Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Austria imerudi katika utawala wa mrengo wa kulia

MTEULE THE BEST

Sebastian Kurz (kulia) and the Freedom Party's Heinz-Christian Strache reached a coalition deal
Sebastian Kurz (kulia) na Heinz-Christian Strache wa Freedom Party
Austria inakuwa nchi pekee ya Uropa magharibi kuwa na chama tawala kilicho na misimamo mikali ya mrengo wa kulia
Rais wa Austria, Alexander Van der Bellen ameidhinisha kuundwa serikali ya muungano kati ya chama cha kihafidhina People's Party na cha mrengo wa kulia Freedom Party.
Austria inaelekea kuwa nchi pekee ya Uropa magharibi kuwa na chama tawala kilicho na misimamo mikali ya mrengo wa kulia.
Hii inatokana na hatua ya kiongozi Sebastian Kurz wa chama cha conservative Austrian People's Party kuridhia ushirikiano na chama kidogo cha mrengo wa kulia Freedom Party kinachoongozwa na Heinz-Christian Strache, ambao wao wanaendeleza sera kali hasa dhidi ya wahamiaji.
Bwana Kurz mwenye ana miaka 31 pekee, na kama mpango huu utafanikiwa atakuwa pia kiongozi wa serikali mwenye umri mdogo zaidi duniani.
Kwa muda wa miezi miwili sasa bunge la nchi hiyo limekuwa likijadili vipi kuzuia uhamiaji nchini humo lakini maswali yanaulizwa - je hilo litaathiri vipi wa-Austria wanaotaka kuhamia mataifa mengine?
Vyama hivyo viliitawala nchi pamoja mwisho kati ya mwaka 2000 na 2005.
Viongozi hao wawili hawana taarifa kuhusu mpango wa serikali, lakini nyadhifa nyingi za uwaziri zinatarajiwa kukabidhiwa chama kidogo cha Freedom Party kama sehemu ya makubaliano.
    Uchaguzi wa October 15 ulishindwa kutoa matokeo ya mwisho.
    Kampeni iligubikwa kwa mzozo wa uhamiaji Ulaya, jambo ambalo chama kinachopinga uhamiaji cha Freedom Party kwa muda mrefu kimekuwa kikifanya kampeni kutumia suala hilo.
    Kurz amewavutia wapiga kura wa kihafidhina na wa mrengo wa kulia kwa ahadi zake za kufunga njia wanaozpitia wahamiaji kuingia Ulaya, kupunguza malipo kwa wakimbizi , na kuwazuia wahamiaji kupokea malipo hadi pale watakapokuwa wamishia Austria kwa zaidi ya miaka mitano

    Maoni

    Machapisho maarufu kutoka blogu hii

    MAPENZI: Kuna faida na ni muhimu Mpenzi wako kuwa rafiki yako pia

    Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi.  Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria.  Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao.  Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...

    Urusi: Vikwazo dhidi ya Korea Kaskazini havitafua dafu

    MTEULE THE BEST Image caption Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Sergei Lavrov na mwenzeka wa Marekani Rex Tillerson Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Segei Lavrov amemwambia waziri wa ulinzi nchini Marekani Rex Tillerson kwamba kuiwekea vikwazo zaidi Korea Kaskazini hakutafua dafu. Taarifa iliochapishwa na wizara ya kigeni nchini Urusi inasema kuwa wawili hao walizungumza kwa njia ya simu na kushutumu majaribio ya makombora ya hivi karibuni yaliotekelezwa na Pyongyang . Lakini inasema kuwa bwana Lavrov alisisitiza kwamba diplomasia ndio njia ya pekee ya kumaliza wasiwasi katika rasi ya Korea, na kutaka hatua zozote dhidi ya taifa hilo kusitishwa akionya huenda zikasababisha madhara yasiojulikana. Waziri wa ulinzi nchini Marekani amesisitiza kuwa bado kuna fursa ya kidiplomasia katika kukabiliana na Korea Kaskazini. Mapema rais Trump alichapisha ujumbe katika akaunti yake ya Twitter akisema mazungumzo sio suluhisho.

    Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania

    Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania Miaka 60 siku kama ya leo ugunduzi mkubwa ulifanyika katika eneo la Olduvai Gorge, kwenye kreta ya Ngorongoro. Wanaakiolojia Louis na Mary Leakey waligundua fuvu la mtu anayeaminika kuwa ni wa kale zaidi waliyompa jina la Zinjanthropus. Ugunduzi huo uliofanyika saa nne asubuhi Julai 22, 1959 kipindi hicho kwenye eneo la Tanganyika ulikuwa wa vipande zaidi ya 100 ukasaidia katika kutambua asili ya watu wa awali duniani. Kabla ya ugunduzi huo, wanasayansi na wanahistoria walikuwa wakiamini kuwa binadamu wa kale walitokea Uchina baada ya ugunduzi wa mafuvu ya kale baina ya 1923 na 1927 nchini humo ya Homo eractus, ama maarufu kama Peking Man. Mafuvu hayo ya Uchina yalikuwa na umri wa takribani miaka 750,000. Mafuvu ya Olduvai eneo ambalo kwa sasa lipo Tanzania wakati wa ugunduzi wake lilikuwa na umri wa takribani miaka milioni 1.75, na hakuna mabaki ya mtu wa kale zaidi ambayo mpaka sasa yamegundul...