Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Auawa akichuma kuvu yenye 'nguvu za kiume'

MTEULE THE BEST

 

 

 

Mtu mmoja amepigwa risasi na kuuawa katika kijiji cha Nepal alipokuwa akichuma kuvu fulani inayotambuliwa kwa uwezo wake wa kuongeza nguvu za kiume.
Kuvu hiyo inayotambulika kama ''Himalayan Viagra'' inasemekana kuwaongezea ashki walaji wake.
Kuvu hiyo ni kitega uchumi cha wenye vijiji wa maeneo ya milimani.
Haijulikani kwanini genge hilo la wavamizi liliwashambulia watu hao waliokuwa wakichuma kuvu hiyo katika wilaya ya mugu ila maafisa wa utawala wamethibitisha kuwa watu wengine watatu walijeruhiwa katika shambulizi hilo.
Ukungu au kuvu hiyo humea kwenye mwili wa nondo au mtoto wa kipepeo na kilo moja ya kuvu hiyo inaweza kuuza kwa maelfu ya dola za Marekani nchini Uchina.

 
Auawa akichuma kuvu yenye 'nguvu za kiume'
Biashara hiyo ni mojawapo ya njia ambazo raia wengi masikini wa jamii zinazoishi katika maeneo ya milima ya Hilamaya hujipatia riziki.
Kila mwaka maelfu ya watu kutoka vijijini hufunga safari kwa kutumia nyumbu na ngombe hadi maeneo ya milimani kutafuta ukungu huo unaomea kwenye mwili wa nondo.
Wakati wa msimu wa mavuna, shule hata hufungwa ili wanafunzi wawasaidie wazazi wao kutafuta kuvu.
Hii sio mara ya kwanza kwa ghasia kutokea katika eneo hilo.
Mwaka wa 2009 watu saba waliuawa baada ya mzozo kutokea kuhusu hati miliki ya kutafuta ukungu huo katika maeneo ya milima.
Licha ya utajiri unaotokana na mauzo ya ukungu, raia wengi nchini humo wanaiona kuwepo kwake kama laana kubwa kwa jamii.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

MAPENZI: Kuna faida na ni muhimu Mpenzi wako kuwa rafiki yako pia

Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi.  Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria.  Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao.  Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...

Urusi: Vikwazo dhidi ya Korea Kaskazini havitafua dafu

MTEULE THE BEST Image caption Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Sergei Lavrov na mwenzeka wa Marekani Rex Tillerson Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Segei Lavrov amemwambia waziri wa ulinzi nchini Marekani Rex Tillerson kwamba kuiwekea vikwazo zaidi Korea Kaskazini hakutafua dafu. Taarifa iliochapishwa na wizara ya kigeni nchini Urusi inasema kuwa wawili hao walizungumza kwa njia ya simu na kushutumu majaribio ya makombora ya hivi karibuni yaliotekelezwa na Pyongyang . Lakini inasema kuwa bwana Lavrov alisisitiza kwamba diplomasia ndio njia ya pekee ya kumaliza wasiwasi katika rasi ya Korea, na kutaka hatua zozote dhidi ya taifa hilo kusitishwa akionya huenda zikasababisha madhara yasiojulikana. Waziri wa ulinzi nchini Marekani amesisitiza kuwa bado kuna fursa ya kidiplomasia katika kukabiliana na Korea Kaskazini. Mapema rais Trump alichapisha ujumbe katika akaunti yake ya Twitter akisema mazungumzo sio suluhisho.

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania Miaka 60 siku kama ya leo ugunduzi mkubwa ulifanyika katika eneo la Olduvai Gorge, kwenye kreta ya Ngorongoro. Wanaakiolojia Louis na Mary Leakey waligundua fuvu la mtu anayeaminika kuwa ni wa kale zaidi waliyompa jina la Zinjanthropus. Ugunduzi huo uliofanyika saa nne asubuhi Julai 22, 1959 kipindi hicho kwenye eneo la Tanganyika ulikuwa wa vipande zaidi ya 100 ukasaidia katika kutambua asili ya watu wa awali duniani. Kabla ya ugunduzi huo, wanasayansi na wanahistoria walikuwa wakiamini kuwa binadamu wa kale walitokea Uchina baada ya ugunduzi wa mafuvu ya kale baina ya 1923 na 1927 nchini humo ya Homo eractus, ama maarufu kama Peking Man. Mafuvu hayo ya Uchina yalikuwa na umri wa takribani miaka 750,000. Mafuvu ya Olduvai eneo ambalo kwa sasa lipo Tanzania wakati wa ugunduzi wake lilikuwa na umri wa takribani miaka milioni 1.75, na hakuna mabaki ya mtu wa kale zaidi ambayo mpaka sasa yamegundul...