Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Mateen hakushawishiwa kufanya mauaji Orlando

MTEULE THE BEST

 

Rais wa Marekani, Barack Obama amesema hakuna ushahidi kuwa aliyetekeleza mashambulizi kwenye klabu ya usiku mjini Orlando alikuwa sehemu ya mpango mkubwa wa mashambulizi.

Obama ameeleza shambulio hilo lilisukumwa na msimamo binafsi wa mshambuliaji huyo na hakuna ushahidi kuwa Omar Mateen alipata maelekezo kutoka nje kutekeleza mauaji.
Mkurugenzi wa shirika la kijasusi FBI,James Comey amesema kuna ishara kuwa Mateen alishawishika kupitia mitandao ya intaneti.Lakini amesema haijulikani Mateen alikuwa akiunga mkono kundi gani la kigaidi.
Comey amesema muuaji huyo alieleza kuunga mkono kundi la wanamgambo wa IS na hasimu wa kundi hilo, Al Nusra la nchini Syria.
 


Trump amepinga waislamu kuingia Marekani,jambo ambalo Hillary Clinton haliungi mkono
Mgombea Urais kwa tiketi ya Republican nchini Marekani, Donald Trump amerejea kauli yake akitaka kuwazuia kwa muda waislamu kuingia nchini Marekani.
Katika hotuba yake huko New Hampshire, Trump amesema mfumo wa Idara ya uhamiaji nchini Marekani umeruhusu familia ya Omar Mateen kuingia nchini Marekani huku akidai kuwa wauaji wengine wamendelea kuruhusiwa kuingia nchini humo
''Sababu pekee ya muuaji kuwepo nchini Marekani ni familia yake kuja hapa.huo ndio ukweli, ni ukweli unaopaswa kuzungumziwa.tuna mfumo wa idara ya uhamiaji isiyotekeleza wajibu wake,ambayo haituruhusu kujua ni nani tunaowaruhusu kuingia nchini mwetu na mfumo hauruhusu kuwalinda vyema raia wetu''
Akizungumza jimboni Ohio,Mgombea urais kupitia Chama cha Democratic, Hillary Clinton,amekosoa mpango wa mpinzani wake Donald Trump kuwazuia waislamu kuingia Marekani
''hatua hiyo ya uchochezi ya vitisho kuzuia familia na marafiki wa kiislamu kuingia marekani, pia mamilioni ya wafanya biashara na watalii waislamu kuingia nchini humo inaumiza sehemu kubwa ya waislamu wanaopenda uhuru na kuchukia ugaidi''.
Katika hatua nyingine,Silaha mbili kati ya zilizotumiwa na Mateen zilinunuliwa kwenye kituo cha kuuza silaha.Mmiliki wa duka hilo Edward Henson amesema Mateen alipitia taratibu zote zinazopaswa kupitia wakati wa kununua silaha.

 

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

MAPENZI: Kuna faida na ni muhimu Mpenzi wako kuwa rafiki yako pia

Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi.  Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria.  Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao.  Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...

Urusi: Vikwazo dhidi ya Korea Kaskazini havitafua dafu

MTEULE THE BEST Image caption Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Sergei Lavrov na mwenzeka wa Marekani Rex Tillerson Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Segei Lavrov amemwambia waziri wa ulinzi nchini Marekani Rex Tillerson kwamba kuiwekea vikwazo zaidi Korea Kaskazini hakutafua dafu. Taarifa iliochapishwa na wizara ya kigeni nchini Urusi inasema kuwa wawili hao walizungumza kwa njia ya simu na kushutumu majaribio ya makombora ya hivi karibuni yaliotekelezwa na Pyongyang . Lakini inasema kuwa bwana Lavrov alisisitiza kwamba diplomasia ndio njia ya pekee ya kumaliza wasiwasi katika rasi ya Korea, na kutaka hatua zozote dhidi ya taifa hilo kusitishwa akionya huenda zikasababisha madhara yasiojulikana. Waziri wa ulinzi nchini Marekani amesisitiza kuwa bado kuna fursa ya kidiplomasia katika kukabiliana na Korea Kaskazini. Mapema rais Trump alichapisha ujumbe katika akaunti yake ya Twitter akisema mazungumzo sio suluhisho.

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania Miaka 60 siku kama ya leo ugunduzi mkubwa ulifanyika katika eneo la Olduvai Gorge, kwenye kreta ya Ngorongoro. Wanaakiolojia Louis na Mary Leakey waligundua fuvu la mtu anayeaminika kuwa ni wa kale zaidi waliyompa jina la Zinjanthropus. Ugunduzi huo uliofanyika saa nne asubuhi Julai 22, 1959 kipindi hicho kwenye eneo la Tanganyika ulikuwa wa vipande zaidi ya 100 ukasaidia katika kutambua asili ya watu wa awali duniani. Kabla ya ugunduzi huo, wanasayansi na wanahistoria walikuwa wakiamini kuwa binadamu wa kale walitokea Uchina baada ya ugunduzi wa mafuvu ya kale baina ya 1923 na 1927 nchini humo ya Homo eractus, ama maarufu kama Peking Man. Mafuvu hayo ya Uchina yalikuwa na umri wa takribani miaka 750,000. Mafuvu ya Olduvai eneo ambalo kwa sasa lipo Tanzania wakati wa ugunduzi wake lilikuwa na umri wa takribani miaka milioni 1.75, na hakuna mabaki ya mtu wa kale zaidi ambayo mpaka sasa yamegundul...