klabu ya Spurs haina kipengee ambacho kinaweza kumruhusu kuondoka na mwenyekiti wake Daniel Levy yuko tayari kuhakikisha kuwa anasalia katika klabu hiyo.(Daily Telegraph)



Napoli Maurizio Sarri

The Blues pia huenda wakamlenga mkufunzi wa Ufaransa na Paris St-Germain Laurent Blanc kuchukua mahala pake Antonio Conte. (Daily Mail)


Chelsea inasema kuwa haitalipa dau la Ā£7m ili kununua kandarasi ya mkufunzi wa Napoli Maurizio Sarri. (Guardian)



Mmiliki wa Chelsea Roman Abramovich

Mmiliki wa Chelsea Roman Abramovich angependelea kulipwa kitita cha Ā£1.17bn iwapo ataamua kuiuza Chelsea (Times)


Chelsea imesitisha mazungumzo ya kandarasi mpya na kipa wake Thibaut Courtois na huenda wakamuuza raia huo wa Ubelgiji mwenye umri wa miaka 26. The Blues inalenga kumsajili kipa wa Roma na Brazil Alisson, 25. (Sky Sports)


Juventus imeiuliza Chelsea iwapo inamhitaji mshambuliaji wa Argentina Gonzalo Higuain, 30, ikiwa ni katika mipango ya kumsajili tena mshambuliaji wa Uhispania Alvaro Morata, 25. (London Evening Standard)


Kocha mpya wa Arsenal Unai Emery anataka kumnunua kiungo wa kati kinda Yacine Adli 17 kutoka Paris St-Germain.



Unai Emery

Mchezaji huyo anayeichezea timu ya taifa ya Ufaransa ya wachezaji wasiozidi umri wa miaka 18 pia amevutia timu kama vile Bayern Munich, Barcelona na Real Madrid. (London Evening Standard)


Newcastle imehusishwa na beki wa klabu ya Sassuolo 26 Gian Marco Ferrari, ambaye alihudumu msimu uliopita kwa mkopo katika klabu ya Sampdoria. (Newcastle Chronicle)



Kipa wa zamani wa Manchester United Peter Schmeichel, 54, anakaribia kujiunga na klabu ya Sporting kama mkufunzi wa kipa. (Correio da Manha, via Sport Witness)

Kipa wa zamani wa Manchester United Peter Schmeichel, 54, anakaribia kujiunga na klabu ya Sporting kama mkufunzi wa kipa. (Correio da Manha, via Sport Witness)


Aliyekuwa mkufunzi wa klabu ya Spurs Harry Redknapp anaamini kwamba mpwa wake , Frank Lampard, anafaa kumsajili nahodha wa zamani wa Chelsea Jhn Terry, 37, katika klabu ya Derby. (Talksport)



Harry Redknapp

Manchester United inatafuta kumsajili afisa wa kusaka wachezaji nchini Ufaransa huku Klabu hiyo ikiendelea kuimarisha mtandao wake wa utafutaji wa wachezaji wenye vipawa . (Manchester Evening News)


Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

MAPENZI: Kuna faida na ni muhimu Mpenzi wako kuwa rafiki yako pia

Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi.  Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria.  Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao.  Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...

Urusi: Vikwazo dhidi ya Korea Kaskazini havitafua dafu

MTEULE THE BEST Image caption Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Sergei Lavrov na mwenzeka wa Marekani Rex Tillerson Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Segei Lavrov amemwambia waziri wa ulinzi nchini Marekani Rex Tillerson kwamba kuiwekea vikwazo zaidi Korea Kaskazini hakutafua dafu. Taarifa iliochapishwa na wizara ya kigeni nchini Urusi inasema kuwa wawili hao walizungumza kwa njia ya simu na kushutumu majaribio ya makombora ya hivi karibuni yaliotekelezwa na Pyongyang . Lakini inasema kuwa bwana Lavrov alisisitiza kwamba diplomasia ndio njia ya pekee ya kumaliza wasiwasi katika rasi ya Korea, na kutaka hatua zozote dhidi ya taifa hilo kusitishwa akionya huenda zikasababisha madhara yasiojulikana. Waziri wa ulinzi nchini Marekani amesisitiza kuwa bado kuna fursa ya kidiplomasia katika kukabiliana na Korea Kaskazini. Mapema rais Trump alichapisha ujumbe katika akaunti yake ya Twitter akisema mazungumzo sio suluhisho.

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania Miaka 60 siku kama ya leo ugunduzi mkubwa ulifanyika katika eneo la Olduvai Gorge, kwenye kreta ya Ngorongoro. Wanaakiolojia Louis na Mary Leakey waligundua fuvu la mtu anayeaminika kuwa ni wa kale zaidi waliyompa jina la Zinjanthropus. Ugunduzi huo uliofanyika saa nne asubuhi Julai 22, 1959 kipindi hicho kwenye eneo la Tanganyika ulikuwa wa vipande zaidi ya 100 ukasaidia katika kutambua asili ya watu wa awali duniani. Kabla ya ugunduzi huo, wanasayansi na wanahistoria walikuwa wakiamini kuwa binadamu wa kale walitokea Uchina baada ya ugunduzi wa mafuvu ya kale baina ya 1923 na 1927 nchini humo ya Homo eractus, ama maarufu kama Peking Man. Mafuvu hayo ya Uchina yalikuwa na umri wa takribani miaka 750,000. Mafuvu ya Olduvai eneo ambalo kwa sasa lipo Tanzania wakati wa ugunduzi wake lilikuwa na umri wa takribani miaka milioni 1.75, na hakuna mabaki ya mtu wa kale zaidi ambayo mpaka sasa yamegundul...