MTEULE THE BEST
Muuaji wa Jo Cox ajigamba mahakamani
Thomas Mair, mtu aliyeshtakiwa kwa mauaji ya mbunge wa Uingereza amefikishwa mahakamani Central London.
Alipoambiwa
aseme jina lake, mtu huyo mwenye umri wa miaka hamsini na mbili alisema
nikimnukuu ''jina langu ni kifo kwa wasaliti,uhuru kwa Uingereza''.Mair pia ameshtakiwa kwa kumdhuru vibaya Cox,kupatikana na bunduki na silaha nyingine hatari.
Kifo chake kimesababisha kusitishwa kwa majuma kadhaa kampeini za kura ya maoini juu ya Uingereza kujiondoa katika uanachama wa muungano wa EU
Maoni