Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Mkuu wa NYS akamatwa Kenya kuhusiana na ufisadi


Maafisa nchini Kenya wamemkamata mkuu wa shirika la huduma kwa vijana NYS kama sehemu ya uchunguzi kuhusu kuibiwa kwa takriban dola milioni 100 katika shirika hilo.


Vyombo vya habari vya Kenya vimeripoti kuwa mkurugenzi mkuu wa shirika hilo la huduma kwa vijana NYS Richard Ndubai amekamatwa mapema leo pamoja na maafisa wengine wakiwemo mahasibu na maafisa wanaosimamia ununuzi wa vifaa NYS pamoja na wafanyabiashara waliohusika katika kandarasi na zabuni kadhaa.


Mkuu wa idara ya upelelezi amesema watu 17 wamekamatwa ili kuhojiwa kuhusiana na kashfa hiyo ya ufisadi inayoikumba NYS.


Mwendesha mkuu wa mashitaka pia amesema mashitaka dhidi ya washukiwa waliotajwa katika kashfa hiyo yataanza mara moja. Hata hivyo majina ya washukiwa hayajatolewa hadharani.


Mabilioni yapotea NYS


Vituo vya televisheni vya K24 na Citizen vimeripoti kuwa katibu wa kudumu wa wizara ya utumishi kwa umma, vijana na jinsia Lilian Mbogo Omollo amejisalilisha kwa polisi akiwa ameandamana na mawakili wake.




Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta


Vyombo vya habari nchini Kenya katika kipindi cha majuma kadhaa sasa vimekuwa vikiripoti kuwa shilingi bilioni 10 ambazo ni sawa na dola takriban milioni 100 zimeibiwa kwa njia za kilaghai kupitia malipo ya zabuni ghushi katika shirika la huduma kwa vijana.


Shirika la Habari la Reuters halikuweza kuzungumza na Ndubai ambaye anazuiwa na polisi na pia haikuweza kuwasiliana na wakili wake.


Licha ya ahadi za mara kwa mara alizozitoa Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta alipochaguliwa kwa mara ya kwanza kuliongoza taifa hilo mnamo mwaka 2013 za kupambana vilivyo na ufisadi, wakosoaji wake wanamshutumu kwa kujikokota katika kuwachukulia hatua za kisheria maafisa wa ngazi ya juu serikalini wanaotuhumiwa kuhusika na ufisaidi.


Wachambuzi wanasema kushitakiwa na kufungwa kwa maafisa wakuu ndiyo njia pekee ya kukomesha jinamizi la ufisadi nchini humo.


Ufisadi wawaghadhabisha Wakenya


Ripoti hizo za kuibiwa kiasi kikubwa cha fedha katika shirika hilo la NYS, ambapo si mara ya kwanza mabilioni ya fedha kupotea katika shirika hilo, kumewaghadhabisha na kuwavunja moyo Wakenya wengi hasa ikizingatiwa kuwa mwaka 2015 NYS ilikumbwa na kashfa kama hii ya sasa, na hakuna hatua madhubiti zilichukuliwa dhidi ya watuhumiwa. Mwanaharakati Boniface Mwangi ameitisha maandamano siku ya Alhamisi wiki hii kupinga kukithiri kwa ufisadi.


Mwanaharakati Boniface Mwangi


Jambo jingine linalowakera Wakenya ni kuwa wizi huo unatokea katika shirika linalopaswa kuwapa uwezo vijana kuwa na maarifa na kuwasaidia kupata ajira. Wiki iliyopita, wachunguzi waliwaita watu zaidi ya 40 katika idara ya upelelezi kuwahoji kuhusiana na kupotea kwa fedha hizo za NYS.


Ofisi ya mwendesha mashitaka imesema ina msingi wa kuanzisha hatua za kisheria dhidi ya washukiwa.


Rais Kenyatta amezilaumu asasi zilizotwishwa majukumu ya kupambana na ufisadi kwa kujivuta katika kupambana na ufisadi. Mwaka 2016, mkuu wa tume ya kupambana na ufisadi alisema Kenya inapoteza thuluthi moja ya bajeti yake kwa ufisadi. Hiyo inamaanisha kiasi cha takriban dola bilioni 6 hupotea kutokana na ufisaidi.


Licha ya wizara ya fedha kukanusha kuwa Kenya inapoteza kiasi kikubwa kama hicho cha fedha, Rais Kenyatta alikiri kuwa ufisadi umefikia viwango ambavyo vinatishia usalama wa kitaifa


Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

MAPENZI: Kuna faida na ni muhimu Mpenzi wako kuwa rafiki yako pia

Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi.  Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria.  Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao.  Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...

Urusi: Vikwazo dhidi ya Korea Kaskazini havitafua dafu

MTEULE THE BEST Image caption Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Sergei Lavrov na mwenzeka wa Marekani Rex Tillerson Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Segei Lavrov amemwambia waziri wa ulinzi nchini Marekani Rex Tillerson kwamba kuiwekea vikwazo zaidi Korea Kaskazini hakutafua dafu. Taarifa iliochapishwa na wizara ya kigeni nchini Urusi inasema kuwa wawili hao walizungumza kwa njia ya simu na kushutumu majaribio ya makombora ya hivi karibuni yaliotekelezwa na Pyongyang . Lakini inasema kuwa bwana Lavrov alisisitiza kwamba diplomasia ndio njia ya pekee ya kumaliza wasiwasi katika rasi ya Korea, na kutaka hatua zozote dhidi ya taifa hilo kusitishwa akionya huenda zikasababisha madhara yasiojulikana. Waziri wa ulinzi nchini Marekani amesisitiza kuwa bado kuna fursa ya kidiplomasia katika kukabiliana na Korea Kaskazini. Mapema rais Trump alichapisha ujumbe katika akaunti yake ya Twitter akisema mazungumzo sio suluhisho.

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania Miaka 60 siku kama ya leo ugunduzi mkubwa ulifanyika katika eneo la Olduvai Gorge, kwenye kreta ya Ngorongoro. Wanaakiolojia Louis na Mary Leakey waligundua fuvu la mtu anayeaminika kuwa ni wa kale zaidi waliyompa jina la Zinjanthropus. Ugunduzi huo uliofanyika saa nne asubuhi Julai 22, 1959 kipindi hicho kwenye eneo la Tanganyika ulikuwa wa vipande zaidi ya 100 ukasaidia katika kutambua asili ya watu wa awali duniani. Kabla ya ugunduzi huo, wanasayansi na wanahistoria walikuwa wakiamini kuwa binadamu wa kale walitokea Uchina baada ya ugunduzi wa mafuvu ya kale baina ya 1923 na 1927 nchini humo ya Homo eractus, ama maarufu kama Peking Man. Mafuvu hayo ya Uchina yalikuwa na umri wa takribani miaka 750,000. Mafuvu ya Olduvai eneo ambalo kwa sasa lipo Tanzania wakati wa ugunduzi wake lilikuwa na umri wa takribani miaka milioni 1.75, na hakuna mabaki ya mtu wa kale zaidi ambayo mpaka sasa yamegundul...