Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Kinana amkabidhi Bashiru kijiti CCM

Enzi mpya imeanza katika chama tawala nchini Tanzania CCM baada ya msomi wa chuo kikuu cha Dar es Salaam, Dk Bashiru Ally kukabidhiwa ofisi na mtangulizi wake Abdulrahman Kinana siku ya Alhamis(31.05.2018).


Msomi  huyo aliyesifika kutokana na uchambuzi wa masuala ya siasa na kupenda kushiriki mijadala ya majukwaani sasa ameingia kwenye ulingo halisi wa kisiasa na anatazamiwa kuanza kukabiliana na hoja kutoka upinzani ambao wakati fulani alikaa nao meza moja kupigania yale yanayoonekana kuwa ni masuala ya pamoja ya kitaifa.


Ujio wake ndani ya CCM tayari umezusha mjadala wa hoja hasa kutokana na misimamo yake aliyokuwa akiionyesha wakati alipokuwa akishiriki kwenye mijadala ya wazi ikiwamo ile iliyohusu hali ya kisiasa nchini na umuhimu wa kuwa na katiba mpya.


Katibu mkuu mpya wa CCM Dr. Bashiru Ally aliyekuwa mhadhiri UDSM


Katika moja ya mijadala hiyo, msomi huyo ambaye anatajwa kuwa ni mtu mwenye kuegemea falsafa za kijamaa na uzalendo, aligusia kwa kina kuhusu haja ya Tanzania kuwa na katiba mpya.


Akijadili kwenye mjadala huo, alisema ili siasa ya Tanzania istawi vyema lazima kupatikane katiba mpya akisema katiba iliyopo siyo muafaka kwa Tanzania ya sasa yenye kufuata mfumo wa vyama vingi.



Hata hivyo, msomi huyo ameanza kuchanga upya karata zake akifuata nyayo za wasomi waliomtangulia ambao kwa nyakati tofauti waliachana na ufundishaji katika vyuo vikuu na kujiunga  serikalini  ama katika taasisi nyingine za kiutendaji.


Huku akitetea nafasi yake ya awali ya uchambuzi, Dk Bashiru amejibu hoja ya waandishi wa habari waliotaka kujua kama ataendelea na msimamo huo au la akisema kuwa, "kazi niliyopewa si ya jukwaa au siasa za majukwaani, siasa za majukwaani ni mwenyekiti wa chama. Na ni marufuku kwa mtendaji kufanya kazi ya mwanasiasa."


Kwaherini. Abdurahman Kinana akiwaaga wana CCM


Kuteuliwa kwake ndani ya CCM kumekuja siku chache baada ya kuongoza kamati iliyoundwa na mwenyekiti Rais John Magufuli iliyokuwa ikichunguza mali ya chama na kisha kuwasilisha ripoti yake ambayo iliwatuhumu baadhi ya vigogo wa chama hicho kuhusika katika kuhujumu mali hizo.


Ama, Dk Bashiru aliyekuwa mkufunzi wa masuala ya siasa na utawala wa umma katika chuo kikuu cha Dar es Salaam sasa anaingia katika orodha ya wasomi wengi ikiwamo maprofesa waliochana na taalamu zao na kuchukua majukumu serikalini.


Baadhi ya wachambuzi wa mambo wanaonyesha wasiwasi kuhusu kuendelea kupukutika kwa wasomi wa ngazi za juu wanaobadili taaluma zao baada ya kukabidhiwa majukumu mengine serikalini.


Moja ya kizingiti ambacho kitakuwa ni mtihani wake wa kwanza ni namna atakavyofanikiwa kushughulikia ubadhirifu alioubaini wakati alipokuwa katika kamati ya kutathmini mali za chama.


Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

MAPENZI: Kuna faida na ni muhimu Mpenzi wako kuwa rafiki yako pia

Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi.  Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria.  Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao.  Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...

Urusi: Vikwazo dhidi ya Korea Kaskazini havitafua dafu

MTEULE THE BEST Image caption Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Sergei Lavrov na mwenzeka wa Marekani Rex Tillerson Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Segei Lavrov amemwambia waziri wa ulinzi nchini Marekani Rex Tillerson kwamba kuiwekea vikwazo zaidi Korea Kaskazini hakutafua dafu. Taarifa iliochapishwa na wizara ya kigeni nchini Urusi inasema kuwa wawili hao walizungumza kwa njia ya simu na kushutumu majaribio ya makombora ya hivi karibuni yaliotekelezwa na Pyongyang . Lakini inasema kuwa bwana Lavrov alisisitiza kwamba diplomasia ndio njia ya pekee ya kumaliza wasiwasi katika rasi ya Korea, na kutaka hatua zozote dhidi ya taifa hilo kusitishwa akionya huenda zikasababisha madhara yasiojulikana. Waziri wa ulinzi nchini Marekani amesisitiza kuwa bado kuna fursa ya kidiplomasia katika kukabiliana na Korea Kaskazini. Mapema rais Trump alichapisha ujumbe katika akaunti yake ya Twitter akisema mazungumzo sio suluhisho.

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania Miaka 60 siku kama ya leo ugunduzi mkubwa ulifanyika katika eneo la Olduvai Gorge, kwenye kreta ya Ngorongoro. Wanaakiolojia Louis na Mary Leakey waligundua fuvu la mtu anayeaminika kuwa ni wa kale zaidi waliyompa jina la Zinjanthropus. Ugunduzi huo uliofanyika saa nne asubuhi Julai 22, 1959 kipindi hicho kwenye eneo la Tanganyika ulikuwa wa vipande zaidi ya 100 ukasaidia katika kutambua asili ya watu wa awali duniani. Kabla ya ugunduzi huo, wanasayansi na wanahistoria walikuwa wakiamini kuwa binadamu wa kale walitokea Uchina baada ya ugunduzi wa mafuvu ya kale baina ya 1923 na 1927 nchini humo ya Homo eractus, ama maarufu kama Peking Man. Mafuvu hayo ya Uchina yalikuwa na umri wa takribani miaka 750,000. Mafuvu ya Olduvai eneo ambalo kwa sasa lipo Tanzania wakati wa ugunduzi wake lilikuwa na umri wa takribani miaka milioni 1.75, na hakuna mabaki ya mtu wa kale zaidi ambayo mpaka sasa yamegundul...